Nitaitumia vema haki yangu kikatiba kuipigia kura ya HAPANA katiba pendekezwa - mwana CCM

Nitaitumia vema haki yangu kikatiba kuipigia kura ya HAPANA katiba pendekezwa - mwana CCM

President Elect

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
693
Reaction score
212
Nikiwa mwanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi mwenye kadi# natamka bayana kuwa nitaitumia vema haki yangu ya kikatiba kuipigia kura ya HAPANA katiba inayopendekezwa. Kuwa mwana CCM hakuninyimi utashi wa kufanya maamuzi sahihi kwa taifa letu, nitasema kweli daima! Nawaomba sana wana CCM wenzangu wenye uchungu na taifa letu mniunge mkono!

Mapinduzi ya kweli yataletwa na wana CCM ndani ya CCM. Jamani tusiwe vipofu, nchi yetu inaangamia mikononi mwetu tungali tunaona, tuchukue hatua kabla jua halijazama!!!

Kura ya HAPANA kwa katiba inayopendekezwa, ndio jibu sahihi la katiba hiyo kuboreshwa ndani ya siku 60 kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba!
 
Jabla hujatushawishi tuseme hapana ni vyema ukatupa udhaifu unaodhani twatakiwa tuukatae kuliko kutushawishi tuseme hapana kwakua wewe unasema hapana twambie sababu ambayo unadhani twatakiwa kusema hapana ichambue tushawishi kwa hoja na si kwakugeneralize kama ulivyofanya
 
Jabla hujatushawishi tuseme hapana ni vyema ukatupa udhaifu unaodhani twatakiwa tuukatae kuliko kutushawishi tuseme hapana kwakua wewe unasema hapana twambie sababu ambayo unadhani twatakiwa kusema hapana ichambue tushawishi kwa hoja na si kwakugeneralize kama ulivyofanya

1. Katiba ya nchi ni maridhiano ya pande zinazokinzana, katiba pendekezwa sio!
2. Katiba ni mkataba ulioridhiwa na pande mbili, watawala na watawaliwa - katiba pendekezwa imezingati maslahi ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa
3. Katiba pendekezwa imempa madaraka makubwa mno rais kuamua/kuteua bila mipaka na halazimiki kufuata ushauri hata kama ni wa manufaa kwa taifa letu
4.Haki za msingi zimetolewa kwa mkono mmoja zikaporwa kwa mkono wa pili, mwananchi hawezi kudai haki yake mahakamani
5.Wananchi hawajapewa muda wa kutosha kuisoma na kuielewa katiba pendekezwa
6.Daftari la wapiga kura halijaboreshwa, hata kufikia tarehe ya kupiga kura ya maoni litakuwa bado, hivyo kuwanyima watu haki yao
 
nikiwa mwanachama hai wa chama cha mapinduzi mwenye kadi# natamka bayana kuwa nitaitumia vema haki yangu ya kikatiba kuipigia kura ya hapana katiba inayopendekezwa. Kuwa mwana ccm hakuninyimi utashi wa kufanya maamuzi sahihi kwa taifa letu, nitasema kweli daima! Nawaomba sana wana ccm wenzangu wenye uchungu na taifa letu mniunge mkono!

Mapinduzi ya kweli yataletwa na wana ccm ndani ya ccm. Jamani tusiwe vipofu, nchi yetu inaangamia mikononi mwetu tungali tunaona, tuchukue hatua kabla jua halijazama!!!

Kura ya hapana kwa katiba inayopendekezwa, ndio jibu sahihi la katiba hiyo kuboreshwa ndani ya siku 60 kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba!


aaaaaa ha ha ha ha prezidaa kumbe mwanachama hai tena unapumua, haya bana weka namba ya kadi yako hapa tuone na hakika wewe ni mamluki unataka kutumia mwavuli wa chama kufanya uhalifu humu ndani ha ha ha tumekushtukia unatafuta kuonewa huruma na wana jf peleka zako usitutibue sie wazalendo wa nchi hii hiloooooo!!
 
