Prince Tumbo
JF-Expert Member
- Apr 5, 2013
- 910
- 247
Kwanza niombe radhi kwa wateja wote wa benki hii. Benki hii huitwa na hujulikana hivo kwa kiswahili na jina hili liliasisiwa na Rais mstaafu Benjamin William Mkapa katika kuianzisha. NMB ni kirefu cha maneno National Micro-Finance Bank, sio tofasiri ya neno la kiswahili,haviendani hata kidogo na "kabwela". Maana ya neno kabwela ni "maskini" jina hili sio nick name, ni official name. Wateja wa benki hii wengi ni walimu na watumishi wengi wa serikali ambao serikali iliweka utaratibu wa kulipa mishahara yao kupitia benki hii. Ni kwa sababu zipi serikali iliamua kutumia neno hili la kuudhi na kudhalilisha wateja?...au ndugu zangu,labda mimi sielewi maana ya neno hili?...kama wengi tunafahamu neno hili "kabwela-maskini" ni vizuri serikali i-withdraw hili neno...naomba maoni yako....