Nissan yaunda magari mapya yanayotumia umeme

Nissan yaunda magari mapya yanayotumia umeme

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,772
Reaction score
22,598

Nissan yaunda magari mapya ya umeme

Kampuni ya magari ya Nissan imezindua magari mapya ya umeme, wakati inakabiliana na ushindani unaozidi kukua wa magari ya umeme

Aina hiyo mpya ya magari yanaweza kusafiri mwendo wa asilimia 50 zaidi baada ya kupata chaji, kwa mujibu wa kampuni hiyo.

Hata hivyo bado magari hayo hayajafikia mwendo wa magari wa Tesla na GM.

Magari hayo yanayofahamika kama 'Leaf' yanakabiliwa na ushindani mkali wakati sekta ya magari yanayotumia umeme inazidi kukua.

Magari mapya ya Leaf yameuzwa nchini Japan kuanzia Oktoba na yataanza kuuzwa sehemu zingine mwaka ujao.

Kati ya mabadiliko yaliyofanyiwa hayo magari hayo ni mfumo wa kujindesha unaofahamika kama ProPilot Park, ambao huyawezesha kepenya maeneoimagumu hususan wakati wa kuegeshwa.

Pia yana teknolojia ya kujiendesha yenyewe hasa kwenye babara ambayo inaelekea upande mmoja tu.

Bei ya magari hayo itaanzia yen 3,150,360 au pauni 22,220.

Magari hayo yanayofahamika kama 'Leaf' yanakabiliwa na ushindani mkali wakati sekta ya magari yanayotumia umeme inazidi kukua.
 
Ni maendeleo mazuri. Sisi bongo bado tunahesabu vyerehani 4 na kudai tuna kiwanda!
 
Back
Top Bottom