Nitapata wapi riwaya iitwayo MKIMBIZi kwa Dar es salaam.

Zeddicus

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2012
Posts
627
Reaction score
535
Hello wana Jf

Kama title yangu hapo juu inavyosema, nimekitafuta sana hicho kitabu bila mafanikio yeyote mwenye information kuhusu mahala naweza kukipata anisaidie.Pia riwaya za B.Mtobwa nazo yeyote mwenye information anisaidie.
Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Dah, nimekumbuka mbali sanaaaa, sijui itapatikana vipi riwaya ile. sikumbuki hata wahusika ila nafaham tu yupo mwanamke mmoja alipata shida sana ndani ya riwaya ile
 
nenda ubungo, kwa wale wauzaji vitabu wanaopanga chini pale nje karibu na vibanda vya kukatia tiketi, mi ndipo nilipotutulia matoleo yote ya Mtobwa like "Tutarudi na roho zetu, najisikia kuua tena, mikononi mwa Nunda, Lazima ufe Joram, Salamu kutoka kusimu, Pesa zako zinanuka, Dar es Salaa usiku, Nyuma ya Pazia na na Zawadi ya Ushindi" Hata hazina iliyolaaniwa cha Eddie Ganzel utakipata pale bila kusahau vya uchumi kama 'the monk who sold his Ferrari, Laws to success and so on'
 
Mkimbizi nadhani hakijatoka bado,kilichotoka karibuni from the same author ni MDUNGUAJI (The Sniper),ila kama upo Dar waweza muuliza mwandishi/mtunzi wake anaitwa Hussein Tuwa.
 

Asante sana...mkuu inaonesha dhahiri kabisa na wewe ni mdau wa usomaji vitabu..Thumb up Mkuu!
 
Mkimbizi nadhani hakijatoka bado,kilichotoka karibuni from the same author ni MDUNGUAJI (The Sniper),ila kama upo Dar waweza muuliza mwandishi/mtunzi wake anaitwa Hussein Tuwa.

Mkuu, mbona mkimbizi kilitoka muda mrefu tu.
 
Dah, nimekumbuka mbali sanaaaa, sijui itapatikana vipi riwaya ile. sikumbuki hata wahusika ila nafaham tu yupo mwanamke mmoja alipata shida sana ndani ya riwaya ile

Yaani acha tu mkuu..tangu niisome kimepita kitambo sana, na hamu niipate niisome tena that is why nahangaika kuitafuta.
 
JF ni kisima cha Busara maana B. Mtobwa namkumbuka kwa riwaya za kusisimua thnx waungwana!
 
Dah umenikumbusha mbali sana,riwaya ya mkimbizi ilifanya ninunue gazeti la kiu,Yule mtunzi Hussein Issa Tuwa anapatikana hata kwenye facebook unaweza kumtafuta.Ukifanikiwa utoe taarifa na sisi tufate
 
Dah umenikumbusha mbali sana,riwaya ya mkimbizi ilifanya ninunue gazeti la kiu,Yule mtunzi Hussein Issa Tuwa anapatikana hata kwenye facebook unaweza kumtafuta.Ukifanikiwa utoe taarifa na sisi tufate

Nimewasiliana nae kupitia account yake ya facebook amesema kwa sasa kitabu kinachopatikana ni MDUNGUAJI(The Sniper), kipo Scholastica Bookshop Mlimani city.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…