Nitasafirishaje mazao kutoka Tanzania kwenda Kenya kwa kutumia gari?

kamandamchovu

Member
Joined
Feb 5, 2017
Posts
19
Reaction score
10
Sijawahi fanya biashara ya kuvuka boda, sasa nataka nisafirishe mazao yangu nijaribu na soko la Kenya kama naweza kupata angalau faida maana huko Dar madalali hawana huruma na mtaji wangu.

Mwenye uzoefu wa ninachotaka kukifanya NAOMBA ANISAIDIE TAFADHALI
 
ningekushauri hivi, tafuta siku ufunge safari hadi tarakea(rombo) ni mpakani wa boda ya kenya na tz. Ndio mpaka mzuri wa kuingizia au kuuliza maswali yote kuhusu jinsi ya kupeleka mazao kenya. Ningekusaidia ila kw sasa hivi nilishahamia kwa trump huku, miaka kadhaa imepita nilikuwa napeleka tandam zima la kitunguu kila wiki nairobi ama nyeri kulingana na bei. fika pale utasaidika bro
 
Kama nimemuelewa vizuri sio usafiri tu ni kwamba hata kitu cha muhimu zaid "Soko" hana, kama una uwezo wa kumsaidia mawasiliano ya hao wafanya biashara wa Nairobi na huko kwingine ungemsaidia, atengeneze soko, pili ndio aende hapo tarakea

ngoja na mm nitie timu hapa, manake nafanya mambo haya haya , soko DSM linatunyoosha sio kidogo...
 
Asante sana broo....!!
 
Kweli mzee ..nashukuru umenielewa
 
0755 919 857....nakulink na huyu jamaa anasafirishaga shehena ya bidhaa tokea mwanza hadi Kenya kwa zaidi ya miongo kadhaa. Ana uzoefu wa kutosha.

Hopefully atakuwa msaada zaidi kwako.
 
Chukua mazao yako. Yapakize kwenye gari halafu washa gari uekeo elekea kenya.

Ni hayo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…