Afrolink-Tz Consult Ltd
JF-Expert Member
- Feb 25, 2018
- 424
- 950
Habari zenu wanaforum hii
Hakuna jambo jema na lenye furaha kama kuwekeza katika biashara au ujasiriamali na mambo yakakuendea vema kwani mafanikio ni ndoto na malengo ya kila mmojawetu pindi anapoamua kuwekeza, hakuna anaependa neno hasara au kufilisika kwani unakuwa umewekeza rasilimali fedha, maarifa na muda pia.
Lakini si kila anaeingia katika uwekezaji huweza "kutoboa" na kufikia kilele cha mafanikio yake atakayo. Tafiti zisizo rasmi zinaonyesha ya kwamba katika miaka mitano ya kwanza ya biashara nyingi zinazoanzisha asilimia 15 (15%) hufilisika ndani ya mwaka wa kwanza wa uwekezaji na asilimia hamsini tu (50%) ndiyo huweza kufika na kuvuka miaka mitano ya awali toka zianzishwe, asilimia thelathini na tano (35%) hufilisika kati ya mwaka wa pili hadi wa tano toka kuanzishwa kwake.
Hivyo ukiona umeanzisha biashara au ujasiriamali na toka kuanza kwako umevuka miaka mitano ya awali basi huna budi kujipongeza!
Zipo sababu nyingi zinazochangia kama uzoefu, ujuzi, kukosa watu sahihi, gharama za uwekezaji, mzunguko wa biashara nk.
Kwa leo napenda tuangalie je utabaki salama wewe mmiliki wa biashara dhidi ya madeni na mambo mengine kwa biashara yako inapofilisika?
Hebu tuangalie baadhi ya njia hizo:
1. Jitenge na biashara yako kisheria
Kuanzisha biashara kwa mtindo wa umiliki wa peke yako (sole proprietor) au kwa kushirikiana (partnership) ni rahisi sana na wenye gharama nafuu. Lakini mfumo huu hauwezi kukutenganisha na biashara yako pindi inapotokea majanga kama kufilisiwa kwani hakuna mpaka wa umiliki uliopo baina ya mali zako na wewe mmiliki binafsi. Hivyo basi ili ujitenge na janga la namna hii badili mfumo wa umiliki. Anzisha biashara lakini katika mfumo wa kampuni yenye ukomo (Private company limited by shares) kwanikampuni husimama kama "entity" inayojitegemea tofauti na wamiliki. Iwapo linapotokea janga la kufilisika bhasi wadeni wako watachukua mali za kampuni na sio zako binafsi
2. Usijitoe dhamana kwa mali yako binafsi
Hii mara nyingi hutokea katika masuala ya mikopo. Unakuta mwanahisa mmojawapo anaamua kutoa dhamana binafsi kama nyumba nk kwa ajili ya kuisapoti kampuni kuwezeshwa kifedha eg mkopo nk. Sasa kampuni inapokuja kushindwa kulipa mkopo au kufilisika dhamana yako binafsi nayo itabebwa. Acha kampuni ijisapoti yenyewe katika masuala ya kuwezeshwa.
3. Epuka kuwafanya wanafamilia/rafiki kuwa watendaji wakuu wa biashara yako labda wawe wanajua masuala ya biashara kwa ujumla wake
Ukifuatia kwa makini utaona katika Watanzania 5 wanaoanzisha biashara katika muundo wa kampuni zenye ukomo ni Mtanzania 1 tu anaekubali kuanzisha kampuni ya namna hiyo na mtu asiye na nasaba naye. Si vibaya kuanzsisha au kuweka wanahisa na watendaji wakuu wa kampuni kuwa wanafamilia au marafiki lakini je wanaufahamu juu ya nini wanachoenda kusimamia? Je biashara ikifilisika wanatambua nao wanawajibika binafsi katika kuhakikisha haki za wadeni zinalipwa? Hakikisha basi wawe wanajua A,B, Che za uendeshaji biashara na uwajibikaji juu ya madeni na mengineyo
4. Tumia wataalam wa biashara inapobidi
Jitahidi kuwatumia na kuwashirikisha wataalam mbalimbali katika biashara zako kujitenga na changamoto za biashara pindi inapofilisika.
Mfano mtumie mwanasheria kwa kila kielelzo unachoandaa au unachoweka kama dhamana kuisapoti biashara yako. Vilevile si vibaya kama utajisajili katika mamlaka za ufilisi na usajili wa mali, kwa Tanzania ni RITA (kama zipo mamlaka nyingine ongeza. hivyo hta kama biashara yako imefilisika wadenui wako watalipwa kwa utaratibu mzuri ulio chini ya usimamizi wa mamlaka husika na huwezi kuguswa mali zako binafsi
5. Jitangaze umefilisika kisheria
Wafanyabiashara wengi huona ni fedheha kubwa kutangaza hadharani kuwa biashara au kampuni yake imefilisika na kudhani ataifunga biashara au kampuni kienyeji/kinyemela na hatimaye wadeni watapotezea madeni. Hii sio rahisi kama tunavyodhani. Kampuni/biashara yako haiwezi kufungwa kirahisi kisheria kama bado ina madeni. Vilevile kuna changamoto kuu kwamba unaweza kuuza mali na kuwalipa wadeni lakini bado madeni yakawa hayajaisha na wadeni sio rahisi kuamini kuwa mali zimeisha zote hivyo hurudi katika mali zako binafsi kufidia madeni yao.
Sasa kama ulijisajili katika mamlaka yoyote iliyosajiliwa au mahakama itasimamia taratibu zote kisheria ikiwa pamoja na kutangaza na taratibu nyingine zoote za kuwalipa wadeni wako ilhali wewe upo "comfortable" dhidi ya kufilisika kwa biashara yako.
