Nissan Xtrail taa ya check engine imewaka

Nissan Xtrail taa ya check engine imewaka

mpwakimeo

Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
91
Reaction score
59
Hii ni Xtrail ya 2007/8. Taa ya check engine inawaka lakini gari inafanya kazi vizuri tu. Nimejaribu procedure za kui-reset lakini bado. Pia nilichomoa battery kwa sekunde chache lakini bado. Kuna jamaa yangu kaniambia yeye inawaka mwaka wa pili sasa na maisha yanaendelea kama kawaida. Kasema kama kungekuwa na tatizo gari isingekubali kuwaka. Ila mimi sijisikii salama hiyo taa ikiwaka. Kama kuna fundi mwenye machine ya kucheki Nissan Xtrail maeneo ya Mwanza, tuwasiliane. Au kama kuna msaada wowote namna ya kuizima (reset) hiyo taa.
Polish_20221013_195920864.jpg
 
Hii ni Xtrail ya 2007/8. Taa ya check engine inawaka lakini gari inafanya kazi vizuri tu. Nimejaribu procedure za kui-reset lakini bado. Pia nilichomoa battery kwa sekunde chache lakini bado. Kuna jamaa yangu kaniambia yeye inawaka mwaka wa pili sasa na maisha yanaendelea kama kawaida. Kasema kama kungekuwa na tatizo gari isingekubali kuwaka. Ila mimi sijisikii salama hiyo taa ikiwaka. Kama kuna fundi mwenye machine ya kucheki Nissan Xtrail maeneo ya Mwanza, tuwasiliane. Au kama kuna msaada wowote namna ya kuizima (reset) hiyo taa. View attachment 2393210
Peleka ikafanyiwe diagnosis. Niliwahi kuwa na shida hiyo issue ikawa sensor. Utaua gari.
 
Tafuta mafundi fasta achana na hadithi za kale eti rafiki yako anaendesha gari yake taa ikiwa inawaka.
utauwa gari kizembe Sana hiyo taa inawaka kuna shida kwenye engine
 
Hii ni Xtrail ya 2007/8. Taa ya check engine inawaka lakini gari inafanya kazi vizuri tu. Nimejaribu procedure za kui-reset lakini bado. Pia nilichomoa battery kwa sekunde chache lakini bado. Kuna jamaa yangu kaniambia yeye inawaka mwaka wa pili sasa na maisha yanaendelea kama kawaida. Kasema kama kungekuwa na tatizo gari isingekubali kuwaka. Ila mimi sijisikii salama hiyo taa ikiwaka. Kama kuna fundi mwenye machine ya kucheki Nissan Xtrail maeneo ya Mwanza, tuwasiliane. Au kama kuna msaada wowote namna ya kuizima (reset) hiyo taa. View attachment 2393210
Achana na habari za gari ya rafiki yako...huyo hajali..
Fanya diagnosis ujue shida iko wapi..kama ni sensa ununue uweke maisha yaendelee..

Utakuja kununua injini kisa kisensa cha laki 2
 
Hapa ndipo mnapoanzaga kuzikosea adabu hizi gari halafu baadae mnasema gari mbovu, mara zinachemsha hovyo, mara spare gharama, mara sijui nini, maneno kibao ila ukweli ni kwamba huwa mnazitafuta ubaya tu hizi gari.

Huyo mwenzako anayetembea na taa ya check engine imewaka atakuja kuhadithia siku moja.


Hiyo taa ya njano ni kukuandaa kuwa kuna changamoto imekuwa detected na inatakiwa kupewa attention. Taa ikibadilika kuwa nyekundu maana yake sasa changamoto imekuwa tatizo na inahitaji utatuzi wa haraka.

So kimsingi bado una nafasi ya kushughulikia tatizo hilo muda huu.

Nissan ni miongoni mwa gari zenye warning system nzuri sana ambayo hukujuza mapema sana. Na ukiwa unajali gari yako hautakuja sikia changamoto ambazo kila mtu huwa anazihadithia.

Nenda gereji yenye diagnosis machine au software wakukagulie codes za hiyo changamoto kwenye engine ili zishughulikiwe chap.
 
Back
Top Bottom