Mkuu kabla ya kuanza kufanya biashara yoyote ni lazima ujitathimini ww mwenye kwanza katika nyanja zifuatazo:-
1) Biashara gani unaipenda?
2) Wateja wako ni kina nani?
3) Soko lake likoje?
4) Nani msimamizi wa biashara yako?
5) Je unashughuri gani mbali na biashara hii
NB: wakongwe watakuja kuongezea
kabla hujafanya chochote chukua million moja na upate elimu kuhusu biashara ndo uweze tumia hio million nne kufanya biashara yeyote utakayoona inakufaa
Nadhani ushauri mzuri ungeutoa hapa hapa ili kama una changamoto na waadau wengine wazitoe. Sina nia ya kudharau lengo lako lakini mtu kama huyu anaeanza ni vizuri ushauri ukawa wa wazi ili wadau wengine wakawa na nafasi ya kushauri maana unaweza ukamshauri kwa nia nzuri lakn kumbe huko ulikomshauri kuna changamoto zikapelekea kuzamisha mtaji wake wakati ingekua wazi wadau wengine wangeongezea pale ulipoishia na kusaidia zaidi.