Nisamehe kaka, sikupenda kukutafuta lakini ni hali ya shida na dhiki vilinijaa

Nisamehe kaka, sikupenda kukutafuta lakini ni hali ya shida na dhiki vilinijaa

Joined
Apr 4, 2024
Posts
25
Reaction score
105
Kaka ni miaka miwili Sasa hatuja wasiliana

Nilikukera Sana kwa simu za mara kwa mara . Nisamehe bro Kuna hali nilikua napitia iliniumiza Sana
Lkn bro kwanini ulinitafuta na kutaka kujua mipango yangu ili unisaidie?

Bro leo nimeamini mtegemea cha ndugu hufa masikini

Niliweka tumaini kwako lkn haikua kama ulivyoniahidi

Nisamehe bro kwasababu nilikusumbua Sana ...ujumbe wako wa mwisho kwangu uliniambia una mambo mengi unasomesha .

Bro sikupenda kukutafuta lkn ni hali ya shida na dhiki vilinijaa

Leo nimekukumbuka bro 😥 nakusalimia
 
Kama mligombana omba msamaha. Unajua kitu ambacho watu wengi hawakijui ni kwamba kila unachokiona kwako ni changamoto hapo ndio ilipokuwa shule yako yakujifunza juu ya jambo hilo.

Sasa wengi hawataki kujifunza kupitia makosa yao wanataka kujifunza kupitia wengine, na hali kama hiyo ndio maana halisi ya mtihani

Fikiri mwenzako katika mtihani ya true & false yeye kaweka false wakati jibu ni true sasa wewe makosa yake si ufaulu wako,? Na ndiyo maisha yalivyo kila mmoja lazima ajibu mtihani wake mwenyewe na hakuna wakumsaidia mwenzake. Ukiona umefeli katika maisha, usipeleke lawama sehemu yeyote maana mtihani ulikuwa wakwako na wewe ndio ulioujibu na hakuna haja yakumlaumu mtu katika mtihani ulioufanya mwenyewe
 
Kaka ni miaka miwili Sasa hatuja wasiliana

Nilikukera Sana kwa simu za mara kwa mara . Nisamehe bro Kuna hali nilikua napitia iliniumiza Sana
Lkn bro kwanini ulinitafuta na kutaka kujua mipango yangu ili unisaidie?

Bro leo nimeamini mtegemea cha ndugu hufa masikini

Niliweka tumaini kwako lkn haikua kama ulivyoniahidi

Nisamehe bro kwasababu nilikusumbua Sana ...ujumbe wako wa mwisho kwangu uliniambia una mambo mengi unasomesha .

Bro sikupenda kukutafuta lkn ni hali ya shida na dhiki vilinijaa

Leo nimekukumbuka bro 😥 nakusalimia

inatokea sometimes kwenye maisha kuna watu wanajitokeza kama kuku chora ulipokwama kimaisha na kupotea katika mazingira ya ukimya, hadi pale unapogundua si vyema kutilia maanani ahadi za binadamu
 
Mkuu Asante kwa kinielewa
mimi sikumuomba msaada yeye ndo alinitafuta
Mkuu pole sana, iliwahi kunikuta kipindi fulani mwaka jana. Nlipigiwa sim na rafiki yangu mKenya (ambae hatukutafutana kwa kipindi kirefu) akiniahidi kuna tender ya ujenzi kaipata na nijiandae kwenda huko muda wowote tukashirikiane ujenzi. Ila cha ajabu alikaa kimya pasipo majibu kwa miezi kadhaa....mpaka pale nlipokuja kugundua amepost tiktok tender kashaifanya na anajinadi kwa kufanikisha....... "ahadi pekee ya kuzingatia ni ya Mungu na si mwanadamu"
 
Hii ilinitokea mimi, sister yupo shirika la umma mi nipo nipo tu sina mishe ya kueleweka

Katika moja na mbili nikawa namwambia anipige tafu mdogo wake akawa ananiambia majukumu yake

Siku akaniambia anaenda kukopa milions kadhaa ili anunue gari, nikamwambia usinunue gari fungua kitega uchumi kiwe kinakuingizia pesa akanipuuza
Kanunua gari, kafanya na mambo kadhaa pesa imekata

Akabaki na deni, kalipa deni kamaliza nikamwambia nikopee 3 mil kisha ntakuwa nakulipa kila mwezi au kama huniamini nifungulie ofisi nitakuorodheshea vitendea kazi ninavyovihitaji niwe napiga kazi jioni utakuwa unapitia hesabu kisha mimi utanifikiria, pia haikumuingia

Nikasema isiwe kesi mi mwanaume na nipo tayari kufa nikiwa natafuta kwa njia halali (kipindi hicho anamaliza deni nilikuwa napiga mishe kiwandani nalipwa 169k kwa mwezi)

Nikakaza nikawa napiga overtime kwa mwezi nikawa naambulia 220k take home

Huku kitaa kuna mwana (RIP) alinipa laptop baada ya kuona nipo fresh kwenye mambo ya IT, nikawazaaaa nikaona huu mshahara hapa kiwandani siwezi kutoboa zaidi ya kuishia kwenye kula na kulipa kodi ya chumba

Nikazama Dubai ya Dar kuulizia tool nakuta 325k, nikacheki AliExpress nakuta 180k nikajilipua kuagiza (nikasema ntajua ntaishi vipi maana nilibaki na 40k tu) baada ya mwezi nikatumiwa sms na posta nikachukue mzigo wangu


