Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Sintofahamu imetokea mkoani Njombe na hii ni baada ya moto ambao bado haujafahamika chanzo chake kuwaka na kuteketeza eneo la kituo cha kusambaza umeme mkoani humo.
Mara tu baada ya kudhibiti moto huo, Kaimu meneja wa TANESCO mkoa wa Njombe Mhandisi Lazaro Bartazai alidokeza kuwa hakuna athari kubwa zilizojitokeza kutokana na moto huo na kuongeza kuwa wanaendelea kufanya tathmini ya athari zilizopatikana.
Injinia Lazaro Joel Mwakanyasa Mrakibu msaidizi wa jeshi la zimamoto na uokoaji ambaye ni kaimu kamanda wa jeshi la Zimamoto mkoa wa Njombe amesema wakati tukio hilo likitokea tarehe 4 Septemba 2024, majira ya saa tisa na nusu alasiri walipokea taarifa kutoka kwa raia mwema juu ya moto kuwaka eneo la kituo na kufika mapema kuudhibiti moto huo.
Aidha ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Njombe kuwa makini wanapochoma moto ili kutokuleta madhara ikiwamo kuchoma miundombinu iliyojengwa na serikali kwa gharama
Soma pia: Njombe: Afariki ndani ya gari akiota moto kwenye jiko la mkaa
Source: Jambo Online
Mara tu baada ya kudhibiti moto huo, Kaimu meneja wa TANESCO mkoa wa Njombe Mhandisi Lazaro Bartazai alidokeza kuwa hakuna athari kubwa zilizojitokeza kutokana na moto huo na kuongeza kuwa wanaendelea kufanya tathmini ya athari zilizopatikana.
"Kilichotokea mpaka tukakata umeme ni moto umeunguza maeneo ya store jirani na kituo chetu cha kusambazia umeme lakini haujaleta athari kubwa"
Injinia Lazaro Joel Mwakanyasa Mrakibu msaidizi wa jeshi la zimamoto na uokoaji ambaye ni kaimu kamanda wa jeshi la Zimamoto mkoa wa Njombe amesema wakati tukio hilo likitokea tarehe 4 Septemba 2024, majira ya saa tisa na nusu alasiri walipokea taarifa kutoka kwa raia mwema juu ya moto kuwaka eneo la kituo na kufika mapema kuudhibiti moto huo.
"Tulikuta moto umeshaanza kuwaka lakini kwa kushirikiana naa wanachi pamoja na wafanyakazi wa TANESCO tulishirikiana kuuzima lakini chanzo cha moto hatujatambua chanzo"
Aidha ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Njombe kuwa makini wanapochoma moto ili kutokuleta madhara ikiwamo kuchoma miundombinu iliyojengwa na serikali kwa gharama
Soma pia: Njombe: Afariki ndani ya gari akiota moto kwenye jiko la mkaa
Source: Jambo Online