Nitakula vipi mlo kamili?

Nitakula vipi mlo kamili?

Elisha

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2011
Posts
381
Reaction score
662
Habarini!!

Kama Kuna kitu kimekuwa kinanitatiza maishani basi ni namna ya kupangilia mchanganyiko wa makundi mbali mbali ya vyakula ili kupata mlo kamili.

Ombi langu kwa anayejua mlo kamili ni nini, anipe mifano miwili mitatu, nile nini na nini ili nipate mlo kamili?!

Mungu akubariki!
 
Mfano:-
Breakfast
Muhogo/magimbi/kiazi/ndizi/ ya kuchemsha +kachumbari+ yai la kukaanga + chai ya rangi au ya maziwa baadae kidogo unashushia juisi ya chungwa au kula machungwa yenyewe.


Chapati+ maharagwe/kunde/mbaazi/ +chai ya maziwa au ya rangi ukashudhia chungwa au tikiti baadae.

Mkate wa kutoast unaupaka cheese + legumes kidogo (maharage au nduguze) + juisi ya chungwa.


Mkate wa kutoast+ yai la kukaanga + parachichi/guacamole + juisi ya tikiti maji

Smoothie za matunda tofauti tofauti mfano waweza saga maziwa, ndizi,tende, embe, parachichi, papai kwa seti utakapangilia mwenyewe ukashiba siku nzima au Kama upo kwenye diet utachagua matunda yenye nishati kidogo.

Lunch:-
Kama mpenzi wa ugali na wali hapa ndio mahala pa kujilipua.

Ugali (dona au unga wowote wa nafaka ndogondogo Kama kweli unajali mlo kamili) + nyama kavu/samaki + kachumbari na mboga mboga kwa wingi + matunda mepesi (tikiti, tango, parachichi,)

Wali ndondo + kachumbari+ kamchicha/ spinach + matunda mepesi.


Viazi mviringo vya kuoka, kitoweo na salad/ kachumbari nyingii ..


Jioni.
Kama ulikula vizuri mchana basi jioni haina haja ya kujijaza calories zisizo na matumizi, unaweza kulalia either.

Salad ya matunda mepesi (tango, nyanya, parachichi utatupia olive oil, olives na cheese)

Salad ya majani, nyanya, olives, olive oil ukalia samaki au nyama kavu.

Smoothie,

Supu ya mbogamboga


Supu ya kuku

Supu ya samaki.

Humo utatupiamo mbogamboga ziwe nyingi zaidi.

Natumai nimejaribu mkuu unaweza kupangilia kwa mtindo huo kulingana na mazingira yako na vinavyopatikana.
 
Mfano:-
Breakfast
Muhogo/magimbi/kiazi/ndizi/ ya kuchemsha +kachumbari+ yai la kukaanga + chai ya rangi au ya maziwa baadae kidogo unashushia juisi ya chungwa au kula machungwa yenyewe.


Chapati+ maharagwe/kunde/mbaazi/ +chai ya maziwa au ya rangi ukashudhia chungwa au tikiti baadae.

Mkate wa kutoast unaupaka cheese + legumes kidogo (maharage au nduguze) + juisi ya chungwa.


Mkate wa kutoast+ yai la kukaanga + parachichi/guacamole + juisi ya tikiti maji

Smoothie za matunda tofauti tofauti mfano waweza saga maziwa, ndizi,tende, embe, parachichi, papai kwa seti utakapangilia mwenyewe ukashiba siku nzima au Kama upo kwenye diet utachagua matunda yenye nishati kidogo.

Lunch:-
Kama mpenzi wa ugali na wali hapa ndio mahala pa kujilipua.

Ugali (dona au unga wowote wa nafaka ndogondogo Kama kweli unajali mlo kamili) + nyama kavu/samaki + kachumbari na mboga mboga kwa wingi + matunda mepesi (tikiti, tango, parachichi,)

Wali ndondo + kachumbari+ kamchicha/ spinach + matunda mepesi.


Viazi mviringo vya kuoka, kitoweo na salad/ kachumbari nyingii ..


Jioni.
Kama ulikula vizuri mchana basi jioni haina haja ya kujijaza calories zisizo na matumizi, unaweza kulalia either.

Salad ya matunda mepesi (tango, nyanya, parachichi utatupia olive oil, olives na cheese)

Salad ya majani, nyanya, olives, olive oil ukalia samaki au nyama kavu.

Smoothie,

Supu ya mbogamboga


Supu ya kuku

Supu ya samaki.

Humo utatupiamo mbogamboga ziwe nyingi zaidi.

