Njia ya Kutokea: Kabla ya Mengine kupitia Ibara Nyingine Waamue kwanza Muundo wa Muungano!

Njia ya Kutokea: Kabla ya Mengine kupitia Ibara Nyingine Waamue kwanza Muundo wa Muungano!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
M. M. Mwanakijiji

Bunge la Katiba linaweza kujikuta linatumia fedha nyingi na muda na mwisho likakwama kwenye suala la Muundo wa Muungano kwenye sura ya sita ya rasimu ya Katiba. Lakini hili peke yake si sababu kubwa ya mimi kupendekeza kuwa kabla ya kwenda mbali na kupitia vifungu vingine vya rasimu hiyo wajumbe waamue kwanza suala la muundo wa Muungano kwanza. Kuna sababu moja kubwa.


Rasimu ya Katiba ilivyo sasa imeandikwa na kupangwa ikiwa imedhania (assume) kuwa kutakuwepo na Serikali tatu. Kwamba Ibara zake nyingi na muundo wake umefikiria kuwa Bunge la wananchi watakubali uwepo wa serikali tatu na kuridhia mfumo wa Shirikisho lenye nchi mbili na serikali tatu – Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano.

Kutokana na ukweli huo basi suala la uwepo wa Tanganyika na vyombo vyake vya kiutawala – Mahakama, Baraza la Wawakilishi, Waziri Mkuu (Rais wake) ni la muhimu zaidi kuliko kuendelea na mchakato huu ulivyo sasa. Bunge halipaswi kuendelea na kupitia vifungu vingine vya rasimu bila kuamua kwanza aina ya muundo wa Muungano – kama ni Serikali Mbili, Moja au Tatu kama inavyopendekezwa.

Pande Mbili Zinazokinzana
Hadi hivi sasa ni wazi kuwa upo upande mmoja unaotaka kuendelea kwa mfumo wa Serikali Mbili na wapo wale ambao wanapendekeza mfumo wa Serikali Tatu. Sasa, vyovyote itakavyokuwa kuna matokeo mawili yanayowezekana:

Moja, Wanaotaka Serikali mbili – wengi wakiwa ni wana CCM – wakashinda na hivyo rasimu ya Katiba ni LAZIMA ifanyiwe marekebiso makubwa na Bunge la Katiba ili kuondoa vipengele vinavyozungumzia muundo wa serikali tatu;

Pili, wanaotaka Serikali Tatu – wapo wana CCM na wapinzani – wakashinda na hivyo rasimu ya Katiba kuweza kuendelea bila mabadiliko makubwa ya kimuundo. Hata hivyo kukubalika kwa serikali tatu kutalazimisha mchakato huu wa Katiba ulilvyo sasa usitishwe kwani kwa maoni yangu – na kwa unyenyekevu nayatoa – Bunge hili Maalum la Katiba halipaswi kujadili rasimu ya Katiba ya Muungano bila wawakilishi kutoka vyombo na wananchi wa Tanganyika.

Nini kifanyike basi?


