Nishaurini nisiumie tena jamani..

MKAROLINA

Member
Joined
Feb 26, 2011
Posts
58
Reaction score
8
Habari za hasubuhi wana JF!Mapenzi jamani yanaumiza sana. Nina mpenz wangu ki ukweli nina mpenda sana ila juzi juma mosi kimetokea kisa kimoja. Niliingia kazini juma mosi hasubuhi na ilipofika lunch time nilimpigia cm na kumsalimia... tulisalimiana na kuendelea na mazungumzo yetu. Baadae nikamuaga na kukata cm ili niendelee na kazi. Kwa vile napmpenda mpenz wangu ambae tunatarajia tuwe wachumba Mungu akijalia nilimpigia tena cm saa kum jion nikiwa bado niko kazini nikamwambia kama ningewah kutoka ningeenda kumtembelea kwan tupo mbali kidogo kama kuvuka wilaya moja na nyingine kwan J 2 (sunday) nisingeingia kazini.. akafurah sana akaniambia ananitegemea nikamwambia kama nitapata gari nitakuja..Nikatoka jion kazini nikawa nimekosa usafiri nikampigia cm na kumueleza kuwa magari kwa sa hiyo sitoweza kupata kwan ilikuwa ni saa 12:20 pm kwa vile tayari alikuwa na shauku ya kuniona akaniambia ngoja anitafutie usafir then atanipa no za hyo dreva ili anichukue.. nikamwambia poa.. baada ya kama dakikia tano akaniambia nifanye faster gari linanifuata ila kwa upes zaid. Ki ukweli nilikuwa sijamaliza kujiandaaa nikamwambia 'Baby bado namalizi kujiandaa kama nitamchelewesha basi aende tu'' Mpenz akachukia na kukata cm.. baadae akapiga cm na kuniambia kama umegoma kuja sawa.Mpenz akawa amechukia hakunipigia cm na co kawaida yake mpaka ilipofika saa 09:30pm akaniambia yupo kwenye gari anaelekea CLUB, nikamwambia Baby mbona hukuniambia kama unaenda mpaka upo kwenye gari ndo unaniambia? akajibu kuwa uliniudh.. Bas mtot wa kike nikamwambia poa... Akiwa Club akanipigia cm tukaongea na baadae akanipigia ila kutokana na kelele za Club hatukuwa tunaelewana. Ilipofika saa 00:00am nikazima cm na kulala.J 2 nikaamka saa 08:10am nikawasha cm akanipigia akaniuliza mbona nilizima cm maana alinitafuta sana hakunipata nikamwambia nililala... Bas akawa bado ana hasira hatukuongea sana akakata cm. Ilipo fika saa 09:15am akapiga cm akaniuliza nina ratiba gani nikamwambia nipo nataka baadae niende saloon akasema poa.. Hazikupita dakika tano akapiga tena na kuniambia ana nguo chafu kama ningeweza ningeenda kumsaidia kufua... nikamwambia poa ngoja nipande gari nije... nikajiandaa nikapanda gari nikaenda... nikiwa kwenye gari akanipigia akaniuliza nimefika wapi nikamwambia na nikamwambia anisaidie kuloweka hizo nguo ili nikifika nifue kwan ingebid kurudi the sama day coz J 3 natakiwa kuingia kazini... akasema sawa.Cha ajabu nilipofika home nikamkuta anafua.. nikamuuliza Baby mbona unafua tena? akaniambia usijali nimeona nikusaidie... nikaingia ndani nikachukua kanga nikatoka nikataka kufua akanikatazz... bas nikamuacha akawa anafua.... katika kupiga story na utani tukawa tunataniana kama kawaida mpaka akamaliz kufua tukaingia ndani... tukiwa na mdogo wake wa kiume tunapiga wote story akaongea kitu mm nikacheka akaniambia unacheka na adui yako?nikamwambia kama utani ''mmh mimi ni adui yako? akajibukwan hujui? mm nikajua ni utani nikanyamaza tukaendelea na story.. baadae na yy akaniambia Sweety njoo nikuambia na mm kwa utani nikamjibu ww c umesema mm ni adui yako mbona unaniita? akasema kwa hiyo hutaki kuja nikajib ndio.. nikaona ananyanyuka na kunipa poch yangu ... nikashangaa na kumuuliza unamaanisha niende au? akasema sijui... nikachukua poch kama utani nikanyanyuka nikamwambia bye... akasema poa na ukiondoka usinipigie cm.. mm nikiwa kwenye utan nikatoka nje nikijua ataniita nikaona kimya bac na mm nikaondoka...Mpaka nimefiak nyumban sikumpigia cm na yy hakunipigia na sasa niko o fscn hawez kunipigia cm kwan haturuhusiw kuingia na cm mpaka mm nimpigie na cm ya ofic. Swali langu je? nimpigie cm au nimuache? na je ananipenda kweli au alifanya vile kwa lengo gani? mnisaidie please ili nisije kulia tena kwa ajili ya mapenz.Ni mm lina
 

