Nisaidieni kimawazo

Nisaidieni kimawazo

msasa

Member
Joined
Nov 27, 2008
Posts
81
Reaction score
1
Nina ex-wife ambaye kwa mda mrefu mawasiliano yetu tunafanya kwa ajili ya mtoto wetu mpendwa ambaye anaishi nae yeye. Zaidi ya hapo akinipijia labda kwa shari tu ila hatuna mawasiliano zaidi ya hapo. Sasa jana kanipijia simu tena alikuwa mpole hadi nikashangaa alichoniambia kuwa alitaka kunisalimia tu nikamshukuru nikakata sim, nikawa nawaza manake haijawahi kutokea mara akapijia tena akanambia this week anaomba tuonane nikamwambia ntachek kama nitapata nafasi. Kwa sasa nina wife wangu mwingine mpendwa naishi nae. Sasa ushauri kutoka kwenu maanake ninajiuliza sana hasa nini anachoniitia ni heri au shari nisaidieni
 
Sisi hatuwezijua kama anakuitia shari au heri la msingi kubali wito but nenda na wifi na usisitize uwepo wake kwatika mazungumzo kwani hakuna siri kati yako na mkeo.
 
Du hapo mkuu usitie maguu kama unampenda huyu mkeo ulie nae sasa, anaweza akakutega mwishoe mkasau yaliyopita na kuganga yajayo.
 
Du hapo mkuu usitie maguu kama unampenda huyu mkeo ulie nae sasa, anaweza akakutega mwishoe mkasau yaliyopita na kuganga yajayo.

Unajuaje pengine hata hamwitii hayo anayojiwazisha. Wanasema kataa neno usikatae wito. Aende tu BUT aende na my wife wake wa sasa.
 
Hakuna ubaya wowote kuonana nae kwani ni mzazi mwenzako na vilevile katika uhusiano wenu kuna mambo mengi mliyofanyiana ambayo kila mmoja wapo kwa wakati wake huyakumbuka na hasa yale mazuri na yalioyokuwa yakiwafanya mfurahie mapenzi yenu.Nadhani amekumbuka ndio maana kwa upole kakubigia simu na kutaka muonane.
 
Unajuaje pengine hata hamwitii hayo anayojiwazisha. Wanasema kataa neno usikatae wito. Aende tu BUT aende na my wife wake wa sasa.
yes,,nenda lakini na mkeo. nyie ni wazazi na tena yawezekana amekumbana na magumu kwenye malezi ya mwanenu anahitaji mtu wa kushare naye, kuwa wazi kwa wife wako in every step, mshirikishe na awepo.
 
Kusitasita kwako tayari nishaona kwamba wewe una hali fulani ya natakasitaki!...Lakini
ukitaka kuishi vizuri na huyo bibie ndugu, simamakiume mwambie machoni jambo la ukweli bila kumwogopa. Kama ni mambo ya mtoto ni bora muelewane jinsi ya kulikabili, lakini si vyema kuitana konakona
 
Mkuu msasa wewe si mwanaume? nenda onana naye, ni mzazi mwenzio. nenda ukiwa na nia thabiti kuwa hakuna kukumbushia. zaidi zaidi ulizia kwa nini ameamua kukuita sasa na sio wakati uliopita.

Nisingeshauri uende na mkeo, kwa sababu naye hatakuwa huru kusema anachotaka kusema. atajisikia kidogo embarrased. Mkabili kiume ukishatoka hapo utapata jibu.
 
Hivi kwani mliachana katika mazingira gani? Ni wewe ulimwacha sababu ya uliyenaye au...,

Wito wake unategemea zaidi na jinsi mlivyoachana, kama bado anamapenzi nawe hapo ni majaribu sana ya kukutana naye kona. Wanawake wana kasumba sana.

Anaweza kuja kwako na kuwa mwingine kabisa ukasahau yaliyopita,atakubembeleza sana, ili tu akishakuweka kwenye line, maumivu yatabaki kwa mkeo na familia yako.

She is already a loser, nothing to worry, sasa kilichobaki huenda anataka kukuharibia na wewe. UENENDE KWA AKILI MAANA NI MJANJA KAMA NYOKA, ikibidi msikutane usiku, na wala mafichoni kama kweli unaipenda ndoa yako.

Kila la heri mkuu, we ndo kidume sasa angalia usiangushwe.


