Nisaidieni wana JF

Nisaidieni wana JF

Suzzie

Member
Joined
Feb 25, 2009
Posts
98
Reaction score
12
Kuna trip ya kwenda kigali mwezi wa nane kwa ajili ya mkutano wa kidini. tumeambiwa tubebe bidhaa za kitanzania ambazo tunaweza kwenda uza huko. naomba ushauri wenu nipeleke nini?
 
Jaribu kuchukia masai shuka.....shanga......vitu vya asili ya Kitanzania......sandals zile zenye shanga........etc....
 
Jaribu kuchukia masai shuka.....shanga......vitu vya asili ya Kitanzania......sandals zile zenye shanga........etc....

Asante Preta, na wengine wote japo wengine wanaleta utani.
 
Jaribu kuchukia masai shuka.....shanga......vitu vya asili ya Kitanzania......sandals zile zenye shanga........etc....

Dr tamaduni zetu na wao karibu zinafanana haswa kwenye hizo bidhaa ndogondogo za kitamaduni...

Mwaka jana nilipata kupita kwenye banda la Wanyarwanda pale sabasaba, nikakutana na vitu vingi tu vya kitamaduni kama ambavyo vinauzwa Soko la vinyago Mwenge(Dar), au hapo Arusha opposite na ofisi za Mkuu wa Mkoa(sijui kama lile soko bado lipo)...
 
Jaribu kuchukia masai shuka.....shanga......vitu vya asili ya Kitanzania......sandals zile zenye shanga........etc....

Kwa nini achukie hivo vitu, vina tatizo gani?
 
Mnanichekesha nyie wanajf. Mwaya Suzzie hebu tusubiri wenye info kama akina malila wanaojua kila kona.Ukienda wasalimie 'kwetu pazuri'
 
Handbags, sandals, mashati ya kiume, vikoi na vipochi vidogo vya mkononi vilivyorembwa kiafrika
 
kama unaenda kwa ajili ya dini fanya dini, kama unaenda kibiashara fanya biashara ila ukichanganya mara zote biashara itaimeza dini na kama ni dini ndio kusudio hutaambulia kitu
 
kama unaenda kwa ajili ya dini fanya dini, kama unaenda kibiashara fanya biashara ila ukichanganya mara zote biashara itaimeza dini na kama ni dini ndio kusudio hutaambulia kitu

Tajiri sana, naenda kidini ila siku ya mwisho kutakuwa na maonyesho ndiyo maana tumeshauriwa kubeba bidhaa zetu za kitanzania. najua sitaambulia patupu.
 
Back
Top Bottom