Niwashitaki wapi Airtel Money kwa uhuni walionifanyia?

Niwashitaki wapi Airtel Money kwa uhuni walionifanyia?

Nazjaz

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2011
Posts
7,730
Reaction score
9,088
Leo tarehe 28.10.2020 Airtel kwa kupitia huduma yao ya Airtel Money wamenisababishia usumbufu mkubwa sana, fedheha na kudharaulika kwa hali ya juu.

Nilikuwa nimeenda shambani Bagamoyo kupiga kura kwani ndiko nilikojiandikishia. Niliweza kupiga kura yangu vizuri, nikaingia shambani KUENDELEA na wajibu mwingine.

Baada ya kumaliza kazi za shambani nikaanza kujiandaa na safari. Nikaendesha hadi kituo cha mafuta nikawaagiza waniwekee mafuta ya elfu hamsini. Nikawekewa na kupewa risiti. Nilipoangalia pochi ndogo kwenye handbag nikagundua nimeiacha nyumbani.
Nikamuuliza pump attendant kama naweza kulipa kwa Airtel Money, akanijibu ndio, nikaingia kwenye menu ya miamala *150*60#.
Majibu naambiwa network error, mind you tayari mafuta yamo kwenye tank.

Nikajaribu kupiga namba 100 huduma kwa wateja, kimashine kinaongea utopolo usio na msaada, hamna unaweza kuongea na call center kwa msaada zaidi. Basi wahudumu wa kituo cha mafuta wakaniweka pembeni, nimedhalilishwa Sana, nimetukanwa, nimekebehiwa na nimefanyiwa dhihaka za kila aina, nimeitwa kila jina baya.

Bahati nzuri akatokea mtu ananifahamu, akaja kuangalia nimekutwa na Nini, nikampa kisa na mkasa, A to Z. Akanilipia 50k nikaondoka.
Nimeumia Sana, inakuwaje TCRA iruhusu kampuni ya mawasiliano itoe huduma bila ya kuwa na kitengo cha huduma kwa wateja? TCRA imeshindwa kuset quality control za service providers, nadhani TCRA iko na shida kubwa ya udhibiti.

Ndugu wajuzi naomba kujulishwa hatua za kufuata ili niwashitaki wahuni Hawa washike adabu
 
Pole kwa matusi, hongera kwa kumiliki gari na kuweza kuweka mafuta ya pesa taslimu 50,000.
Kweli wewe utaendelea kuwa hivyo. What is gari by the way? Unaumia mi kuwa na gari? Ukiwa na vyura wawili, mmoja mzuri na mwingine mbaya, na ukatakiwa uwale wote wakiwa hai, anza kumla yule mbaya zaidi.

Amka, ondoka na utoke kwenye comfort zone, kapambane huko nje kuna magari tele tele mazuri kuliko hii vanguard inayokupagawisha.
 
Very sad, ni ipi kazi ya TCRA? Yepi malengo ya kuanzishwa kwake?
Mara nyingi hizi taasisi zetu 'so called' za umma haziko kwa ajili ya umma bali zipo kwa ajili ya watawala. Kwahiyo hata tuumie vipi sisi 'umma' maadam haliwagusi watawala basi si tatizo kwao linalotakiwa kurekebishwa.

Hatari sana mkuu.

Sent from my SM-N910W8 using JamiiForums mobile app
 
Kweli wewe utaendelea kuwa hivyo. What is gari by the way? Unaumia mi kuwa na gari? Ukiwa na vyura wawili, mmoja mzuri na mwingine mbaya, na ukatakiwa uwale wote wakiwa hai, anza kumla yule mbaya zaidi.
Amka, ondoka na utoke kwenye comfort zone, kapambane huko nje kuna magari tele tele mazuri kuliko hii vanguard inayokupagawisha.
Duh yamekuwa hayo, hata sijakuelewa mimi sili chura. Kumbe una miliki Vanguard duh hizo gari za wenye hela, mimi pikipiki inanitosha kwa sasa, nikijaaliwa nitanunua Toyota IST kwa mkopo. Napita tu kufurahisha genge mara moja moja. Pole tena kwa mkasa uliokukuta uwe na siku njema.
 
Duh yamekuwa hayo, hata sijakuelewa mimi sili chura. Kumbe una miliki Vanguard duh hizo gari za wenye hela, mimi pikipiki inanitosha kwa sasa, nikijaaliwa nitanunua Toyota IST kwa mkopo. Napita tu kufurahisha genge mara moja moja. Pole tena kwa mkasa uliokukuta uwe na siku njema.
Namiliki na majoka pia, sumu nauza ulaya, nakula madola. Una swali zaidi?
 
Namiliki na majoka pia, sumu nauza ulaya, nakula madola. Una swali zaidi?
Mkuu upo vizuri ila kuweka mambo yote pembeni, kuhusiana na mkasa uliopata unaweza kupeleka malalamiko yako, taratibu zipo wazi kwenye "Terms and Conditions za Airtel Money" SECTION 18 kama hapo chini, ila ni zoezi refu sana ambalo litakupotezea muda, sana sana "out of good will" mtafanya settlement utakayopewa labda bundle ya data/voice/sms ambayo si kitu ukilinganisha na muda uliotumia.
new.png


Na pia angalizi muhimu kwako, kwenye Terms & Conditions ambazo ndio the only legally binding agreement kati yako wewe na Airtel Money:

1. Hakuna sehemu katika ambayo wewe kama mteja "Customer" upo entitled kuwasiliana directly na call center, claim waliyonayo ni kwamba hiyo 100 uliyopiga inatosha kukupatia msaada kama ungesikiliza kila chaguo walilokupatia.