Nikasema sasa tayari Laptop ninayo na Tool ya kuanzia maisha tayari ninayo, nini kifuatacho, ni kuacha kazi yes naachaje sasa?
Maana nikiandika barua ya kuacha kazi nitakosa stahiki zangu na PPF pia watanizingua

Nikasema ngoja niwazingue mabosi wanifikishe kwa HR ili wanitimue kazi ofcoz hili wazo likapita, nikawazinguaaaa mwisho wa aiku wakajaa mpaka kwenye vikao vya utovu wa nidhamu nikawa nawajibu shit

Wakaafikiana wanifukuze, hapo mimi siwazi maana nauamini uwezo wangu, pili nimeshapoteza 4 yrs sioni la maana nililifanya, nikasema ntajua mbele ya safari

Siku ya siku nikalimwa barua ya kuachishwa kazi then wakanipa kama 700k hivi nikasema fresh maana hata wasingenipa nilikuwa nna uhakika wa kutoboa maana nilishajipanga

Mtu mzima kiroho safi bila connection nikazama Dubai ya Dar kuanza kupambana

Nikapambana kama wiki mbili tu tabia yangu ya uaminifu na uwezo wangu katika kazi vikanifanya nipate goli

Kuanzia hapo mambo yakawa bam bam

Sa hivi mimi ndo nampiga tafu sister japo yeye bado yupo serikalini ila anakwamaga, maana anapokea mshahara wa digit 7 ila akishakatwa madeni anabaki na bajeti ya kula tu na hapo anasomesha watoto watatu

Kimoyo moyo najisemea wee ngoja siku ukinikalia vizuri nitakufundisha namna ya kutumia mikopo
 
Hii ilinitokea mimi, sister yupo shirika la umma mi nipo nipo tu sina mishe

Katika moja na mbili nikawa namwambia anipige tafu mdogo wake akawa ananiambia majukumu yake

Siku akaniambia anaenda kukopa milions kadhaa ili anunue gari, nikamwambia usinunue gari fungua kitega uchumi kiwe kinakuingizia pesa akanipuuza
Kanunua gari, kafanya na mambo kadhaa pesa imekata

Akabaki na deni kalipa deni kamaliza nikamwambia nikopee 3 mil kisha ntakuwa nakulipa kila mwezi au kama huniamini nifungulie ofisi nitakuorodheshea vitendea kazi ninavyovihitaji niwe napiga kazi jioni utakuwa unapitia hesabu kisha mimi utanifikiria, pia haikumuingia

Nikasema isiwe kesi mi mwanaume na nipo tayari kufa nikiwa natafuta kwa njia halali (kipindi hicho napiga mishe kiwandani nalipwa 169k kwa mwezi)

Nikakaza nikawa napiga overtime kwa mwezi nikawa naambulia 220k takehome

Huku kitaa kuna mwana (RIP) alinipa laptop baada ya kuona nipo fresh kwenye mambo ya IT, nikawazaaaa nikaona huu mshahara hapa kiwandani siwezi kutoboa zaidi ya kuishia kwenye kula na kulipa kodi ya chumba

Nikazama Dubai ya Dar kuulizia tool nakuta 325k, nikacheki AliExpress nakuta 180k nikajilipua kuagiza baada ya mwezi nikatumiwa sms na posta nikachukue mzigo wangu


Nikasema sasa tayari Laptop ninayo na Tool ya kuanzia maisha tayari ninayo, nini kifuatacho, ni kuacha kazi yes naachaje sasa?
Maana nikiandika barua ya kuacha kazi nitakosa stahiki zangu na PPF pia watanizingua

Nikasema ngoja niwazingue mabosi wanifikishe kwa HR ili wanitimue kazi ofcoz hili wazo likapita, nikawazinguaaaa mwisho wa aiku wakajaa mpaka kwenye vikao vya utovu wa nidhamu nikawa nawajibu shit

Wakaafikiana wanifukuze, hapo mimi siwazi maana nauamini uwezo wangu, pili nimeshapoteza 4 yrs sioni la maana nililifanya, nikasema ntajua mbele ya safari

Siku ya siku nikalimwa barua ya kuachishwa kazi then wakanipa kama 700k hivi nikasema fresh maana hata wasingenipa nilikuwa nna uhakika wa kutoboa maana nilishajipanga

Mtu mzima kiroho safi bila connection nikazama Dubai ya Dar kuanza kupambana

Nikapambana kama wiki mbili tu tabia yangu ya uaminifu na uwezo wangu katika kazi vikanifanya nipate goli

Kuanzia hapo mambo yakawa bam bam

Sa hivi mimi ndo nampiga tafu sister japo yeye bado yupo serikalini ila anakwamaga, maana anapokea mshahara wa digit 7 ila akishakatwa madeni anabaki na bajeti ya kula tu na hapo anasomesha watoto watatu

Kimoyo moyo najisemea wee ngoja siku ukinikalia vizuri nitakufundisha namna ya kutumia mikopo
Hongera

Hata na hivyo una moyo kwakweli!
 
Hongera

Hata na hivyo una moyo kwakweli!
Mkuu, maisha haya,

niliwahi kupitia kipindi kigumu hadi nikatamani kujiua,

sema nilishajiapiza tangu kipindi nipo kidato cha pili(maana nilikuwa nasoma kwa shida sana) kwamba nife nikiwa kwenye harakati za utafutaji
 
Back
Top Bottom