Mashine: Zipo za umeme na za kufyatua kwa mkono, sijui unapendelea ipi kati ya hizo? Za umeme utapata matofali mengi zaidi kwa siku tofauti na ya mkono, faida nyingine ya mashine ya umeme inapunguza idadi ya vibarua, wanabaki wa kuchanganya zege, na kubeba tofali kuzipanga eneo lake baada ya kufyatuliwa..
Changamoto: Kuna wakati wateja wanapungua, unaweza kaa na matofali kwa muda mrefu usifanye kazi, hii inasababishwa na wateja kufulia hivyo shughuli za ujenzi kusimama, hali inayoweza kusababisha upunguze wafanyakazi.
Faida: Itategemea eneo ulilopo, na ushindani wa kibiashara uliopo eneo husika..
Gharama za uendeshaji: Itategemea na idadi ya wafanyakazi/vibarua ulionao, kwasababu ni mgeni, vyema ukawa na vibarua wachache ili kupunguza gharama, kama ukitumia mashine ya umeme pia utatakiwa kununua umeme.
Uendeshaji: Hapa ujipange, hakikisha unaemuweka kusimamia awe mwaminifu kwako, hasa kuhesabu mifuko ya cement iliyotumika kwa siku, na idadi ya matofali yaliyofyatuliwa.
Tahadhari: Hakikisha eneo unalofungua mradi pawepo na shughuli nyingi za ujenzi maeneo ya jirani, zitakazokuwezesha kutotegemea wateja wachache, hawa wauzaji unaowaona huku mjini, wengi wana wateja wao, ambao huchukua matofali na kuyapeleka maeneo ya ujenzi kwa makubaliano fulani, ikiwemo kupunguziwa bei, kitu ambacho kwako mgeni itakuwa ni hasara.
NB: Niko karibu na wauza cement so hao jamaa wa kufyatua matofali pia ni wateja wa cement, story nao huwa zinapigwa.
Taarifa nyingine nitaongezea, kama idadi ya mifuko inayotumika, na idadi ya matofali unayofyatua kwa siku kwa mashine ya umeme, na mashine ya mkono, na kiasi cha umeme ambacho mashine ya kufyatua kwa umeme inakula kwa siku.