1. Katiba ya nchi ni maridhiano ya pande zinazokinzana, katiba pendekezwa sio!
2. Katiba ni mkataba ulioridhiwa na pande mbili, watawala na watawaliwa - katiba pendekezwa imezingati maslahi ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa
3. Katiba pendekezwa imempa madaraka makubwa mno rais kuamua/kuteua bila mipaka na halazimiki kufuata ushauri hata kama ni wa manufaa kwa taifa letu
4.Haki za msingi zimetolewa kwa mkono mmoja zikaporwa kwa mkono wa pili, mwananchi hawezi kudai haki yake mahakamani
5.Wananchi hawajapewa muda wa kutosha kuisoma na kuielewa katiba pendekezwa
6.Daftari la wapiga kura halijaboreshwa, hata kufikia tarehe ya kupiga kura ya maoni litakuwa bado, hivyo kuwanyima watu haki yao

Busara ni kitu cha bure na wala huhitaji kwenda darasani kufundishwa busara. Busara ni namna mtu anapotumia hekima yake mbele ya wengine. Tanzania hatuna Watawala au watawaliwa, nikujulishe kwamba Katiba Inayopendekezwa inasema "Sisi wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu"
 
Leo kuna kanisa nilihudhulia ibada ya asubuhi imesomwa waraka wa askofu ujumbe umekuwa wazi kama hayo mambo ya mahakama ya nanihii yamo pigeni hapana!!! Kumbe akina gwajima wapo wengi tofauti ni kuwa mmoja alitukana ila content imeeleweka kwa waumini, serikali kama inaweza kuchomoa hii kitu ifanye mazingira ya upigaji kura yasije kuwa magumu wakaanza kuwaandama halmashauri na wakurugenzi kuwafukuza hali mambo yanaonekana wazi kwenye hili!!
 
Namaanisha namsona sehemu anazosimamia jao bado kura ni siri na kila mtu anauelewa tofauti japo kuna vitu sivikubali ndani ya rasimu inayopendekezwa na pia hili swala la katiba sio swala la chama ni swala la nchi sasa hata kupiga kura hatupigi kichama tunapiga kwakuzingatia ni wapi nchi yetu tunataka iende.
 
1. Katiba ya nchi ni maridhiano ya pande zinazokinzana, katiba pendekezwa sio!
2. Katiba ni mkataba ulioridhiwa na pande mbili, watawala na watawaliwa - katiba pendekezwa imezingati maslahi ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa
3. Katiba pendekezwa imempa madaraka makubwa mno rais kuamua/kuteua bila mipaka na halazimiki kufuata ushauri hata kama ni wa manufaa kwa taifa letu
4.Haki za msingi zimetolewa kwa mkono mmoja zikaporwa kwa mkono wa pili, mwananchi hawezi kudai haki yake mahakamani
5.Wananchi hawajapewa muda wa kutosha kuisoma na kuielewa katiba pendekezwa
6.Daftari la wapiga kura halijaboreshwa, hata kufikia tarehe ya kupiga kura ya maoni litakuwa bado, hivyo kuwanyima watu haki yao


Ndugu yangu acha porojo,nenda kagombee ubunge ili wengi wa kusikie kupitia bunge Tv lakini haiwezekani kupata nafasi kwa sababu wewe ni mnafiki na muongo,huwezi kupinga kila kitu we kiumbe gani usiye na chembe ya uelewa???? Afu unakalia kurudia yale yale ambayo nimshakupa za uso kwa sababu umekaririshwa ha ha ha ha wenzako juzi walikua wanagongana wao kwa wao kwa umbugila wao wa kutokusoma na kuelewa hoja! Teh teh teh teh kadaaaa nenda kalale bhana umechoka leo.
 
Namaanisha namsona sehemu anazosimamia jao bado kura ni siri na kila mtu anauelewa tofauti japo kuna vitu sivikubali ndani ya rasimu inayopendekezwa na pia hili swala la katiba sio swala la chama ni swala la nchi sasa hata kupiga kura hatupigi kichama tunapiga kwakuzingatia ni wapi nchi yetu tunataka iende.


Kumbe umeone ee kura ni siri bhana tena ukapige kula achana na PResident elect anayejifanya Kada wa chama Kilicho madarakani na wakati huo huo yuko UKAWA hata hatumuelewi tumemshtukia ha ha ha.

Suala la katiba sio suala la chama ni la watanzania wote maana tunaweka msingi wa mustakabali wataifa letu.
 
Leo kuna kanisa nilihudhulia ibada ya asubuhi imesomwa waraka wa askofu ujumbe umekuwa wazi kama hayo mambo ya mahakama ya nanihii yamo pigeni hapana!!! Kumbe akina gwajima wapo wengi tofauti ni kuwa mmoja alitukana ila content imeeleweka kwa waumini, serikali kama inaweza kuchomoa hii kitu ifanye mazingira ya upigaji kura yasije kuwa magumu wakaanza kuwaandama halmashauri na wakurugenzi kuwafukuza hali mambo yanaonekana wazi kwenye hili!!