Natumai nimejaribu mkuu unaweza kupangilia kwa mtindo huo kulingana na mazingira yako na vinavyopatikana.
Heshima kwako! Ubarikiwe sana kwa mchango wako!
 
Habarini!!

Kama Kuna kitu kimekuwa kinanitatiza maishani basi ni namna ya kupangilia mchanganyiko wa makundi mbali mbali ya vyakula ili kupata mlo kamili.

Ombi langu kwa anayejua mlo kamili ni nini, anipe mifano miwili mitatu, nile nini na nini ili nipate mlo kamili?!

Mungu akubariki!
Mkuu, kula ushibe. I mean hakikisha tumbo liko full full. Mengine waachie wazungu.
 
Mkuu, kula ushibe. I mean hakikisha tumbo liko full full. Mengine waachie wazungu.
Hapa ndipo waafrika tunapoanguka[emoji23][emoji23][emoji23]eti tuwaachie wazungu. Yaani unataka daktari ndiye akuambie kula embe mbivu asubuhi mbili,mchana mbili na jioni mbili. Tubadilike nasi tupate afya nzuri siyo kujaza tumbo mkuu
 
Binafsi naamini kwa kula mlo kamili tunapata mpaka afya ya ubongo. Tunakuwa uwezo mzuri wa kufikiri. Kula hovyo kunaweza kupelekea hata kupata magonjwa badala ya kupata afya! Waafrika tuna haki pia ya kula vizuri! Inawezekana sikula vizuri hapo kabla lakini natamani sana wanangu wale vizuri wapate afya na akili pia. Ahsante kwa mchango wako!
 
Hapa ndipo waafrika tunapoanguka[emoji23][emoji23][emoji23]eti tuwaachie wazungu. Yaani unataka daktari ndiye akuambie kula embe mbivu asubuhi mbili,mchana mbili na jioni mbili. Tubadilike nasi tupate afya nzuri siyo kujaza tumbo mkuu
Afrika quantity ndio priority, wala sio quality. Hakikisha tumbo linakuwa full, hata kama unakula ugali na kushushia uji wa mahindi.
 
Binafsi naamini kwa kula mlo kamili tunapata mpaka afya ya ubongo. Tunakuwa uwezo mzuri wa kufikiri. Kula hovyo kunaweza kupelekea hata kupata magonjwa badala ya kupata afya! Waafrika tuna haki pia ya kula vizuri! Inawezekana sikula vizuri hapo kabla lakini natamani sana wanangu wale vizuri wapate afya na akili pia. Ahsante kwa mchango wako!

Jitahidi sana kulimit sehemu wanazokula, hakikisha watoto wanakula nyumbani na si sehemu nyengine Kama hakuna sababu ya kufanya hivyo. hii itakupa uhakika wa kile wanachoandaliwa kua ni salama na chenye faida kwa afya ya mtoto.


Epuka sana fast foods, haziongezi chochote zaidi ya calories na risks za kupata magonjwa mabaya.


Muhamasishe mama watoto awatengenezee healthy treats nyumbani ili wanapopata hamu ya kutafuna tafuna watafute snacks zenye faida, watoto wanapenda rangi, mnaweza kudesign matunda kwa kuchanganya rangi ikawa kivutio kwao.


Usisahau miongoni mwa vyakula muhimu sana kwa watoto:-
Maziwa,
cheese(jitahidi upate genuine brand Kama uwezo upo mfano kiri , al marai ),
salmon,
sardines,
Parachichi,
Carrots,(hizi unaweza ukawazoesha wakawa wanatafuna Kama snacks)

Biringanya,
ufuta nk.
Vipo vingi sema hakikisha vile unavyoweza kumudu unawapa watoto Mara kwa Mara.

Kataa vitu Kama soda, jus cola and likes, pipi, biskuti, chama and other funny names kuingia ndani ya nyumba yako wala kupewa watoto wako, fanya iwe sheria itasaidia somehow kupunguza au kukata matumizi ya hivyo vitu.




We're what we eat......ukiangalia sana kuhusu hili athari yake ipo moja kwa moja kwa vijana wetu wa tunaokula sembe na kachumbari....uwezo wao wa kufikiri unafifia mno as days goes on....hawawi critical thinkers na wanabehave in very annoying manners, pamoja na utandawazi, lishe duni inachangia kwa kiasi kikubwa sana kuwabomoa...........

majanga yanakua mengi kwa sababu watu hawazinourish akili zao ziwe kwenye optimum level ya matumizi.


Wazee wetu walikua bora kwa sababu wao walikua na access na chakula asili na katika ubora wake.....wazungu na jamii nyingi nje ya Africa mpangilio wa chakula ni utamaduni unaoheshimiwa na kurithishwa kwa hiyo watoto wanakua wakiwa na uelewa na nidhamu kuhusu eating habits.
 
