SoC02 Njia za uchumi na furaha ya kudumu

Stories of Change - 2022 Competition

MlakiKaskazi

Member
Joined
Aug 11, 2022
Posts
10
Reaction score
8
Wakati tulionao jambo kubwa zaidi kwa watu wengi ni kujimudu kimaisha. Kila mtu anaamini ili aheshimike anahitaji kujiepusha kuwa tegemezi kwa watu wengine.

Wengi tunaamini kuwa na uchumi mzuri ndio msingi wa furaha maishani. Hili ni kweli japo sio msingi pekee. Swali la msingi la kujiuliza hapa ni "je kila njia ya kutafuta uchumi/kipato inaleta furaha tunayoitafuta?"

Ukiangalia vijana wengi hapa Tanzania utagundua kuwa wengi wao wanachanganya kati ya 'furaha' na 'raha'.

Ilipokuwa lengo ni kuwa na uchumi mzuri watu wengi hawajali kuhusu njia wanazotumia kupata huo uchumi.

Mathalani wapo vijana wanaonekana kuwa na maisha mazuri lakini wanajihusisha na tabia hatarishi kama uwizi, ulaghai, uasherati, ushoga n.k

"Uchumi unaotokana na mambo ambayo sio sahihi hauwezi kukuletea 'furaha' maishani badala yake utapata 'raha' kitu ambacho si cha kudumu."

Haya yalikuwa maneno ya kijana Kaba mzaliwa wa Kilimanjaro, mbele ya wafungwa wenzake baada ya kutafakari Mapito yake kwenye maisha na alipo sasa.
 
Upvote 3
Mwanamuziki R.Kelly ni mfano wa mtu ambaye alishindwa kutofautisha kati ya raha na furaha... matokeo yake yupo alipo leo hii ijapokuwa kuna kipindi alikuwa katika kilele cha mafanikio kwenye macho ya wengi! wengine ni wakina Michael Jackson, Whitney, na Chungu ya watu maarufu wa zamani ndani na nje ya nchi.
 
Hayo yote yamechangizwa na utandawazi, kwenye social media zote wanaopata likes na followers wengi ni wale wanaoanika maisha ya anasa na starehe wanazofanya.

Wadada wenye macho matatu, ndinga kali, makeup za nguvu, mavazi yanayoendana na fashion za kisasa pamoja na posts za airport, hotelini na viwanja mbalimbali ndio habari ya mjini.

Mabinti na vijana wengi wanatamani kuishi maisha ya maonesho kama waonayo kwenye mitandao. Role models wa vijana wengi wamekuwa ni wasanii na socialites.

Hili limefanya vijana wengi kutafuta hela kwa mbinu yoyote ile iwe kuuwa, ushoga, kuuza madawa, kutumika, uchawi n.k ilimradi wapate raha.

Ni funzo kubwa sana kutofautisha raha na furaha.
 
Kabisa, unakuta mtu anatesa leo, ila baada ya miaka 10 ni kama hujawahi kushika hela maisha yake yote. Wanaishia kuhadithia tu

Bora kipato cha kawaida lakini kinacholeta amani na furaha kwenye maisha
 
Kabisa, unakuta mtu anatesa leo, ila baada ya miaka 10 ni kama hujawahi kushika hela maisha yake yote. Wanaishia kuhadithia tu

Bora kipato cha kawaida lakini kinacholeta amani na furaha kwenye maisha
Mfano mwingine siku hizi kuna kitu kinaitwa "uchawa" ni kama aina ya upambe iliyoendelea zaidi.
Wanaume watu wazima wenye familia wanakuwa na kazi ya kuwasifia wasanii wanaoonekana wameendelea au watu wengine maarufu kwenye kila kitu.
Hizo sifa sio bure, wanapata hela na magari (kama inavyotangazwa)
Hii tabia inampa mtu pesa lakini inaharibu heshima yake kwa sababu inafanya mtu aonekane wa hovyo na inashusha hata heshima ya familia mbele ya jamii iliyostaarabika.
Lakini machawa hawajali kwa kuwa wanapata pesa na hicho ndio kipaumbele chao.

Kwa mtu mwanaume wa kisawa sawa hawezi kuwa na kazi ya kusifia wanaume wengine mpaka kwenye ujinga ilimradi tu mkono uende kinywani.
Wakati mwingine hawa machawa huingia kwenye ugomvi usio na tija mfano mwanaume mbaba mtu mzima anagombana hadi na wanawake waliowahi kuwa kwenye mahusiano na wale matajiri wanaowaweka mjini.

Machawa wengine wanatuhumiwa kwa tabia zisizofaa kama ushoga, utapeli nk.

Watu wa aina hii wanapata raha (baadhi ya nyakati) lakini hawana furaha ya kudumu kwa kuwa njia wanayoitumia sio ya sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…