Nipo single, haya ni Matumizi yangu ya wiki moja - nipe ushauri

Nilivyoiona hiyo sadaka .. nimehisi unaimani kubwa kubwa, Naona nikuache na ulivyojipangia hayo mengine, Mungu anakuwezesha sana
Imani au ujinga ndiyo mana wachunga kondoo wamejawa viburi na kuishi maisha ya anasa kwa wajinga wajinga kama hawa!
 
Mkuu ww unajua kazi ya friji?
Kwa hiyo kazi ya fridge ni kuwekea nyanya na wali uliobaki!!?? Hizi ni akili za kimasikini siyo za mtu mwenye malengo ya kufanikiwa. Fridge ni anasa tena ya kipumbavu. Wewe unajua fridge kwa mwezi utatumia kiasi gani gharama za umeme kwa kuhifadhi dagaa na nyama,bidhaa ambazo kila siku zipo sokoni!??
 
Ninaongelea watu ambao tupo busy kweli kweli kupata huo muda wa kwenda kununua nyanya za mia 2 kila siku gengeni, unachukulia kuwa na fridge ni anasa?
Mkuu hebu acha kulisha watu matango pori!?? Km mtu unasema ana huo u busy huo muda wa kupika anautoa wapi!?? Yaani upate muda wa kupika halafu ukose muda wa kununua nyanya na nyama Dar es salaam hii!?? Huyu ni mpumbavu awala siyo mjinga. Na hizi ni akili za masikini..si unaona hata sadaka anatoa zaidi kuliko alizowapa ndugu!?? Huwezi kufanikiwa kwa mtindo huo wa maisha. Kama hana muda kiasi hicho kwa nn apike,si ale kwa mama lishe!?? Unanunua fridge kwa gharama kubwa,halafu unaongeza gharama za umeme kwa ajili ya kuweka wali wa shilingi elfu 1 uliobaki!!??
 
Sorry bro tukikuwa tunapeana uzoefu and plus jokes mkuu,wala sikumaanisha kejeli,kumradhi mkuu
 
Mimi matumizi yangu ya umeme natumia unit 2 tu kwa siku kuanzia friji pamoja na kuwasha taa ambazo gharama yake ni 500 tu kwa siku.sasa hapo Kuna hasara gani.
Punguza mawazo ya kikoloni ndugu yangu.
Ukisema friji linalosaidia kupata maji ya barid ya kunywa na vyakula visiharibike ni anasa,je television utasemaje?maana kazi ya tv ni kufurahisha macho tu na haizuii njaa.
 
hao ndugu wakijua unapeleka pesa yote sadaka wao unawapunja watakuroga
 
mkuu hii bajeti ni wiki moja kma nilivyo specify , cm bando hua naunga la mwez, maji na umeme vipo ndo maana.

Sinywi pombe ,sivuti sigara na nimesema kua nipo single ( sina demu)
Hahaha kama huna dem wala mke ni sawa endelea hvo hvo.
 
Haa naona mtumishi umeshaanza kuweka akiba yako mbinguni safi sana 75000tsh si mchezo kwa kweli,Mungu azidi kukubariki sawasawa na imani yako.
 
ha ha ha hilo life nimepitia dah ukipika mboga majani halafu kikifuata ugali unatoka na mamboga
 
Walokole bhana [emoji23][emoji23]
Sadaka utadhani umewahi kuongea na Mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…