Jitahidi sana kulimit sehemu wanazokula, hakikisha watoto wanakula nyumbani na si sehemu nyengine Kama hakuna sababu ya kufanya hivyo. hii itakupa uhakika wa kile wanachoandaliwa kua ni salama na chenye faida kwa afya ya mtoto.


Epuka sana fast foods, haziongezi chochote zaidi ya calories na risks za kupata magonjwa mabaya.


Muhamasishe mama watoto awatengenezee healthy treats nyumbani ili wanapopata hamu ya kutafuna tafuna watafute snacks zenye faida, watoto wanapenda rangi, mnaweza kudesign matunda kwa kuchanganya rangi ikawa kivutio kwao.


Usisahau miongoni mwa vyakula muhimu sana kwa watoto:-
Maziwa,
cheese(jitahidi upate genuine brand Kama uwezo upo mfano kiri , al marai ),
salmon,
sardines,
Parachichi,
Carrots,(hizi unaweza ukawazoesha wakawa wanatafuna Kama snacks)

Biringanya,
ufuta nk.
Vipo vingi sema hakikisha vile unavyoweza kumudu unawapa watoto Mara kwa Mara.

Kataa vitu Kama soda, jus cola and likes, pipi, biskuti, chama and other funny names kuingia ndani ya nyumba yako wala kupewa watoto wako, fanya iwe sheria itasaidia somehow kupunguza au kukata matumizi ya hivyo vitu.




We're what we eat......ukiangalia sana kuhusu hili athari yake ipo moja kwa moja kwa vijana wetu wa tunaokula sembe na kachumbari....uwezo wao wa kufikiri unafifia mno as days goes on....hawawi critical thinkers na wanabehave in very annoying manners, pamoja na utandawazi, lishe duni inachangia kwa kiasi kikubwa sana kuwabomoa...........

majanga yanakua mengi kwa sababu watu hawazinourish akili zao ziwe kwenye optimum level ya matumizi.


Wazee wetu walikua bora kwa sababu wao walikua na access na chakula asili na katika ubora wake.....wazungu na jamii nyingi nje ya Africa mpangilio wa chakula ni utamaduni unaoheshimiwa na kurithishwa kwa hiyo watoto wanakua wakiwa na uelewa na nidhamu kuhusu eating habits.
Ubarikiwe mno! Nimejifunza mengi, ahsante sana!
 
Binafsi naamini kwa kula mlo kamili tunapata mpaka afya ya ubongo. Tunakuwa uwezo mzuri wa kufikiri. Kula hovyo kunaweza kupelekea hata kupata magonjwa badala ya kupata afya! Waafrika tuna haki pia ya kula vizuri! Inawezekana sikula vizuri hapo kabla lakini natamani sana wanangu wale vizuri wapate afya na akili pia. Ahsante kwa mchango wako!
Mlo kamili : chukua sahani yako imagine unachora msalaba katikati ya sahani ili upate vipande (robo robo) 4. Robo ya kwanza iwe ni vyakula vya wanga (ugali, wali, mihogo, chapati, mkate nk)... Robo ya pili iwe ni vyakula vya protini na mafuta (nyama, samaki, kuku, cooking oil, mtindi nk)... Robo ya tatu vyakula vyenye vitamins/madini mbalimbali (dagaa, Karanga/nuts mbalimbali)... Robo ya mwisho ni mbogamboga na matunda....
 
Mlo kamili : chukua sahani yako imagine unachora msalaba katikati ya sahani ili upate vipande (robo robo) 4. Robo ya kwanza iwe ni vyakula vya wanga (ugali, wali, mihogo, chapati, mkate nk)... Robo ya pili iwe ni vyakula vya protini na mafuta (nyama, samaki, kuku, cooking oil, mtindi nk)... Robo ya tatu vyakula vyenye vitamins/madini mbalimbali (dagaa, Karanga/nuts mbalimbali)... Robo ya mwisho ni mbogamboga na matunda....
Umenipa akili mpya! Ahsante sana kwa mchango wako. Nimejifunza pakubwa sana, Mungu akubariki sana!
 
Mkuu, kula ushibe. I mean hakikisha tumbo liko full full. Mengine waachie wazungu.
Kuna siku nilikula tikiti tu nikalala....tumbo lililalamika usiku kucha, wengine tumezoesha matumbo kukaa full na vitu vizito vizito hadi sio vizuri
 
Kuna siku nilikula tikiti tu nikalala....tumbo lililalamika usiku kucha, wengine tumezoesha matumbo kukaa full na vitu vizito vizito hadi sio vizuri
Tumbo langu limezoea kukaa likiwa "top top"
Kusema nile matunda tu pekee yake na nilale, siwezi kwakweli.
Labda nile parachichi, tena iwe walau nusu ndoo.
 
