Niunganishe soko la Kitunguu Kampala

Bei ya kitunguu maji na kitunguu swaumu Dar sahivi imefika sh ngapi?? Kwa anaejua msaada.
 
Yes mbegu zote za dukan ni kilo moja kwa eka moja au mara nyingine hata hata kilo moja inabaki.
Kuna jamaa yangu alisia Neptune F1 kwa uwiano wa kilo 2 kwa heka na ziliota vizuri kabisa, lakini bado hazikutosha.
 
Bei ya kitunguu maji na kitunguu swaumu Dar sahivi imefika sh ngapi?? Kwa anaejua msaada.
Bei ya Kitunguu
Kongowea Kenya: 5,000KSh./Gunia100Kg
Kawangware Kenya: 103,200TSh./Gunia120Kg
Kariakoo: 100,000TSh./Gunia100Kg
Lushoto: 110,000TSh./Gunia100Kg
Kirumba: 120,000TSh./Gunia100Kg
Arusha: 80,000TSh./Gunia100Kg
Makambako: 90,000TSh./Gunia120Kg
Morogoro: 90,000TSh./Gunia100Kg
Soweto: 74,000TSh./Gunia120Kg
: 146,000TSh./Gunia120Kg
Mwanakwerekwe ZnZ: 110,000TSh./Gunia120Kg
Dodoma: 70,000TSh./Gunia100Kg
Mombasa ZnZ: 120,000TSh./Gunia120Kg

Hizo bei ni kwa mujibu wa TAHA tarehe 28/11/2016
 
Kibali unaweza pata kwa madalali wa magari.Sababu nimesafirisha dagaa bila kibali wala nini,tulikua tunalipia gunia 1 sh 500/= kwa mwenye kibali.Tafuta market mkuu.


Na asanteni mlio haribu uzi wangu na kuja kubishania jinsi ya kulima kitunguu na ipi mbegu safi,wakati threads za mada kama hiz0 zinapatikana humu.
 
Uko vizuri mkuu,vp kuhusu Kampala ?
 
Nafikiri Hawa wanaouza mbegu hizi wengine sio waaminifu kabisa mbegu zinakuwa zime expiry, labda nitafute wakala mkubwa wa mbegu anaye eleweka
Balton arusha mkuu...wana mbegu bora na nzuri...unapewa na msaada jinsi ya kutunza zao lako likupe mazao mardadi
 


Sidhani Kama kila mtu ana fahamiana Na wenye vibali Au wanao safirisha dagaa mkuu. Lakini pia mwisho wa siku kibali Ni bure mkuu na ili kuepusha kukwamishwa ni bora kuwa Na chako.
 
Ahsante sana kwa mrejesho ndugu yangu Mungu akubariki sana.
 
Ha ha ha ha, wazoe kaka hii tabia mbona ipo sana, kuna jamaa mmoja nakumbuka alifungua thread ya kuomba msaada nini sijui sikumbuki vizuri, aiseh yan yaliyokuwa yanajadiliwa mengine na kichwa cha mada kingine kwahiyo wazoe ndugu zako ndivyo walivyo, ila ningewashauri kwa anaetaka kujua kuhusu mbegu bora ya kitunguu apitie kwenye uzi ule unaohusu maswala ya kilimo kuna mambo mengi sana yamejadiliwa kuhusu mbegu hope mtaambulia kitu tusiwe wavivu kusoma haya mambo yalishajadiliwa kipindi cha nyuma.
 
Mkuu yaani kitunguu kimoja tu nacho utafute soko la nje?

Kwani heka moja ya kitunguu si inaingia kwenye fuso moja? Sasa mzigo wa fuso moja unashindwaje kusafirishwa Kampala? Hata akisema anapeleka Darful la muhimu ni maslahi.
 
Kwani heka moja ya kitunguu si inaingia kwenye fuso moja? Sasa mzigo wa fuso moja unashindwaje kusafirishwa Kampala? Hata akisema anapeleka Darful la muhimu ni maslahi.
Hukunielewa mkuu nilikuwa namaanisha nini?
 
Huyo mhindi ndio anauza bei hiyo au?ukienda kariakoo kopo la gram 50 ni sh 6000 halafu chance ya kuota ni ishu
Nenda balton Changombe dar biashara na mswahili huwa hazina uhakika wao wana laana ya kupiga tu ndo wajuacho wanajali kupata hela ya Leo tu,na km zikiota wanaweka chache pia hawachelewi kukubandika.
 
Wamechafua uzi? Hakuna lililokusaidia kwenye hayo?
 
Fafanua tukuelewe lakini nahisi ulikuwa unambeza mdau kwa kutafuta mteja wa kitunguu nje ya nchi.
Unaona,, na wewe unarudia makosa yale yale! Hivi hili neno "Kitunguu" halina wingi? Hebu msiharibu lugha yetu mwanana ya Kiswahili mpaka imetinga AU siyo mchezo! Tujitahidi kuzungumza Kiswahili sahihi ili tusije tukaulizwa "huko shuleni huwa mnaenda kufanya nini?
 
Kamanda msimu wake umeishaumeisha kwa sasa
 
Mkuu naomba mrejesho ikiwa ulifaniiwa kuuza vitunguu nje ya nchi? Mimi pia natarajia kuvuna baada ya mwezi mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…