Mmmmmmmmmmmm!!!!!?ueleweki mahakama ya nanihiii ndio nini hueleweki kama hutaki kuwa wazi toka hapa, usituchanganyie mada.
 
Mmmmmmmmmmmm!!!!!?ueleweki mahakama ya nanihiii ndio nini hueleweki kama hutaki kuwa wazi toka hapa, usituchanganyie mada.
umenielewa lakini mie mwoga kuanzisha mijadala ya mashambuliano ya maneno, nimeweka hivyo kupunguza jazba za kiumini miongoni mwa wachangiaji
 
umenielewa lakini mie mwoga kuanzisha mijadala ya mashambuliano ya maneno, nimeweka hivyo kupunguza jazba za kiumini miongoni mwa wachangiaji

Mlendamboga, tushirikiane kujenga nchi yetu maana hapa utaifa ni amali yetu na ni nyumbani kwetu ambapo tuatamani siku zote kuwa ni mahli salama pa sisi Watanzania kuishi. Tuijenge sasa wewe na mimi kwa kuipa Katiba Mpya. Simama imara Mtanzania jenga nchi yako.
 
[font=&quot]busara ni kitu cha bure na wala huhitaji kwenda darasani kufundishwa busara. Busara ni namna mtu anapotumia hekima yake mbele ya wengine. Tanzania hatuna watawala au watawaliwa, nikujulishe kwamba katiba inayopendekezwa inasema “sisi wananchi wa jamhuri ya muungano wa tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu”[/font] [font=&quot] [/font]

sisi wananchi wa JMT tunasema hapana, narudia tena hapana.
 
1. Katiba ya nchi ni maridhiano ya pande zinazokinzana, katiba pendekezwa sio!
2. Katiba ni mkataba ulioridhiwa na pande mbili, watawala na watawaliwa - katiba pendekezwa imezingati maslahi ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa
3. Katiba pendekezwa imempa madaraka makubwa mno rais kuamua/kuteua bila mipaka na halazimiki kufuata ushauri hata kama ni wa manufaa kwa taifa letu
4.Haki za msingi zimetolewa kwa mkono mmoja zikaporwa kwa mkono wa pili, mwananchi hawezi kudai haki yake mahakamani
5.Wananchi hawajapewa muda wa kutosha kuisoma na kuielewa katiba pendekezwa
6.Daftari la wapiga kura halijaboreshwa, hata kufikia tarehe ya kupiga kura ya maoni litakuwa bado, hivyo kuwanyima watu haki yao

Daa ndugu unajitahid kuandika rubbish....mbon sion kitu hapo.....vihoja vya kitoto ambavyo kila siku vinajibiwa.....eti katiba inayopendekezwa imezingatia matakwa ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa...nan kakwambia....more than 70% ya hii kitu it talks about citizen...na haki zao kingine haki ipi imetolewa na kupokwa kwingine acha kifuata mkumbo bila ushahid.....75%. Ya mapendekez mapendekez ya warioba yameingia kweny katiba hii..mengine yameongezwa kwa mantiki ya kuboresha...waulize wasanii na walemavu walikosa nin kweny mapendekezo ya warioba humu yameongezwa...tusiwe kweny mkumbo wa wanasiasa waliokuw na dhamir ya kupat kitu flani wamekikosa sasa wanataka kuharibu mchakato
 
Daa ndugu unajitahid kuandika rubbish....mbon sion kitu hapo.....vihoja vya kitoto ambavyo kila siku vinajibiwa.....eti katiba inayopendekezwa imezingatia matakwa ya watawala na kutupilia mbali matakwa ya watawaliwa...nan kakwambia....more than 70% ya hii kitu it talks about citizen...na haki zao kingine haki ipi imetolewa na kupokwa kwingine acha kifuata mkumbo bila ushahid.....75%. Ya mapendekez mapendekez ya warioba yameingia kweny katiba hii..mengine yameongezwa kwa mantiki ya kuboresha...waulize wasanii na walemavu walikosa nin kweny mapendekezo ya warioba humu yameongezwa...tusiwe kweny mkumbo wa wanasiasa waliokuw na dhamir ya kupat kitu flani wamekikosa sasa wanataka kuharibu mchakato

Tatizo lake anakurupuka tu ndo maana unakuta anachokiandika hakina sequency
 
Tatizo la Tanzania sio katiba! tatizo ni utendaji hata katiba tungepewa na malaika kama hatuna uongozi thabit wenye maadili mambo yangekuwa vile vile! Look now Magufuli is real trying lakini katiba ni ile ile!
 
Back
Top Bottom