Tumbo langu limezoea kukaa likiwa "top top"
Kusema nile matunda tu pekee yake na nilale, siwezi kwakweli.
Labda nile parachichi, tena iwe walau nusu ndoo.
Nusu ndoo 😂😂😂 dah
 
Tumbo langu limezoea kukaa likiwa "top top"
Kusema nile matunda tu pekee yake na nilale, siwezi kwakweli.
Labda nile parachichi, tena iwe walau nusu ndoo.
We mwamba noma sana aisee! Nusu ndoo! Upo vizuri!
 
Naongezea kidogo tu juu ya tabia ambazo unaweza kujirekebisha pia
1. Usipende sana kula viini vya mayai, kula ile sehemu nyeupe ya nje ya yai. Ikiwa kuna ulazima wa kula na kiini cha yai basi usile zaidi ya vitatu kwa wiki
2. Jenga tabia ya kunywa maji ya dafu mara kwa mara, yana benefits nyingi unaweza kugoogle
3. Wanasayansi wanasisitiza sana suala la kunywa maji mengi kila siku lakini sio rahisi kufuata sheria hii. Kwa hiyo kuna njia rahisi sana ya kukufanya unywe maji mengi kwa siku, hakikisha unakuwa na chupa ya maji pembeni. Kwa mfano chukua chupa ya maji ya Afya 600ml ijaze maji kisha uwe unajipa zoezi la kunywa maji kidogokidogo hadi yaishe. Rudia kujaza chupa mara mbili tena yaani kwa siku walau jumla iwe chupa tatu za 600ml, utajikuta unakunywa lita 1.8 kila siku. Afya ya ngozi pia itaimarika, maana ubora wa ngozi huanzia ndani na sio nje kama wengi wanavyofikiri na kuishia kujipaka bidhaa za viwandani ili ngozi ing'ae
4. Kula mboga za majani kila siku. Lakini kuwa mwangalifu usile mchicha kila siku maana mchicha unaongeza sana damu, usije ukawa na damu nyingi sana, hivyo changanya-changanya mboga
5. Tunza matunda kwenye friji ili ule muda wowote utakaojisikia lakini kula matunda mengi mchana
6. Kwenye suala la kunywa maji hakikisha unakunywa mengi mchana na usiku kunywa kidogo sana au usinywe kabisa
7. Kula chakula kidogo asubuhi na usiku ila mchana jimwage, shindilia msosi wa maana
8. Tumia mafuta ya zaituni (Olive oil) kupikia na kama ni ghali sana bora utumie ya alizeti
9. Fanya mazoezi kila siku. Tena ungejua, mazoezi ambayo wanasayansi huwa wanashauri ufanye ni rahisi sana na karibia kila mtu huweza kufanya kwa mfano kukimbia, kutembea, kuogelea, kurukaruka na yale ya kujinyoosha. Hata sio magumu kama yale ya kunyanyua vyuma[emoji28]
10. Ogopa sana matumizi makubwa ya nyama nyekundu, badala yake kula nyama nyeupe. Miaka ya 1800s wanasayansi wa Ulaya walisisitiza sana kula nyama nyekundu lakini baada ya kuona madhara yake leo hii wanasisitiza ule mboga za majani na nyama nyeupe. Wamasai hula sana nyama nyekundu na damu, matokeo yake wanakua kwa haraka sana, ni warefu lakini hufa mapema. Majirani zao Wakikuyu, wa Kenya ni vegeterians, wanakula sana mboga za majani kuliko nyama, ni wafupi na huishi maisha marefu sana. Nyama nyekundu kula mara mojamoja mfano nyama ya nguruwe ni hatari sana kiafya kuliko nyama nyingine nyekundu kama ng'ombe, mbuzi, kondoo, n.k. Kula nyama nyeupe kwa wingi mfano samaki na kuku. Watu wa Mwanza, Bukoba, Musoma, ukanda wa ziwa Nyasa, Mtwara, Lindi, Pwani Tanga, Zanzibar na Kigoma wanaenjoy samaki aisee [emoji39][emoji39]
11. Kula katika timetable, yaani kama breakfast ni saa moja basi kila siku iwe hivyo. Unapaswa kula katika timetable nzuri uliyojiwekea kila siku. Kama lunch unakula saa saba mchana, basi kila siku saa saba mchana ikifika kula lunch hata kama huna njaa.
Kuna mambo mengi sana, nikipata muda nitakuja kuendeleza maana hii haijaishia hapa.
 
Back
Top Bottom