Pre GE2025 No refom No election inawapelekesha sana CCM, Makalla anadai CHADEMA imeanza kushindwa kabla ya uchaguzi mkuu

Pre GE2025 No refom No election inawapelekesha sana CCM, Makalla anadai CHADEMA imeanza kushindwa kabla ya uchaguzi mkuu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayehusika na Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, amewataka Watanzania kupuuza madai ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwamba uchaguzi hautafanyika bila mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Akizungumza siku ya Jumanne Machi 4, 2025 katika kikao cha viongozi wa CCM wa mashina, kata, matawi na mabalozi wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Makalla amesema kuwa CHADEMA inakosea kuwaambia wafuasi wao wasijiandikishe kwa madai kuwa hakutakuwa na uchaguzi.

"CHADEMA wameshawaambia wafuasi wao wasijiandikishe kwa sababu hakutakuwa na uchaguzi, kwa hiyo wameanza kushindwa kabla. Wanajiongezea matatizo kwa kukosa wanachama wao kujiandikisha. Nilimsikia Tundu Lissu akisema ‘Ujiandikishe iweje? So what?’ Nikasema shughuli imeisha hapa, hawa wameshakubali kushindwa," amesema Makalla.

Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025



Ameendelea kusisitiza kuwa uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa sheria na katiba, na kwamba madai ya CHADEMA kwamba "No Reform, No Election" ni propaganda zisizo na msingi.
1741087372817.png

"Reform zimeshafanyika na uchaguzi utafanyika. Ninataka niseme ukweli, puuzeni propaganda kwamba eti ‘No Reform, No Election’. Uchaguzi upo. CHADEMA hawana mamlaka wala uwezo wa kuzuia uchaguzi, wanapoteza muda wao na wa Watanzania. Uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria na katiba, na hakuna chama chochote kinachoweza kuuzuia," amesisitiza Makalla.

Kauli yake inakuja huku mijadala ikiendelea kuhusu mustakabali wa uchaguzi na msimamo wa vyama vya siasa juu ya mazingira ya kisiasa nchini Tanzania.

Source: Jambo TV
 
Vyama vya upinzani tz nona wanacheza ngoma ambayo hata midundo yake hawaijui
 
CPA makala hajamuelewa TAL juu ya no reforms no election???
Ndo mana Ccm wakawalipa wahariri njaa kina mawala na balile juzi ili wakawazodoe kina LISU NA WENZIWE???
 
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayehusika na Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, amewataka Watanzania kupuuza madai ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwamba uchaguzi hautafanyika bila mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Akizungumza siku ya Jumanne Machi 4, 2025 katika kikao cha viongozi wa CCM wa mashina, kata, matawi na mabalozi wa Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Makalla amesema kuwa CHADEMA inakosea kuwaambia wafuasi wao wasijiandikishe kwa madai kuwa hakutakuwa na uchaguzi.

"CHADEMA wameshawaambia wafuasi wao wasijiandikishe kwa sababu hakutakuwa na uchaguzi, kwa hiyo wameanza kushindwa kabla. Wanajiongezea matatizo kwa kukosa wanachama wao kujiandikisha. Nilimsikia Tundu Lissu akisema ‘Ujiandikishe iweje? So what?’ Nikasema shughuli imeisha hapa, hawa wameshakubali kushindwa," amesema Makalla.

Ameendelea kusisitiza kuwa uchaguzi utafanyika kwa mujibu wa sheria na katiba, na kwamba madai ya CHADEMA kwamba "No Reform, No Election" ni propaganda zisizo na msingi.
View attachment 3258490
"Reform zimeshafanyika na uchaguzi utafanyika. Ninataka niseme ukweli, puuzeni propaganda kwamba eti ‘No Reform, No Election’. Uchaguzi upo. CHADEMA hawana mamlaka wala uwezo wa kuzuia uchaguzi, wanapoteza muda wao na wa Watanzania. Uchaguzi upo kwa mujibu wa sheria na katiba, na hakuna chama chochote kinachoweza kuuzuia," amesisitiza Makalla.

Kauli yake inakuja huku mijadala ikiendelea kuhusu mustakabali wa uchaguzi na msimamo wa vyama vya siasa juu ya mazingira ya kisiasa nchini Tanzania.

Source: Jambo TV

Sidhani kama uhalisia upo hivi.

Ni kweli kabisa kwamba hakuna uwezekano wa kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu Mwaka huu wa 2025.
Aidha, ni kweli kabisa kwamba Hoja za Watu wa CHADEMA ni za kweli, pia ni za msingi. Hoja zao zina mashiko kuhusiana na Kukosekana kwa Mamlaka zinazoaminika kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi ulio huru, wa HAKI na ulio wa Wazi.

Jambo muhimu zaidi la kuzingatiwa ni kwamba: KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA MIFUMO YA UCHAGUZI. NA KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA KATIBA YA NCHI.

KAMWE HAUPO KABISA UWEZEKANO WA KUBADILISHA KATIBA YA NCHI KWA NJIA ZA KIDEMOKRASIA. HAUPO UWEZEKANO!

Kwa bahati mbaya sana, huu ndio Ukweli mchungu Sana kupita kiasi!
 
Kwani kuna shida gani kuteleleza madai ya Chadema?
 
Ushindi mwingine unakuwa hata haunogi.. Manake unakuwa sawa unapigana na mfu. Halafu unasema nimeshinda.

Yaani Hainogii... Na nafsi inakusuta... Halafu Ramadhani mtu anafunga!!!

Ngoja tusubiri maigizo... Ila za mwizi ni 40...
 
Baada ya uchaguzi wakisusia wajue hawana ruzuku inayotakana na kura za uchaguzi.

Sasa sijui hiko chama kitaendeshwa na hela gani.

Nasubiria plan B ya jinsi watavyoendesha chama baada ya uchaguzi, sitoshangaa wakienda kupiga magoti kwa mwamba awabebe.

Udhani kama Lissu ni mtu anaefikiria vitu kwa kina kabla ya maamuzi yake.
 
Back
Top Bottom