Nisha Atumia Mbinu Za Wema Sepetu Kumnasua Ney Wa Mitego?!? Amwanza Rasmi!!!

Ibrahim300

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2010
Posts
390
Reaction score
68
Baada ya kupigana ili kupinga tetesi kuwa aliavya mimba, Nisha sasa amejeuza gemu kwa kumkumbuka mpenzi wake wa zamani, Ney wa Mitengo.

Staa huyu aliweza kufanywa upelelezi na mapaparazi ambao wako chini ya mwavuli wa GPL na kupitia mawasiliano ya simu ya mkononi, iligundulika kuwa Nisha anatamani penzi la Ney.

Ilikuwaje?
Mdaku ambaye anauhusiano wa karibu na mastaa hao wawili aliweza kuvuja meseji zote za simu ambazo zilikuwa wakiwasiliana nazo na kumfikia paparazi wa gazeti la GPL.

Kupitia hizo meseji, inasemekana kuwa Nisha ametumia mitindo flani ya mitego kumnasa Ney Mwenyewe.

Baada ya kuzinasa meseji hizo paparazi wa GPL aliingia mzigoni kuwasaka mastaa hao ili kujua kama wana mpango wa kurudiana.

Wa kwanza kupatikana alikuwa ni Nisha ambaye alisema: “Dah, ni kweli ninawasiliana na Nay kama rafiki wa kawaida tu.

“Nay ana demu wake na mimi nina bwana wangu.”

Kwa upande wa Nay wa Mitego alipata kigugumizi kidogo kulizungumzia hilo lakini akakiri kupata meseji hizo za mitego lakini akadai hakuna kinachoendelea kati yao.

Wema Alimshauri Nisha jinsi ya kunasua waume nini?


Stori imedondoshwa kutoka
Nisha Atumia Mbinu Za Wema Sepetu Kumnasua Ney Wa Mitego?!? Amwanza Rasmi!!! -bkuHABARI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…