msani
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 1,801
- 1,191
habari zenu wana mmu.
leo nimekutwa na tukio ambalo sijajua tatizo ni nini na nifanye,
nina gf wangu ambaye kwa sasa yuko kwao nje ya mkoa,na kipindi fulani tulikuwa na matatizo ya mawasiliano baina yetu maana alikuwa hapokei simu mara nyingi ninapompigia,baadae nikaanza kuhisi huenda ana jamaa huko.Tukakwaruzana na baadaye tukasuruhisha na tatizo la simu likapungua kwa asilimia kubwa.Nilikuwa nafahamiana na mdogo wake na muda mwingi nilikuwa naongea naye akinipigia kwani mie kupiga mara kwa mara niliona sio vizuri na inaweza hatarisha mahusiano yetu.Huyu mdogo mtu akawa ananiambia mara kwa mara kuwa huyu mwenzangu sio mwaminifu kwangu anapokuwa nyumbani na akanikumbusha mgogoro wa simu na kuwa kuna jamaa ambapo si mmoja huwa anamtoa mara nyingi na kurudi nyumbani usiku wakati mwingine hata saa sita usiku.Kuna siku aliniambia kuwa jana dada alitoka na jamaa na kurudi saa tano usiku lkn mie mara nyingi takribani kila siku tunaongea naye na ananiambia yuko nyumbani usiku huo,nikakasirika sana baada ya kuambiwa na mdogo mtu hiyo taarifa ila nikajisemea moyoni nisifanye pupa.Leo 5/11/2011 saa 3 usiku mdogo mtu akanipigia simu tukaongea tu kwa muda wa dk 15 na baadae mada ya dada ikagusiwa nami nikataka kujua zaidi,akanisimulia halafu akasema hata leo hayupo nyumbani na ametoka na jamaaa fulani.kijana jazba ikanipanda na kwa kuwa natumia simu 2 nikapiga na simu ya pili huku tukiongea na mdogo mtu,uzuri gf wangu akapokea simu na kumuuliza kama ananipenda na akajibu ananipenda,nikamuuliza tena mara ya pili akaanza kulia,ndipo nilipomuuliza yuko wapi na akaniambia yuko nyumbani na akawa amepaniki na kumuita modgo wake ili nithibitishe kama ni kweli niko home na akamuita mdogo kwa sauti ya juu na huku nikisia,nikakata simu ya mdogo mtu,baadaye gf wangu akaniambia huyu hapa ongea naye,nikazuga kidogo kisha akampa gf wangu simu huku akilia sana kwa swali nililomuuliza na kumtuhumu kuwa hayuko nyumbani.
sasa nimeshindwa kuelewa nini kinaendelea na lipi ni kweli maana leo gf alikuwa nyumbani na nimeambiwa kuwa ametoka na nifanyeje angalau niweze kujua ukweli kwani mi niko mbali kwani nashindwa tena kumwamini mdogo mtu, na nahisi naibiwa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
leo nimekutwa na tukio ambalo sijajua tatizo ni nini na nifanye,
nina gf wangu ambaye kwa sasa yuko kwao nje ya mkoa,na kipindi fulani tulikuwa na matatizo ya mawasiliano baina yetu maana alikuwa hapokei simu mara nyingi ninapompigia,baadae nikaanza kuhisi huenda ana jamaa huko.Tukakwaruzana na baadaye tukasuruhisha na tatizo la simu likapungua kwa asilimia kubwa.Nilikuwa nafahamiana na mdogo wake na muda mwingi nilikuwa naongea naye akinipigia kwani mie kupiga mara kwa mara niliona sio vizuri na inaweza hatarisha mahusiano yetu.Huyu mdogo mtu akawa ananiambia mara kwa mara kuwa huyu mwenzangu sio mwaminifu kwangu anapokuwa nyumbani na akanikumbusha mgogoro wa simu na kuwa kuna jamaa ambapo si mmoja huwa anamtoa mara nyingi na kurudi nyumbani usiku wakati mwingine hata saa sita usiku.Kuna siku aliniambia kuwa jana dada alitoka na jamaa na kurudi saa tano usiku lkn mie mara nyingi takribani kila siku tunaongea naye na ananiambia yuko nyumbani usiku huo,nikakasirika sana baada ya kuambiwa na mdogo mtu hiyo taarifa ila nikajisemea moyoni nisifanye pupa.Leo 5/11/2011 saa 3 usiku mdogo mtu akanipigia simu tukaongea tu kwa muda wa dk 15 na baadae mada ya dada ikagusiwa nami nikataka kujua zaidi,akanisimulia halafu akasema hata leo hayupo nyumbani na ametoka na jamaaa fulani.kijana jazba ikanipanda na kwa kuwa natumia simu 2 nikapiga na simu ya pili huku tukiongea na mdogo mtu,uzuri gf wangu akapokea simu na kumuuliza kama ananipenda na akajibu ananipenda,nikamuuliza tena mara ya pili akaanza kulia,ndipo nilipomuuliza yuko wapi na akaniambia yuko nyumbani na akawa amepaniki na kumuita modgo wake ili nithibitishe kama ni kweli niko home na akamuita mdogo kwa sauti ya juu na huku nikisia,nikakata simu ya mdogo mtu,baadaye gf wangu akaniambia huyu hapa ongea naye,nikazuga kidogo kisha akampa gf wangu simu huku akilia sana kwa swali nililomuuliza na kumtuhumu kuwa hayuko nyumbani.
sasa nimeshindwa kuelewa nini kinaendelea na lipi ni kweli maana leo gf alikuwa nyumbani na nimeambiwa kuwa ametoka na nifanyeje angalau niweze kujua ukweli kwani mi niko mbali kwani nashindwa tena kumwamini mdogo mtu, na nahisi naibiwa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!