 
Nina ex-wife ambaye kwa mda mrefu mawasiliano yetu tunafanya kwa ajili ya mtoto wetu mpendwa ambaye anaishi nae yeye. Zaidi ya hapo akinipijia labda kwa shari tu ila hatuna mawasiliano zaidi ya hapo. Sasa jana kanipijia simu tena alikuwa mpole hadi nikashangaa alichoniambia kuwa alitaka kunisalimia tu nikamshukuru nikakata sim, nikawa nawaza manake haijawahi kutokea mara akapijia tena akanambia this week anaomba tuonane nikamwambia ntachek kama nitapata nafasi. Kwa sasa nina wife wangu mwingine mpendwa naishi nae. Sasa ushauri kutoka kwenu maanake ninajiuliza sana hasa nini anachoniitia ni heri au shari nisaidieni


Mzee, kilichowaachanisha hakiwezi kuwaunganisha kamwe, mawasiliano ya kawaida na ya wazi na mzazi mwenzio kuhusu mtoto/watoto ni kitu cha kawaida,lakini epuka sana kurudia mwanamke au mume mlieachana labda kama mazingira ya kuachana kwenu ni ya kawaida na wewe huna mke au mume mwingine.

Binadamu tumeumbwa wapole wa midomo, muonekano na mienendo yetu lakini roho zetu zinaficha siri kuu!.....hujui kwa nini anakutafuta na kwa ushauri tafadhali sana epuka kuwasiliana nae kwa sms au simu katika mazingira tata (unaelewa) kama mtoto anaishi nae ni bora ongea na mkeo wa sasa umchukue uishi nae wewe akue katika makuzi mazuri vinginevyo atakuvuruga ukose na huyo mke wa sasa........Kina mama wana mambo mzee,
kama unayajua vizuri maandiko matakatifu, kumbuka yaliyomfika ADAM kupitia EVA (HAWA) au SAMSONI yule mwanaume aliyekuwa na nguvu nyingi kwa DELILA,.viumbe wajinsi hii wapo wengine (sio wote) ni hatari sana....utajifunza mengi....anatafuta alichokipoteza muda mrefu huyo, ............lakini ukithubutu kumhurumia, huwezi tena kurejea kwenye hii JF kutueleza matokeo yake!
 
Wewe nenda kamsikilize ndio uje hapa utuambie kuwa amekwambia nini. Saasa unasita kama anataka mimba nyingine je?
 
Mkuu msasa wewe si mwanaume? nenda onana naye, ni mzazi mwenzio. nenda ukiwa na nia thabiti kuwa hakuna kukumbushia. zaidi zaidi ulizia kwa nini ameamua kukuita sasa na sio wakati uliopita.

Nisingeshauri uende na mkeo, kwa sababu naye hatakuwa huru kusema anachotaka kusema. atajisikia kidogo embarrased. Mkabili kiume ukishatoka hapo utapata jibu.
Jamani nyie wote mliomshauri aende na mkewe kwa huyo ex-wife wake mnaijua tabia au reaction ya mkewe au m,namsahuri na yeye anamwaga asante hapa tu? Wake wengine vichefu chefu nyie!! Haya nenda naye Bwana wewe ndio unajua
 
Mhhh sidhani kama itakuwa vizuri kwenda na mke wako wa sasa hivi...Hivi mfano umeenda nae hivi kweli ataweza kuongea kama jinsi inavyotakiwa??Mkubwa wewe mwanaume nenda na kamsikilize nini anasema ila ninachokushauri kwamba mchukue rafiki yako wa karibu usiende mwenyewe na ukifika pale usinywe kinywaji chochote kile......
 
Unajuaje pengine hata hamwitii hayo anayojiwazisha. Wanasema kataa neno usikatae wito. Aende tu BUT aende na my wife wake wa sasa.

MJO1, sidhani katika huu mwaliko mke wa sasa alikuwa included. Kwenda naye itakuwa ni kutafuta shari, lakini labda mama ana shida ambayo haihusiani na mtoto na anataka mwenzake amsaidie. Kwa maoni yangu nenda lakini kama unaitiwa nanihii...kazi kwako, Utajiju!
 
wewe nenda kamcheki:
nenda na mkeo wa sasa kama mkeo umemwambia na anajua kama una mtoto nje ya ndoa:
ukifika usiendekeze masihara na kumsikiliza anyoosh maelezo kwakile alokuitia:
fanya utaratibu wa kumchukua mtoto mara moja:
we nenda kaka wala usohofu, kama kawaida kaka si unajua halua haina kipolo??!!!!
 
Back
Top Bottom