Nitafanyaje ili nikipika mandazi na sambusa zisiyonye mafuta?

Nitafanyaje ili nikipika mandazi na sambusa zisiyonye mafuta?

Lateni

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2012
Posts
676
Reaction score
335
Habari , ninapenda sana kupika mandazi, sambusa n.k ila nikishaivisha mandazi yanakua yamenyonya mafuta mengi sana, na ndani yanakua hayana nyama. Ninaomba mnijulishe nifanyaje ili yatoke vizuri bila kunyonya mafuta mengi na kukosa nyama.

Asante.
 
hakikisha mafuta yamechemka vizuri halafu kaanga baada ya hapo weka kwenye gazeti au tissue ili yanyonywe mafuta hayo..
 
Habari , ninapenda sana kupika mandazi, sambusa n.k ila nikishaivisha mandazi yanakua yamenyonya mafuta mengi sana, na ndani yanakua hayana nyama. Ninaomba mnijulishe nifanyaje ili yatoke vizuri bila kunyonya mafuta mengi na kukosa nyama.

Asante.

Weka chumvi kidogo wakati wa kukanda, husaidia maandazi yasinyonye mafuta mengi.
 
Lateni sielewi unakosea wapi, ila katika experience yangu huwa naona baadhi ya vitu ambayo husababisha maandazi kunyonya mafuta ni kukosea wakati wa ukandaji wake. Baadhi ya sababu ni kukandia mafuta mengi, kutoweka kabisa amira (iwe baking powder ama yeast a.k.a amira ya chenga); na pia tabia ya kuyakaanga kwenye moto mdogo mno katika mafuta ambayo bado ni mabichi.

Kama hapa hujanielewa na kupata suluhu, tafadhali naomba process yako ya ukandaji hadi upishi ili kuelewa tatizo lipo wapi.
 
Lateni sielewi unakosea wapi, ila katika experience yangu huwa naona baadhi ya vitu ambayo husababisha maandazi kunyonya mafuta ni kukosea wakati wa ukandaji wake. Baadhi ya sababu ni kukandia mafuta mengi, kutoweka kabisa amira (iwe baking powder ama yeast a.k.a amira ya chenga); na pia tabia ya kuyakaanga kwenye moto mdogo mno katika mafuta ambayo bado ni mabichi.

Kama hapa hujanielewa na kupata suluhu, tafadhali naomba process yako ya ukandaji hadi upishi ili kuelewa tatizo lipo wapi.

Mimi huanza kwa kutia sukari kidogo, iliki, hamira, na ninakandia maji ya uvuguvugu,wakati wa kukanda siweki mafuta, nikishamaliza kukanda, ninayakata na kuyaacha yaumuke , then ninaya kaanga,

nahisi tatizo langu liko hapo kwenye moto mdogo na mafuta mabichi, pia mdau Dora amenishauri niwe naweka chumvi kidogo .
 
Mimi huanza kwa kutia sukari kidogo, iliki, hamira, na ninakandia maji ya uvuguvugu,wakati wa kukanda siweki mafuta, nikishamaliza kukanda, ninayakata na kuyaacha yaumuke , then ninaya kaanga,

nahisi tatizo langu liko hapo kwenye moto mdogo na mafuta mabichi, pia mdau Dora amenishauri niwe naweka chumvi kidogo .

Nimemsoma Dora kwenye suala la chumvi, kweli ujaribu labda itasaidia. Hilo kwa upande wangu sioni kama ni tatizo sana sababu pia situmii kabisa chumvi na maandazi yangu hayanyonyi kabisa mafuta.

Kama umekiri kuwa mafuta huwa watumia mabichi na hali moto mdogo; then tatizo lipo hapo. Ila naweza ongeza tip pia, kitu kinachofanya maandazi yawive vizuri wakati wa kuyakaanga ni namna unga umekandwa (kikando kuwiva na kuchambuka vema).

Kuchangia hilo unaweza pasha mafuta ya kupikia kidogo sana yakawa ya moto sana, ukayatia katika unga wako baada ya michanganyiko kama amira na sukari (kabla ya maji); then ukachanganya ule unga, baada ya hapo ukaendelea na hatua zinazofuata.
 
Sambusa wakati wa ufungaji hakikisha hakuna matundu.
 
Back
Top Bottom