Karibuni tupeane maarifa zaidi
Hakuna jambo jema na lenye furaha kama kuwekeza katika biashara au ujasiriamali na mambo yakakuendea vema kwani mafanikio ni ndoto na malengo ya kila mmojawetu pindi anapoamua kuwekeza, hakuna anaependa neno hasara au kufilisika kwani unakuwa umewekeza rasilimali fedha, maarifa na muda pia.
Lakini si kila anaeingia katika uwekezaji huweza "kutoboa" na kufikia kilele cha mafanikio yake atakayo. Tafiti zisizo rasmi zinaonyesha ya kwamba katika miaka mitano ya kwanza ya biashara nyingi zinazoanzisha asilimia 15 (15%) hufilisika ndani ya mwaka wa kwanza wa uwekezaji na asilimia hamsini tu (50%) ndiyo huweza kufika na kuvuka miaka mitano ya awali toka zianzishwe, asilimia thelathini na tano (35%) hufilisika kati ya mwaka wa pili hadi wa tano toka kuanzishwa kwake.
Hivyo ukiona umeanzisha biashara au ujasiriamali na toka kuanza kwako umevuka miaka mitano ya awali basi huna budi kujipongeza!
Zipo sababu nyingi zinazochangia kama uzoefu, ujuzi, kukosa watu sahihi, gharama za uwekezaji, mzunguko wa biashara nk.
Kwa leo napenda tuangalie je utabaki salama wewe mmiliki wa biashara dhidi ya madeni na mambo mengine kwa biashara yako inapofilisika?
Hebu tuangalie baadhi ya njia hizo:
1. Jitenge na biashara yako kisheria
Kuanzisha biashara kwa mtindo wa umiliki wa peke yako (sole proprietor) au kwa kushirikiana (partnership) ni rahisi sana na wenye gharama nafuu. Lakini mfumo huu hauwezi kukutenganisha na biashara yako pindi inapotokea majanga kama kufilisiwa kwani hakuna mpaka wa umiliki uliopo baina ya mali zako na wewe mmiliki binafsi. Hivyo basi ili ujitenge na janga la namna hii badili mfumo wa umiliki. Anzisha biashara lakini katika mfumo wa kampuni yenye ukomo (Private company limited by shares) kwanikampuni husimama kama "entity" inayojitegemea tofauti na wamiliki. Iwapo linapotokea janga la kufilisika bhasi wadeni wako watachukua mali za kampuni na sio zako binafsi
2. Usijitoe dhamana kwa mali yako binafsi
Hii mara nyingi hutokea katika masuala ya mikopo. Unakuta mwanahisa mmojawapo anaamua kutoa dhamana binafsi kama nyumba nk kwa ajili ya kuisapoti kampuni kuwezeshwa kifedha eg mkopo nk. Sasa kampuni inapokuja kushindwa kulipa mkopo au kufilisika dhamana yako binafsi nayo itabebwa. Acha kampuni ijisapoti yenyewe katika masuala ya kuwezeshwa.
3. Epuka kuwafanya wanafamilia/rafiki kuwa watendaji wakuu wa biashara yako labda wawe wanajua masuala ya biashara kwa ujumla wake
Ukifuatia kwa makini utaona katika Watanzania 5 wanaoanzisha biashara katika muundo wa kampuni zenye ukomo ni Mtanzania 1 tu anaekubali kuanzisha kampuni ya namna hiyo na mtu asiye na nasaba naye. Si vibaya kuanzsisha au kuweka wanahisa na watendaji wakuu wa kampuni kuwa wanafamilia au marafiki lakini je wanaufahamu juu ya nini wanachoenda kusimamia? Je biashara ikifilisika wanatambua nao wanawajibika binafsi katika kuhakikisha haki za wadeni zinalipwa? Hakikisha basi wawe wanajua A,B, Che za uendeshaji biashara na uwajibikaji juu ya madeni na mengineyo
4. Tumia wataalam wa biashara inapobidi
Jitahidi kuwatumia na kuwashirikisha wataalam mbalimbali katika biashara zako kujitenga na changamoto za biashara pindi inapofilisika.
Mfano mtumie mwanasheria kwa kila kielelzo unachoandaa au unachoweka kama dhamana kuisapoti biashara yako. Vilevile si vibaya kama utajisajili katika mamlaka za ufilisi na usajili wa mali, kwa Tanzania ni RITA (kama zipo mamlaka nyingine ongeza. hivyo hta kama biashara yako imefilisika wadenui wako watalipwa kwa utaratibu mzuri ulio chini ya usimamizi wa mamlaka husika na huwezi kuguswa mali zako binafsi
5. Jitangaze umefilisika kisheria
Wafanyabiashara wengi huona ni fedheha kubwa kutangaza hadharani kuwa biashara au kampuni yake imefilisika na kudhani ataifunga biashara au kampuni kienyeji/kinyemela na hatimaye wadeni watapotezea madeni. Hii sio rahisi kama tunavyodhani. Kampuni/biashara yako haiwezi kufungwa kirahisi kisheria kama bado ina madeni. Vilevile kuna changamoto kuu kwamba unaweza kuuza mali na kuwalipa wadeni lakini bado madeni yakawa hayajaisha na wadeni sio rahisi kuamini kuwa mali zimeisha zote hivyo hurudi katika mali zako binafsi kufidia madeni yao.
Sasa kama ulijisajili katika mamlaka yoyote iliyosajiliwa au mahakama itasimamia taratibu zote kisheria ikiwa pamoja na kutangaza na taratibu nyingine zoote za kuwalipa wadeni wako ilhali wewe upo "comfortable" dhidi ya kufilisika kwa biashara yako.
Karibuni tupeane maarifa zaidi