Nisaidieni jamani hili tatizo la hedhi litaniua kwa mawazo

Joined
Jan 9, 2013
Posts
39
Reaction score
30
habari zenu wana Jamii F
jamani naombeni msaada kwa atakayeweza kunisaidia mie mwenzenu nasumbuliwa na tatizo ambalo lilianza tu ghafla mwaka 2006 yaani kutokwa damu bila mpangilio maalumu ni kwamba naingia mwezini kama kawaida ila nikikaa baada ya wiki mbili naaza pata spotting kila siku hadi inapokuja mwezi mwingine nimeshazunguka mahospitalini nimepima vipimo vyote sina kuanzia kansa wala kizazi hakionekani kama kina tatizo ovary zote nimeambiwa ni nzima na nimepima hospitali mbalimbali nilionekana nina goitre dokta akasema hiyo ndio inanizuru lakini hata baada ya kufanya operation sijaona badiliko lolote la kimwil hali ni ile ile walimwengu nisaidieni kwani nami nahitaji siku moja niwe mama wa familia hivi kwa hali hii itawezekana kweli au kwa anewajua wataalum nielekezeni tu ntaenda maana nakaribia kumaliza hosp kubwa zote za nchi hii . nITASHUKURU JAMANI KWA YEYOTE ATAKAYENISAIDIA USHAURI AU DAKTARI GANI MZURI NIKATIBIWE NAPATA SHIDA SANA NA HALI HII
 
je uliwahi kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango kama sindano,vidonge,vipandikizi? maana wengine huwa zinawasababishia effects kama hiyo miongoni mwa effects nyingi.ukipatikana ujibu sawa!
 
ulishawahi tembea na mume wamtu????????????????????????????????
 
pole sana kama uko dar jaribu kwenda kwenda kwa Dr ngwale hospitali yake iko posta inaitwa poly clinic karibu na tunakopesha au mkombozi bank
 
Asanteni sana kwa kunitajia hao madaktari nitajitahidi kuwatafuta maana atafutaye hachoki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…