Nitashangaa na kusikitika kama hatutampongeza Dkt. Mwigulu Nchemba na kubadilika kwa ukweli mchungu huu

Nitashangaa na kusikitika kama hatutampongeza Dkt. Mwigulu Nchemba na kubadilika kwa ukweli mchungu huu

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"Watanzania waache kuwekeza sana katika Bajeti za Kunywa Pombe kila mara huku wakishindwa hata tu kukata Bima kitu ambacho nadhani kwa Mtu makini ni muhimu zaidi katika Maisha yake "

Chanzo: Cloudstv 360

Mtani wangu kutoka Mkoani Singida Dk. Mwigulu Nchemba unajua fika kuwa GENTAMYCINE sikukubali kutokana na Uyanga wako, ila nisiwe Mnafiki kwa hiki ulichokisema upo sahihi 100% na nakuunga mkono pia.

Binafsi nitajitahidi sasa nami hizi Bajeti zangu za kununua 'Migoma' ya Kwenu Singida pale Kimboka, Beach Kidimbwi na Maandazi Road Msasani nizielekeze katika Kukata Bima yangu kwani ni Aibu na Upopoma (Upumbavu) kama si Ungumbaru (Ujinga) mkubwa kufanya 'Anasa' huku ukiwa huna Bima yoyote.

Kidogo Mtani wangu Waziri Dk. Mwigulu Nchemba naanza sasa Kuiheshimu hiyo 'Doctorate' yako japo huko nyuma kuna Kauli zako fulani fulani zilikuwa zinanilazimisha nianze Kukupuuza kama si Kukudharau pia.
 
Mkubwa bima iko parefu mno
Si kweli kila Mtanzania akiamua Kuacha 'Anasa' au Matumizi ya 'Kipuuzi' na yasiyo ya lazima kuwa na Bima ( hasa ya Afya ) inawezekana. Tujitathmini na tubadilike tafadhali.
 
Mkuu mbona sijaona point kwake, kuwataka watu wanunue mafuta ndani eti uzalendo na wakati mpakani bei ni ya chini?
 
Mwigulu amewahi fanya biashara gani ukiacha hizo bla bla hapo.

FYI Bima ni Extra cost kwa watu wenye biashara kama zile za soko la Kariakoo. Mtu amekodi kizimba anauza vyombo sijui mashuka atakata bima ya kitu gani, ujuaji mwingi mbele giza
 
Mwigulu amewahi fanya biashara gani ukiacha hizo bla bla hapo.
FYI
Bima ni Extra cost kwa watu wenye biashara kama zile za soko la kariakoo... mtu amekodi kizimba anauza vyombo sijui mashuka atakata bima ya kitu gani ... ujuaji mwingi mbele giza

Du, mbona hoja yako ina kauli kavu na kali ujuaji mwingi mbele giza!

Ati Bima ni Extra cost! Faida ya Bima yoyote huwezi kuiona hadi unapofikwa na shida. Mfano ulio wazi ni pensheni (kwa waajiriwa) ambayo kimsingi ni "bima ya maisha baada ya kustaafu". Je, maisha ya wastaafu yangekuwaje kama haikuwa lazima (kisheria) kulipia pesheni kila mwezi kwa makato ya mshahara?

Ushauri wangu itungwe sheria kila leseni ya biashara iambatane na bima kama ilivyo kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri.
 
Wote ambao hawana BIMA ni walevi na wafanya ANASA?

Moja hizo BIMA sio value for money, and its due time hawa watu wakaelewa majority hawana disposable income, hata milo mitatu tu kwao haina uhakika, katika mavazi, malazi, chakula vyote hivyo ni luxury, kwahio wasijitoe ufahamu (hali sio shwari) na kizazi kijacho hiki ambacho wanasema kitafute ajira za kubangaiza kitaa ni kwamba hata pension za uzeeni watakuwa hawana.

In short its a disjointed community that we are building.
 
Usishangae sana mkuu.

Watanzania hatukose excuses kwa mambo yetu lakini tusiyotaka kuwajibikia.

Subiri tuje na hoja😂😂😂😂
 
Bima ni ya muhimu Sana kuna jamaangu mmoja ana gari la biashara baada ya kumshauri kukata bima na kuwa mbishi kwa muda mrefu alielewa somo akazama NMB akakata bima km zari gari likapata ajali alilipwa na watu wa insurance. Kudos Mwigulu nadhani wafanyabiashara waelimishwe umuhim wa bima.
 
Bila kupinga hizo habari za Mwigulu, sioni kwanini aende kutoa ufafanuzi wa jambo ambalo wameshalipitisha, bila kuja kwanza kwetu tujadiliane ili tutoe mawazo yetu?

Kimsingi bunge ni kama limeshashindwa wajibu wake, ni vyema kabla ya Jambo kupitishwa waje mitandaoni, na kwenye media waseme mipango yao kisha tuwahoji.
 
Tuliowahi kuishi na vichaa au punguwani, iko siku anaongea hadi unadhani kapona, kumbe hakuna kitu. Huyu bado hamna kitu!
 
Anashauri watu wasinywe pombe

Huku akipunguza Kodi kwenye pombe.

Contradictory.
 
Back
Top Bottom