2. Section "16. FAILURE OR MALFUNCTION OF EQUIPMENT" ya terms and conditions inawalinda kabisa kwa kutowafunga kukupatia "Guarantee of service" pale ambapo yatatokea mambo yaliyopo nje ya uwezo wao kama na hivi sasa kuna disruption kubwa ya internet services kwa nchi nzima ya Tanzania ambayo imefanywa bila any proper and public communication, hakuna directive yoyote uliyoiona kutoka TCRA mpaka sasa.
failure.png


Hiyo imeongelewa hata kwenye section "4. AIRTEL MONEY SERVICES" kama hapo chini.

service_1.png


Nyuma ya pazia mitandao ya simu inaweza kujiendesha kwa faida kwa kuumiza zaidi wateja kwa vifungu vidogo sana vinavyolinda maslahi yao na TCRA kwa sasa imejikita zaidi katika kulinda maslahi ya serikali kuliko maslahi ya raia.

Jaribu kuangalia Cybercrimes Act, 2015 toka imeanzishwa ni kesi ngapi zimelenga moja kwa moja kuhusu kulinda maslahi ya raia na hii ni sheria iliyotuaminisha itatusaidia kukabiliana na wahalifu wa mitandaoni, unaweza kwenda tu kutafuta simu yako iliyoibwa, usipokuwa makini na kumjua mtu sahihi, usumbufu wake unaweza kununua simu mpya na kuweka bundle hata kwa miezi 6.

Hata hivyo Electronic and Postal Communications (Consumer Protection) regulations zinawalazimu kuwa na call center inayopatikana 24/7 lakini pia humo humo inasema inabidi ufuate "escalation procedures " zilizowekwa na Airtel wenyewe kabla ya kwenda TCRA na kujaza fomu ya malalamiko.
complaints_part_3.png

walk_in.png


Taarifa zaidi ni hapo chini:

Unaweza kupambana kama suala la msingi wa haki kwa mteja bila kujali gharama yoyote kuna mahali inafika lazima msingi ifuatwe, mimi sio mwanasheria nimeandika kutokana na uzoefu niliowahi kupitia kupambana na mitandao ya simu kwenye masuala ya huduma za kibiashara si huduma binafsi, wanasheria wanaweza kuja hapa na kufafanua zaidi, na kunisahihisha kama kuna sehemu nimekosea ila ni zoezi ambalo lazima ujiandae kisaikolojia na kifedha kusimamia haki yako kama mtumiaji wa huduma ya Airtel Money.
 
Leo tarehe 28.10.2020 Airtel kwa kupitia huduma yao ya Airtel Money wamenisababishia usumbufu mkubwa sana, fedheha na kudharaulika kwa hali ya juu.

Nilikuwa nimeenda shambani Bagamoyo kupiga kura kwani ndiko nilikojiandikishia. Niliweza kupiga kura yangu vizuri, nikaingia shambani KUENDELEA na wajibu mwingine.

Baada ya kumaliza kazi za shambani nikaanza kujiandaa na safari. Nikaendesha hadi kituo cha mafuta nikawaagiza waniwekee mafuta ya elfu hamsini. Nikawekewa na kupewa risiti. Nilipoangalia pochi ndogo kwenye handbag nikagundua nimeiacha nyumbani.
Nikamuuliza pump attendant kama naweza kulipa kwa Airtel Money, akanijibu ndio, nikaingia kwenye menu ya miamala *150*60#.
Majibu naambiwa network error, mind you tayari mafuta yamo kwenye tank.

Nikajaribu kupiga namba 100 huduma kwa wateja, kimashine kinaongea utopolo usio na msaada, hamna unaweza kuongea na call center kwa msaada zaidi. Basi wahudumu wa kituo cha mafuta wakaniweka pembeni, nimedhalilishwa Sana, nimetukanwa, nimekebehiwa na nimefanyiwa dhihaka za kila aina, nimeitwa kila jina baya.

Bahati nzuri akatokea mtu ananifahamu, akaja kuangalia nimekutwa na Nini, nikampa kisa na mkasa, A to Z. Akanilipia 50k nikaondoka.
Nimeumia Sana, inakuwaje TCRA iruhusu kampuni ya mawasiliano itoe huduma bila ya kuwa na kitengo cha huduma kwa wateja? TCRA imeshindwa kuset quality control za service providers, nadhani TCRA iko na shida kubwa ya udhibiti.

Ndugu wajuzi naomba kujulishwa hatua za kufuata ili niwashitaki wahuni Hawa washike adabu
Siku hizi makampuni karibu yote ya simu wamefanya menu zao ziwe ngumu kuweza kuongea na huduma kwa wateja. Yani menu zao za kijinga sana sana
 
Siku hizi makampuni karibu yote ya simu wamefanya menu zao ziwe ngumu kuweza kuongea na huduma kwa wateja. Yani menu zao za kijinga sana sana
Wanaogopa Nini?
 
Back
Top Bottom