kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,677
Jeshi la Polisi mkoani Mwanza sasa limeamua kutumia polisi wa kimataifa (Interpol) kuwasaka viongozi wawili wa dini wanaodaiwa kutorokea nchi za nje kukwepa kukamatwa kwa tuhuma za kurekodi kanda zenye maudhui ya uchochezi.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu, amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa viongozi hao ni kati ya viongozi watatu waliokuwa wanasakwa na jeshi hilo tangu Februari mwaka huu kwa tuhuma za kufanya uchochezi.
Aliwataja viongozi wanaosakwa na Interpol kuwa ni Askofu wa kanisa la Tanzania Field Evangelism maarufu kama kanisa la Kwa Neema anayedaiwa kutorokea nchini Marekani na Sheikh Irunga Hassan Kapungu, anayedaiwa kutorokea nchini India.
Hata hivyo alisema, Imam Hamza Omari ambaye alikuwa miongoni mwa viongozi watatu wa dini wanaosakwa na jeshi hilo tayari amekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kurekodi kanda za uchochezi wa kidini.
Kama mnavyofahamu tangu Februari mwaka huu tulikuwa tukiwasaka viongozi hawa kwa tuhuma za kufanya uchochezi, lakini wakawa wametoroka. Tulifanikiwa kumkamata mmoja, wengine wakawa wametoroka, lakini tumepata taarifa kwamba mmoja yupo Marekani na mwingine yupo India, hivyo tumeamua kutumia Interpol kuwasaka na kuwatia mbaronialisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Mangu, Sheikh Irunga Kapungu anatuhumiwa kurekodi kanda tatu tofauti zenye majina ya Rudisha Heshima ya Uislaam, Bakwata ni tawi la Kanisa, na Mauaji ya Kinyama ya Sheikh Abood Logo wa Mombasa ambayo pia ndani yake kuna maudhui yanayoelezea unafiki katika Sensa.
Aidha, alisema kwamba Askofu Mpemba anadaiwa kurekodi kanda yenye jina la Inuka Chinja Ule huku Imam Hamza anadaiwa kurekodi kanda yenye jina la Ndege wote walie, akilia bundi uchuro.
Kamanda huyo wa polisi mkoani Mwanza alisema kwamba kanda zote hizo zina maudhui yanayolenga kuchochea chuki kati ya dini moja dhidi ya nyingine na kati ya wananchi dhidi ya serikali yao.
Alisema kuwa mbali na kuwasaka watuhumiwa waliorekodi kanda hizo, jeshi la polisi pia limepiga marufuku usambazaji wake, na atakayebainika atakamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za uchochezi.
Alitoa wito kwa mtu yeyote mwenye kanda hizo kuzisalimisha polisi ifikapo Jumatatu ya Aprili 15, mwaka huu vinginevyo watakaokutwa nazo watahesabiwa kuwa wachochezi sawa sawa na waliozirekodi.
CHANZO: NIPASHE
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu, amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa viongozi hao ni kati ya viongozi watatu waliokuwa wanasakwa na jeshi hilo tangu Februari mwaka huu kwa tuhuma za kufanya uchochezi.
Aliwataja viongozi wanaosakwa na Interpol kuwa ni Askofu wa kanisa la Tanzania Field Evangelism maarufu kama kanisa la Kwa Neema anayedaiwa kutorokea nchini Marekani na Sheikh Irunga Hassan Kapungu, anayedaiwa kutorokea nchini India.
Hata hivyo alisema, Imam Hamza Omari ambaye alikuwa miongoni mwa viongozi watatu wa dini wanaosakwa na jeshi hilo tayari amekamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kurekodi kanda za uchochezi wa kidini.
Kama mnavyofahamu tangu Februari mwaka huu tulikuwa tukiwasaka viongozi hawa kwa tuhuma za kufanya uchochezi, lakini wakawa wametoroka. Tulifanikiwa kumkamata mmoja, wengine wakawa wametoroka, lakini tumepata taarifa kwamba mmoja yupo Marekani na mwingine yupo India, hivyo tumeamua kutumia Interpol kuwasaka na kuwatia mbaronialisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Mangu, Sheikh Irunga Kapungu anatuhumiwa kurekodi kanda tatu tofauti zenye majina ya Rudisha Heshima ya Uislaam, Bakwata ni tawi la Kanisa, na Mauaji ya Kinyama ya Sheikh Abood Logo wa Mombasa ambayo pia ndani yake kuna maudhui yanayoelezea unafiki katika Sensa.
Aidha, alisema kwamba Askofu Mpemba anadaiwa kurekodi kanda yenye jina la Inuka Chinja Ule huku Imam Hamza anadaiwa kurekodi kanda yenye jina la Ndege wote walie, akilia bundi uchuro.
Kamanda huyo wa polisi mkoani Mwanza alisema kwamba kanda zote hizo zina maudhui yanayolenga kuchochea chuki kati ya dini moja dhidi ya nyingine na kati ya wananchi dhidi ya serikali yao.
Alisema kuwa mbali na kuwasaka watuhumiwa waliorekodi kanda hizo, jeshi la polisi pia limepiga marufuku usambazaji wake, na atakayebainika atakamatwa na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za uchochezi.
Alitoa wito kwa mtu yeyote mwenye kanda hizo kuzisalimisha polisi ifikapo Jumatatu ya Aprili 15, mwaka huu vinginevyo watakaokutwa nazo watahesabiwa kuwa wachochezi sawa sawa na waliozirekodi.
CHANZO: NIPASHE