Niulize Chochote kuhusu Goba

Goba ni mji unaokua kwa kasi ya ajabu
Thread hii natoa fursa kwa watu wanaotaka kuijua Goba kiundani zaidi kuuliza maswali na wenyeji wa Goba tutayajibu kadri tuwezavyo
Kwann Goba wanapenda sana kuvamia majumba hasa kwa wageni wanaohamia?? Hadi kujeruhi
 
Sio GO-BACK mkuu,
Wale vigagula wazee wa kizaramo walipokufa ndio mji huo ukaanza kujengwa na viwanja kuuzwa, zamani ilikuwa ukienda unarudi na kuwaachia hali yao kama palivyo hawakutaka changes, si unajua vichawi! Kwa hiyo una go back,
Dah hii historia umeipata wap
nlichosikia ni kuna mzee alikuwa anaitwa Goba
 
Goba ni mji unaokua kwa kasi ya ajabu
Thread hii natoa fursa kwa watu wanaotaka kuijua Goba kiundani zaidi kuuliza maswali na wenyeji wa Goba tutayajibu kadri tuwezavyo

Mtangazaji ' Mwandamizi ' wa Magic fm Oresti Kawau ( Baba tupake rangi ) anakaa kwa upande gani hapo Goba Mkuu? Nataka ' nikamtembelee ' tafadhali.
 
kunguru maji yashafika??
Uongozi unaturudisha nyuma Goba ilipaswa ifanyiwe distrubution ya maji kama mji uliokua teari,lakini Goba inachukuliwa kama bado ni kijiji ati maji yanatoka kwa wiki mara mbili kweny bomba moja la mtaa
 
Unalikumbuka basi la kijiji cha goba miaka ya 88. Lilikuwa dogo hivi na wazee wana siti zao hata apandie wapi atapishwa. Siti yake. Chako changu likiitwa
mkuu wew ni mkongwe wa Goba?
unakumbuka gari la Mangi miaka ya 2000 land rover bovu bovu hivi
 
Akikujibu nishtue
inategemeana sana, unaweza kuambiwa mil 5 mpaka 12 kwa kiwanja cha 20*20, inategemeana na location, ukaribu na barabara au majirani. unaweza kushangaa unaambiwa viwanja hapa ni bei ghali kisa jirani wamejenga watu maarufu
 
Nashawishika kuhamia goba ngoja nianze kutafuta hela ya kiwanja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…