ndege joni
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 682
- 1,108
Sitaki kuongea sana ila mimi ni mtumishi wa umma, niliomba mkopo kwa ajili ya dharura ya kifamilia mwezi umepita. Nilifuata taratibu zote ila baada ya kila kitu kufanyika na makato kuingizwa kwenye mfumo na afisa utumishi.... form zilirudi kwa afisa mikopo. Cha ajabu tangu form zirudi kutoka utumishi ni wiki 3 na sijaona hako kamkopo na sikahitaji kwa sasa kwa sababu nimeshatatua tatizo langu. Najiuliza, hivi hawa maafisa mikopo kibiri hiki wanakitoa wapi? Pale ofisini ukienda mara nyingi hawapo wakati kazi yao ni kutoa mikopo... wanakuwa wapi? Kama wanataka rushwa si waseme tutoe? Nilimpigia simu mara nyingi hajawahi kupokea na kunujibu sms zangu. Kosa langu ni kuomba mkopo kwao? Kwamba hakuna taasisi nyingine za kukopesha?