Unaonaje ukiandika kwa kutumia aya?
 
Nimejaribu ku Edit nimeshindwa wengine wagen humu ndani jamani... ushauri wenu utanifaa sana
 
wewe hujui matumizi ya (aya, vituo, full stop, viulizo, mshangao!! )
 
Raha zake unazijua wewe na dhiki zake unazijua wewe,kama unaona anakutesa fanya maamuzi kwani unaelekea mapenzi yenu yana utani sana sijaona kwenye hiyo mada kama kuna sehemu mme ongea serious,sasa inawezeka mwenzio anatania hujamuelewa au ndio tabia yake kukujibu pumba mda wote au niseme wewe uko chini yake chakufanya fikiri tena ndio utoe uamuzi....
 
Okay Mkarolina, nakushauri uwe real kwenye mapenzi ili usijeumizwa tena. Siku hizi hakuna kubembelezwa kuna kubembelezana.
Inaelekea una vichembe vya kiburi na jeuri, unaringaringa fulani, na hujali hisia za mwenzio, na wala hujui kuomba msamaha. We unachukulia kila kitu poa tu. Mapenzi yanahitaji effort mamaa.

Hakuna kitu kibaya kama kunyanyang'anywa tonge wakati mimate imeanza kudondoka.
 
Nimepata shida kuisoma, anyway mi naona ni childish love!! Halafu inaonekana wewe sio mdadisi, hujauliza adui yako ina maana gani, yaain wewe kila kitu unachukulia utani mpaka ukafika home, huyo swit yako anaonekana anakupenda bt wewe waonekana ni child ndio maana Gaijin anakuuliza how old are u??
 
Nyie mpo kwenye lugha gongana,,hamwelewani ni mda gani wa utani na upi wa usiriz.

Kunasiku utampiga na mto mkiwa kitandani, yeye akakutoa manundu.

Mi nakushauri umpigie mmyamalize.
Nadhani uko mgodini wewe, atajua tayari ushapata mchimba madini.
 
Pole! Hebu mcheki jamaa uongee naye then urudi hapa jamvini utakapo fikia
 
Re: Nishaurini nisiumie tena jamani.. Una umri gani? @ Gaijin .... Nina miaka 21
 
@ Kaka Jambazi . Sijapata mwingine ila mm kwa sasa napenda kuwa makini sana na mahusiano ili nisiumie.
 
@ Freema.. Jamani yani mimi najitahid kumbembeleza ila ndo kama hivyo ndugu yangu naona kama haelekei vile.
 
Dah, Mko na umri gani? maana hii kesi inaweza kuamuliwa ktk upeo huo pia.
 
@ KubingwaNgoja nimpigie then nitarudi tena. Asante kwa ushauri mzuri.
 
uache kuchukulia kila kitu utani,siku nyingine utakufa kwa hiyo hata kama jamaa anakupachika mimba wewe unafikiria utani,uwe makini dada yangu wanaume sio waminifu hata kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…