NNA PRESHA AFU NIMEBETI

Ingawa betting is not my forte ila I Know what am talking about
 
hahah *****, hiyo laki bora ungenunua maji ya kilimanjaro then uoge nayo.
 

Man City kafanya yake naona.
 
Polee mkuu juve na man city wamekuponza
 
Kanjibai sio mtu mzuri yaani we bet unavyoweza,lakini atatokea mmoja tu tena ambaye humtarajii anakuja anachana mkeka..yaani muhindi sijui mchawi
Kuna siku ilikuwa Europa league nilikuwa nimetambaa kwelikweli yani mikeka nilikuwa nayo miwili mmoja unasoma 1580000 na mwingine mdogo unasoma 30k,basi mzeebaba mechi zoooote zimeenda sawa,akabaki Sevilla nakumbuka alikuwa anacheza na Krasnodar,kwenye mkeka mkubwa Sevilla away x2 na mkeka mdogo Sevilla ashinde normal...basi unaambiwa hadi dk ya 78 Sevilla anaongoza goal 1,nikasema yes hii hela,nilimpa Sevilla kwa sababu kabla ya mechi hiyo alitoka kumpiga mtu 5-0,basi nimeshika mikeka yangu nabana mechi iishe hivyohivyo,dah dk ya 85 Krasnodar wakachomoa,nikasema si mbaya bado dk 5 muhindi leo hatoki nakula huu mkeka mkubwa,lahaula dk ya 90+3 Krasnodar anaongeza goal la pili,unaambiwa Sevilla kakaa 2-1 dadeeeki,siku ile niliapa mimi betting no mwanzo na mwisho leo huyu kanjibai atakuwa na majini


Yaani hadi ushinde bet,siku hiyo muhindi umembana haswaaa yani hana namna
 
Duuh!! Mkuu mi sina neno
 
Mi leo naapa sitabeti tena hii laki moja yangu ningempa mama yangu tu.


Pumbavu kanjibai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…