mwana wa africa
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 548
- 128
Hili swala ni very practicle. Cha kuongeze ni kwamba mkakati wenyewe wa kuraise hiyo milion 10 inabidi uupe muda kama miezi 15 hivi.
Vilevile ni vyema ukawa unaomba support badala ya kukopa kwa sababu huwezi kuwa na uhakika lini utapata full capital ya kuanzisha biashara. Kama idea ni nzuri watu watakuchangia tu. Na usiweke kiwango rasmi cha mtu kuchangia, take michango from as many people as possible.
Halafu maisha yako unayoishi kila siku yaonekane kweli ni mtu unayetafuta pesa kwa ajili ya shughuli fulani Watu hawawezi kukuchangia kama wanaona wewe unaendelea na starehe zako kama kawaida.
ni mtu gani atakae kuchangia tu kiivyo ulivyoelezea kirahisi?
@wote mliosema hii kitu inawezekana na ni rahisi, naombeni mnikopeshe tsh 500,000 each nifanye biashara na hapo hapo nichunguze kwa kuanzia humu kama hili jambo linawezekana au lah.
Ni ngumu sana siku hizi kumkopa mtu hata 50000 .00 kila mtu analalamika pesa ngumu
tatizo letu watanzania vitu vya muhimu tunaingiza uatani mwingi sana na kukatishana tamaa, si zani kama mwanzisha thread alieleza michango ichangwe kutoka humu jf.
Ni ngumu sana siku hizi kumkopa mtu hata 50000 .00 kila mtu analalamika pesa ngumu
tatizo watanzania tunapoona opportunity ambayo tunaweza elezea shida zetu na kusaidiwa huwa tunaambiwa hatupo serious. Mwanzisha thread kasema unaweza kuomba kwa watu wote unaofahamiana nao hata jf, facebook etc. Soma tena topic yake.
umeona hapo? Mtu unayemfata akusaidie anakwambia hana hela, hiyo hoja nzito utaijenga sa ngapi? Hata kama ulishaijenga na yeye hayupo tayari kusikiliza hoja zako utamlazimisha? Jamaa zako ni mifano mizuri inayoonesha kuwa hili jambo ni gumu.. Mimi niko field (ktk project kama tatu hivi) naona vijana/wazee walivyo na hela za nguvu. Lakini hao hao tukiwa mjini utawasikia ktk simu kwa jamaa zao wakilalamika kuwa hela hakuna.
mkuu ni kwa watu unao fahamiana nao, sasa mfano mimi nikuombe pesa nakufamu? Au kisa nakutana na wewe humu ndo nikuombe pesa?
Mimi nimesema mtu unaye fahamina nae yaani mnajuna si mtu mlie kutana nae facebook au members wa jf ukimbilie kumwomba pesa,
Naomba nikuunge mkono 10% only. Kuna Watz wengi wenye hela. Tatizo tunaohitaji hela zao zitusaidie hatujajenga hoja nzito na zilizojaa ushawishi ili hela hizo wazitoe kwetu. Mimi niko field (ktk project kama tatu hivi) naona vijana/wazee walivyo na hela za nguvu. Lakini hao hao tukiwa mjini utawasikia ktk simu kwa jamaa zao wakilalamika kuwa hela hakuna.
Tujenge hoja za nguvu ambazo hazina chembe ya hofu, huku tukiweka vitendo mbele kwa kupunguza maneno,tutachangiwa tu. Mbinu za kuwachangisha ni lazima ziwe za kisasa zaidi.
Siku hizi hata makanisani, ukiomba mchango usio na maelezo unatoka kapa.
umeona hapo? Mtu unayemfata akusaidie anakwambia hana hela, hiyo hoja nzito utaijenga sa ngapi? Hata kama ulishaijenga na yeye hayupo tayari kusikiliza hoja zako utamlazimisha? Jamaa zako ni mifano mizuri inayoonesha kuwa hili jambo ni gumu.
Kuna watu wana hela haswa ila ndio wanaongoza kwa kulalamika wana shida ikiwa ni kivuli cha kuepuka kusaidia wengine.
Heshima kwenu wadau,
Kibiashara kuna njia nyingi za kupata mtaji wa biashara hasa kwa zile zinazoanza ingawa nyingi kati ya hizo ni NGUMU sana, hivyo kupelekea watu wengi kuwa na mawazo mazuri ya kibiashara lakini hushindwa kuyafanikisha kutokana na mitaji. Kwa mtazamo wangu, naona kama ukitumia njia ya kuomba fedha kidogo kidogo kutoka kwa watu wengi walio karibu yako, wanaokuamini, kukuheshimu, kukufahamu na wenye uwezo kiasi itakuwa njia rahisi ukilinganisha na mikopo kutoka taasisi za kifedha ambapo utajikuta unafanya biashara kwa presha na hofu ya kurejesha deni. unaweza kufanya kama ifuatavyo kwa kuchukulia uhitaji wa mtaji wa Tsh 10,000,000:
1 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 100,000 kutoka kwa watu 100 = Tsh 10,000,000
2 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 200,000 kutoka kwa watu 50 = Tsh 10,000,000
3 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 350,000 kutoka kwa watu 30 = Tsh 10,000,000
4 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 500,000 kutoka kwa watu 20 = Tsh 10,000,000
5 - kuomba / kuazima / kukopa Tsh 1,000,000 kutoka kwa watu 10 = Tsh 10,000,000
NB: - Naamini tunafahamiana na watu wengi sana tangu mtoto unakua hadi hapo ulipo, kuanzia uliocheza nao, marafiki wa primary, sekondary, vyuo, kazini, majirani, ndugu, jamaa, marafiki, marafiki uliojuana nao kwenye mitandao kama JF, Facebook, Twitter nk..nina hakika hutakosa watu wasiopungua 100 wenye nia, uelewa na uwezo wa kukufanikishia hili.
- Uhitaji, madhumuni ya kuomba, muda wa kurejesha, malengo ya matumizi inategemea na makubaliano yako na unayemuomba, na si lazima hao watu utakao waomba wajue kusudio lako la njia hii ya kupata mtaji, pia usiombe kama msaada, omba kama mkopo ili baada ya muda mfupi kama miezi miwili ama mitatu uahidi kurejesha.
- Nina imani kiasi cha Tsh 10,000,000 ni mtaji tosha kwa biashara ndogo ndogo kwa kuanzia. Mfano: jiko la baa, kibanda cha chips, salon ya kiume, stationary, internet cafe, duka la jumla, duka la kawaida, genge, grecery, bajaji, duka la nguo hasa mitumba bomba nk.. ambapo itakuwa rahisi kwako kwa muda wa miezi mitatu kuweza kurejesha fedha ulizoomba.
Nawasilisha.