NMB KLiK - Benki Kiganjani mwako

kuna huduma gani humo? mnaweza toa mikopo kwa kupitia huduma hio tu bila kufika kwenu?
Salaam sana Kivumah

Kwa kutumia NMB KLiK unaweza kufanya mengi zaidi ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti ya benki, kufanya miamala mbalimbali ya kibenki na malipo ya huduma na bidhaa, na pia kufanya uwekezaji wa fedha zako kupitia akaunti maalumu (Fixed Account) karibu ujiunge nasi katika safari ya ulimwengu wa kidijitali.

Asante
 
Mkuu,mimi ni mteja wenu tangu kitambo...vp naweza kupata huduma ya loan salary advance (kupatiwa kiasi kidogo cha fedha then mkopo ukitoka mnanikata kwenye salary!
 
Hongereni mmejitahidi, nimeipakua nakuijaribu kuitumia ipo vizuri sana, mmejitahidi.
Mkuu unaweza kuelezea japo machache kuhusu hiyo App?

Nimepokea SMS muda si mrefu ila nimesita kujitosa kuipakua kwanza ili nijiridhishe na yaliyomo kupitia habari kama hizi
 
Ile nmb appy ya zamani imekufa?

Na je ina tofauti gani na hii?

Hii haitakufa kama ile ya mwanzo?
 
ipo vizuri sana tofauti na App ya Zamani hii imekaa vizuri. Nimefurahi hakika
 
Nikiwa na app yenu hii nitakatwa Bundle Tu wakati nafanya miamala ama nitakatwa na pesa katika akaunti yangu?
 
Nmb kiliki amepotea ghafla... Au ana endelea kuhudumia Wateja katk app
 
why sisi tunaotumia windows phone mnatutenga!??kwahiyo sisi hatustahili kuwa na hizo NMB app!?Please be considerably
Hello Tony,
Tunafanyia kazi suala hili na mtapata huduma hii, kwa sasa unaweza ku KLiK kupitia *150*66# na kufaidi huduma zetu.
 
Mkuu,mimi ni mteja wenu tangu kitambo...vp naweza kupata huduma ya loan salary advance (kupatiwa kiasi kidogo cha fedha then mkopo ukitoka mnanikata kwenye salary!
Naam ndugu Monde,
Huduma hiyo inapatikana kama unapitishia mshahara kwenye akaunti yako ya NMB na kuwe na makubaliano ya mwajili wako na sisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…