  1. Baada ya Mwenyekiti na Makamu wake kupatikana na wajumbe wote kuapishwa na baada ya taratibu zote za mwanzo kuwa tayari basi badala ya kuanza kupitia ibara za kwanza za Katiba ambazo hazina utata sana napendekeza wajumbe waende moja kwa moja kwenye moyo wa rasimu – Muundo wa Muungano. Hili liamuliwe kabla kwenda kuamua mambo mengine – kama ni serikali mbili au tatu lijulikane mapema kwani ibara nyingine zote (ukiondoa zile za mwanzo) zinasimama na kuanguka na Sehemu ya Sita ya rasimu ya Katiba.
  2. Endapo itapitishwa Serikali Tatu basi Bunge la Katiba lisitiswe kwa muda (indefinitely) hadi pale ambapo Tanganyika itakapokuwa na Katiba yake, Bunge lake na wawakilishi wake ambao wataingia kwenye Bunge la Katiba. Ikumbukwe hadi hivi sasa hakuna wawakilishi wa Tanganyika wa aina yoyote wakati Zanzibar ina wawakilishi wake.
  3. Baada ya Bunge Maalum kuridhia uwepo wa Serikali ya Tanganyika basu Bunge la kawaida liitishwe mara moja na kufanyia marekebiso Katiba ya sasa chini ya Ibara ya 98 ili kuruhusu kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na vyombo vyake; mabadiliko hayo ya Katiba yaridhiwe na Baraza la Wawakilishi kwa mujibu wa Katiba.
  4. Mabadiliko hayo ya Katiba ya sasa yaweke utaratibu wa wananchi wa Tanganyika kutunga Katiba yao na kufanya uchaguzi wao mkuu ili kujipatia viongozi wake wa kitaifa na wawakilisi; uchaguzi huo ufanyike mapema mwakani ambapo viongozi wote wa kitaifa watapatikana wakiwemo wa Bunge wa Bunge la Tanganyika (sijui litaitwa Baraza la Wawakilishi au Seneti sijui)
  5. Wakati wananchi wa Tanganyika wanafanya mchakato wa kurudisha serikali yao na vyombo vyake vyote (pamoja na alama zake za kitaifa, wimbo wa taifa, bendera n.k) Mchakato wa Katiba Mpya wa hivi sasa utakuwa umesitishwa.
  6. Baada ya Serikali ya Tanganyika kurudi basi suala kubwa la kwanza ambalo litahitaji kuamuliwa ni kama tunahitaji kuendelea kuwa Muungano. Hili litafanyika kwa kupigwa kwa kura ya maoni pande mbili za Muungano – na endapo kila upande utapata angalau asilimia 60 ya wapiga kura kukubali Muungano basi hatua za kuendelea kuandika Katiba Mpya itabidi zifuatwe; kinyume chake utaratibu wa utengano ufanyike ili hatimaye kupatikane mataifa mawili jirani ambayo yatakuwa na uhuru kamili yakidumisha ushirikiano wa kimataifa wan chi jirani.
  7. Endapo wananchi wa Tanganyika na Zanzibar watataka uwepo Muungano basi Baada ya Serikali ya Tanganyika kurudi na kuanza kazi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atavunja Baraza la Mawaziri la sasa na kuzingatia mabadiliko yale ya Katiba (namba 3 hapo juu) kuingiza katika Serikali ya Muungano wa wakilishi kutoka Serikali ya Tanganyika kwa ajili ya masuala ya Muungano na hivyo kupunguza ukubwa. Hili linaweza kuwa rais kufanyika chini ya Rais Kikwete ambaye atasimamia serikali ya mpito kuelekea uundwaji wa Katiba Mpya na Uchaguzi Mkuu Mpya mwishoni mwa mwaka 2015.
Kama kutakuwa na Utengano basi Rais Kikwete atakuwa ni Rais wa Mwisho wa Tanzania iliyoungana na atasimamia serikali ya mpito na makubaliano ya mambo mbalimbali kabla ya Tanganyika na Zanzibar kuachana kuelekea uchaguzi mkuu wa kila nchi. Uwepo wa Serikali ya Tanganyika utasimamia maslahi ya Tanganyika katika kuelekea Utengano huo.

  1. Kama kutakuwa na Muungano wa Serikali tatu basi Bunge Maalum la Katiba liitwe wakati Sheria yake ikiwa imefanyikwa mabadiliko makubwa ya kimfumo ili liakisi uwepo wa Serikali na Wawakilishi kutoka Tanganyika na kutoka hapo mchakato wa Katiba Mpya Muungano uanze upya ili kuhakikisha Katiba Mpya inapatikana kwa njia nzuri zaidi.

Naamini kuendelea na mchakato huu ulivyo sasa bila kuamua masuala haya makubwa ni kujaribu kukwepa kiini cha mgogoro. Wajumbe hawawezi kuendeleea kujadili mambo mengine kabla ya kuamua aina ya Muungano utakaokuwepo; kama utakuwepo. Naamini na napendekeza kuwa waamue kwanza suala la muundo wa Muungano kwani ni kutoka hapo ndiyo mambo mengine yataeleweka.

Napendekeza.
 
Mkuu
Mbona kiini cha mgogoro kilikkuwepo hata kabla ya mchakato?
Tulionya kuwa lazima suala la kura ya maoni kujua kama watu wanataka muungano na wa aina gani, hawataki tuvunje jahazi n.k. ni muhimu kabla ya mchakato. Nashangaa tume ya Warioba iliyosheheni wasomi na watu wenye busara haikuona tatizo hilo mapema.

Rasimu yote ipo katika muundo wa serikali 3. Hakuna kipengele kisichogusa muundo wa serikali.
Ugumu wa vifungu 37 na 38 ni dalili nzuri kuwa mbele ya safari kuna tatizo kubwa.

Wasi wasi wangu ni kuwa ikitokea katiba ikaandikwa, hivi Tnganyika akizunduka na kuja na yake itakuwaje.
Tanganyika atakuwa na haki ya kusema sikushirikishwa wakati nipo katika dawa ya usingizi. Sasa nina fahamu zangu nimezinduka, hiki ndicho ninataka. Hivi hatutarudi kule kwa Baraza la wawakilizshi zanzibar kupora mamlaka na kuwa juu ya JMT?
 
Mkuu
Mbona kiini cha mgogoro kilikkuwepo hata kabla ya mchakato?
Tulionya kuwa lazima suala la kura ya maoni kujua kama watu wanataka muungano na wa aina gani, hawataki tuvunje jahazi n.k. ni muhimu kabla ya mchakato. Nashangaa tume ya Warioba iliyosheheni wasomi na watu wenye busara haikuona tatizo hilo mapema.

Rasimu yote ipo katika muundo wa serikali 3. Hakuna kipengele kisichogusa muundo wa serikali.
Ugumu wa vifungu 37 na 38 ni dalili nzuri kuwa mbele ya safari kuna tatizo kubwa.

