Nisaidieni sheria nipate malimbikizo yangu nssf?

MASHIRI

New Member
Joined
Mar 16, 2013
Posts
3
Reaction score
0
<strong>Jamani wadau wa sheria naombeni msaada!<br>Mi nimekua mfanyakazi wa kuajiliwa shirika fulani hapa TANZANIA yapata miaka 8 lakini nimeamua kuacha kazi mwezi ulioisha ili niendelee na maisha mengine. katika mwezi wote huo nimejaribu kufuatilia barua ya kuacha kazi nimekua nikizungushwa kwa madai ya kwamba nimeacha kazi kati kati ya mwezi kwahiyo nimeipa hasara kampuni, sikufahamu kama sheria inasemaje&nbsp; juu la swala la kuacha kazi&nbsp; ni lazima iwe mwisho wa mwezi au&nbsp; la!nilipambana nikapewa barua lakini sasa kuna lingine ambalo ni zito sana kwangu. Ndugu msomaji nimeenda kupeleka barua yangu NSSF nikaangalia na mafao yangu nimekuta MWAJIRI wangu ameweka 20% ya fedha zangu kwa miaka yote nane. Naombeni msaada wenu nifanyeje maana NSSF wameniambia tarehe 04/06/2013 niendee check yangu ya hiyo 20%. Naombeni msaada wenu wadau mnisaidie nipate mafao yangu yote 100%.<br>&nbsp;&nbsp; Naomba sana msaada wenu ni harakati za ukombozi kjwangu na kwa wengine wenye matatizo kama yangu.<br></strong>
 
Pole sana ndugu yangu, me cna wenyeji na haya mambo, ngoja wanasheria waje hapa watakueleza tuu.
 
Wakati mwingine watu wanashindwa kutoa ushauri kutokana na habari kukosa credibility. Nijuavyo mimi ukiacha kazi unasubiri MIEZI SITA ndipo unaweza kudai mafao wala siyo malimbikizo kama unavyoita wewe. Sasa wewe umeacha kazi mwezi uliopita i.e February, leo machi tayari umeshapeleka madai na kuahidiwa hundi! Anyway labda kwa kujifunza tu as a case study. Hata hivyo fafanua 20% ya nini? Monthly salary? Maana mashirika mengi mwajiri anachangia 10% na mwajiriwa 10% ambayo inaleta 20%. Kama unazungumzia mwajiri wako kushindwa kuwasilisha makato yako kwa mwezi i.e amewasilisha 20% tu ya kile alichopaswa kuwasilisha kwa miaka 8, nenda NSSF wakupe statement yako kuanzia ulipoajiriwa. Ukiipata mwandikie barua mwajiri wako ukimweleza juu ya tatizo hilo. Ambatisha vivuli vya barua yako ya kuajiriwa na kukubaliwa kuacha kazi, salary slip ya kwanza kabisa na mwisho kabisa . Nakala peleka TIRA, NSSF na kwangu kama hutajali
 
Yani 20% namaanisha ameweka 20% ya mafao yangu yote.
 
Kwa ninavyojua mimi stahili yako ni 20% yaani 10%kutoka kwako na 10% inatoa kampuni, labda ufafanue vizuri maana hatujakuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…