Nisaidieni kiwawazo tumsaidie kijana mwenzetu

Nisaidieni kiwawazo tumsaidie kijana mwenzetu

blessing 18

Member
Joined
Jan 17, 2012
Posts
5
Reaction score
0
Nina rafiki yangu ameoa na anawatoto wawili. Tatizo mke wake anamdharau sana hamsikilizi kwa lolote lile. Wakati mmewake anawatunza yeye pamoja na ndugu zake. Ukiangalia kaka huyu hana ndugu kwani wazazi wake walifariki toka akiwa na umri mdogo akalelewa na watu baki na si ndugu zake, alipomaliza masomo na kupata kazi akaamua kuoa ili aweze kufarijika matokeo yake amezidi kujiongezea matatizo

Rafiki yangu huyu anataka akimbilie nje ya nchi amwachie mwanamke nyumba na watoto.

Naleta kwenu swala hili tusaidiane
 
Nina rafiki yangu ameoa na anawatoto wawili. Tatizo mke wake anamdharau sana hamsikilizi kwa lolote lile. Wakati mmewake anawatunza yeye pamoja na ndugu zake. Ukiangalia kaka huyu hana ndugu kwani wazazi wake walifariki toka akiwa na umri mdogo akalelewa na watu baki na si ndugu zake, alipomaliza masomo na kupata kazi akaamua kuoa ili aweze kufarijika matokeo yake amezidi kujiongezea matatizo

Rafiki yangu huyu anataka akimbilie nje ya nchi amwachie mwanamke nyumba na watoto.

Naleta kwenu swala hili tusaidiane

Kukimbia matatizo/changamoto ni uoga,..mwambie apambane akiona vip aachane na huyo mwananmke lakini sio kukimbia tena unakimbia nchi kabisa,...ni sawa na mtu ambaye akipatwa na tatizo anakimbilia kujinyonga.
 
Akimbie? Anamuogopa huyo mwanamke? Hua anapigwa?

Kama anaona hawezi kuendelea kuishi nae tena amwache aanze upya. . . hamna haja ya kukimbia, unless kuna kitu kibaya anapanga kufanya kabla hajakimbia.
 
Badala akimbilie ndani yeye anataka kukimbilia nje?
Mwambie nje kuna simba watamla.
 
hivi kumbe kuachana na mtu ni ngumu hivi?
stuka ,tulia weka sawa implement mfumo dume.
awe mean and rude.....source; kongosho.
 
Nina rafiki yangu ameoa na anawatoto wawili. Tatizo mke wake anamdharau sana hamsikilizi kwa lolote lile. Wakati mmewake anawatunza yeye pamoja na ndugu zake. Ukiangalia kaka huyu hana ndugu kwani wazazi wake walifariki toka akiwa na umri mdogo akalelewa na watu baki na si ndugu zake, alipomaliza masomo na kupata kazi akaamua kuoa ili aweze kufarijika matokeo yake amezidi kujiongezea matatizo

Rafiki yangu huyu anataka akimbilie nje ya nchi amwachie mwanamke nyumba na watoto.

Naleta kwenu swala hili tusaidiane

Sasa kwani ukisema ni wewe tutakudharau?

OK!! By the way, yanini kukimbia? achana nae, muachie hiyo nyumba na watoto, yanini kujitia presha? Ukisha mtema haina haja ya kuoa tena wachana na haya mapresha ya maisha, utajitesa bure kisha upunguze muda wako wa kuishi.
 
Kukimbia matatizo ni kujiongezea matatizo njia nzuri ni kutafuta suluhisho.
Mwambie aongee na mkewe kuhusiana na hilo jambo. Ikishindikana aongee na wazee wa mke wake au viongozi wake wa dini wajadili hayo matatizo yao.
Mwisho vyote vikishindikana, aachane na mkewe alee watoto wake yeye mwenyewe kwani ameshindikana huyo mke.
 
Kwani aliambiwa asimuache Hata Kama anataka kumtoa roho? Mwambie ajikaze kiume amalize tatizo,yeye ameoa hakuolewa....
 
kwani kaoa au kaolewa? ASTOPISHE MISAADA YOTE KWA NDUGU WA MKE NA MATUMIZI YA MKE AYAPUNGUZE SANA,
 
Akimbie!! Mwambie afanye uchunguzi huenda kuna fahari mwingine anayeendesha kichwa cha mkewe kwa remote. Mwambie awe mwanaume ;awe tayari kufanya maamuzi magumu.

Huenda mkewe ameshajua udhaifu wake wa kufanya maamuzi ndo maana anatingisha kiberiti.
 
mpe pole mwambie aende ustawi wa jamii akatoe malalamiko yake
 
Mwambie dogo aowe mke wa pili tu hio ndo dawa ya wanawake.
kama dini inaruhusu aoe mke wa pili,huyo mke wake lazima ataulie,na kama dini yake hairuhusu,atafute kimada wa nje,ili atulizie mawazo huko,huyo wife wake akihisi kuwa jamaa ana kimada,lazima arudishe adabu yake
 
Duh!MWANAUME hayuko kama huyu:source Aspirin
 
kama dini inaruhusu aoe mke wa pili,huyo mke wake lazima ataulie,na kama dini yake hairuhusu,atafute kimada wa nje,ili atulizie mawazo huko,huyo wife wake akihisi kuwa jamaa ana kimada,lazima arudishe adabu yake
Dini gani isio ruhusu uowe mke wa pili?? Hao si wanamzulia Yesu uwongo tu.
 
akikimbia atakuwa hajasolve tatizo mshauri akae chini na mkewe wazungumze ikiwezekana awashirikishe waliomsimamia ndoa yake kupata suluhu
 
Back
Top Bottom