Wasi wasi wangu ni kuwa ikitokea katiba ikaandikwa, hivi Tnganyika akizunduka na kuja na yake itakuwaje.
Tanganyika atakuwa na haki ya kusema sikushirikishwa wakati nipo katika dawa ya usingizi. Sasa nina fahamu zangu nimezinduka, hiki ndicho ninataka. Hivi hatutarudi kule kwa Baraza la wawakilizshi zanzibar kupora mamlaka na kuwa juu ya JMT?
Mkuu nguruvi kwa aina hii ya mchakato na Jinsi ulivyo kamwe hamna katiba mpya itakayopatikana naona kodi za watanzania zikiteketea bure.
 
Last edited by a moderator:
Mwanakijiji ulipashwa kuwa mjumbe wa bunge la katiba una mawazo mazuri
 
MM Mwanakijiji, kimantiki, hayo uliyoyasema ndio hasa yanatakiwa kufuatwa na kutekelezwa ili kukidhi matakwa ya kisheria. Tatizo ni nani mwenye BUsara ya kuyaona hayo unayoyapendekeza?? Sioni CCM au hao Wapinzani wa CCM kuwa na hiyo busara.Wote macho na masikio yao bila kusahau akili zao zinaangalia 2015. Kama walivyokwama kupitisha rasimu ya kanuni ibara ya 37 na 38, nachelea kusema itakapofika muda wa kujadili rasimu ya katiba na hasa hiyo ibara ya sita inayohusu aina ya serikali ya muungano, basi yaliyotokea kwenye rsimu ya kanuni ndio yatatokea kwenye rasimu ya katiba. Tumuombe Mungu awajaalie wajumbe wa bunge la katiba kuiona busara hii unayoieleza hapa. NAUNGA MKONO HOJA
 
Kwa sasa nina haya yakuandika.

Mimi nadhani tuondoe hofu inayoletwa na Katiba ya Sasa ya JMT, kuwa muungano ni lazima. Hivyo tuhoji wananchi (mimi nikiwemo) kwanza kama wanataka muungano ama hawautaki kwa njia ya kura ya siri.

Wakisema hawautaki muungano moja kwa moja tuanze kuziimarisha serikali mbili huru zenye uwakilishi UN yaani serikali ya Zanzibar huru na serikali ya Tanzania Bara huru.

Wakisema wanautaka muungano tuwahoji tena (kwa kura ya siri) kama wanataka serikali moja, tatu, nne, n.k.

Tukisha kujua ni wananchi wanataka serikali ngapi, itakuwa rahisi sana kutunga Katiba ya nchi husika ambayo wala haitaleta mizengwe kama ya sasa.
 
theory ya srekali ngapi zote zilikuwemo kwenye mawazo ya wajumbe wa tume, hususana ya serikali mbili, lakini mabadiliko ya katiba ya zanzibar yalikwamisha hilo pamoja na dhana ya tanganyika/bara kuvaa koti la muungano hivyo kuwabana wa znz/visiwani, so practical likawa hilo la serikali tatu. uzuri wa serikali moja wenzetu hawajaliona hilo sababu ya kutokuwepo kwa serikali tatu na kauli ya samaki mkubwa kumeza mdogo, sasa twende kwenye serikali tatu kuelekea moja, maana koti lililovaliwa na bara katika serikali mbili zilizo sasa linawabana wenzetu, tukilivuwa wataliona linavyo wapwaya.
 
Mkuu
Mbona kiini cha mgogoro kilikkuwepo hata kabla ya mchakato?
Tulionya kuwa lazima suala la kura ya maoni kujua kama watu wanataka muungano na wa aina gani, hawataki tuvunje jahazi n.k. ni muhimu kabla ya mchakato. Nashangaa tume ya Warioba iliyosheheni wasomi na watu wenye busara haikuona tatizo hilo mapema.

Rasimu yote ipo katika muundo wa serikali 3. Hakuna kipengele kisichogusa muundo wa serikali.
Ugumu wa vifungu 37 na 38 ni dalili nzuri kuwa mbele ya safari kuna tatizo kubwa.

Wasi wasi wangu ni kuwa ikitokea katiba ikaandikwa, hivi Tnganyika akizunduka na kuja na yake itakuwaje.
Tanganyika atakuwa na haki ya kusema sikushirikishwa wakati nipo katika dawa ya usingizi. Sasa nina fahamu zangu nimezinduka, hiki ndicho ninataka. Hivi hatutarudi kule kwa Baraza la wawakilizshi zanzibar kupora mamlaka na kuwa juu ya JMT?



Nguruvi- hapa ndipo pana tatizo na siyo kwamba magenious wetu hawalioni. Wakiendelea hivi watakwama halafu watashindwa kuona namna ya kutoka. Upande mwingine ni suala la posho...hawawezi kusitisha mchakato kwa sababu kuna watu wameshachukua na mikopo tayari
 
Back
Top Bottom