'No, we can't ' - is that what our 'Modern' Economists are advising?


Mchango wetu sisi Miafrika kwa kiasi kikubwa sana ni kazi za kutumia miguvu. Tokea utumwani hadi kwenye ukoloni.

Na kama tungekuwa wataalam hivyo basi tungewastukia wazungu tokea mwanzo na kuwapiga chini. Tungewageuzia kibao.

Na hivyo so called vyuo vya Timbuktu na Alexandria leo hii vinafanya nini? Maana mara ya mwisho kuona Timbuktu kwenye Tivii niliona kuwa ni sehemu iliyochoka sana. Hakuna lolote huko. Ni jangwa, mivumbi, mchanga, na jua kali tu. Nenda Oxford uone jinsi palivyo....
 
Mimi naona tatizo kubwa miongoni mwetu ni kutotaka kufuata ushauri wa watalaamu ambao tumewaajiri kufanya hizo kazi. Tunaamua kutokana na political wishes zetu at that particular time.

Nani miongoni mwetu anafuata ushauri wa mtaalamu kwa mfano dokta anasema tuachane na ngono ni chanzo cha HIV wanaofuata na kusikia ni wachache sana.

Usinywe bia, wangapi wanafuata ushauri huo?

Usifanye kazi sana kwani unajistress, wangapi wananfuata?

Ukiendesha high speed likelyhood ya accident ni kubwa?

Those examples are at personal level and they may go up to national level katika scenario nyingine nyingi tu.

inabidi tuheshimu watalaamu wetu kwani wanajua kwa nini wanasema hivyo.
 
Wachumi wengi sana wanaweza kuwa na mawazo mazuri sana, Lakini ukiwa Mchumi na pia ukawa unaona mambo kama haya kwa Taifa letu unaweza kukasirika kabisa na kuona kuwa tumelalia sana mawazo ya kimagharibi zaidi kuliko sisi wenyewe ndani zaidi. Kuna watu wanasema kuwa kuwa na Chuo kinatoa wachumi bora na kuona Taifa letu linapiga hatua kubwa ya maendeleo halisi
 
Hawa wasomi wana vyuo vyetu bwana ni wazuri ila naona wana dance kwenye tune ya wanasiasa. Nao wanaangalia maslahi zaidi mara nyigi kuliko usomi wao unataka nini? Kuna panel zozote za wachumi waliobobeaambao wanajaribu kuyasoma yanayoendelea na kutoa mchango wao hata kama hausikilizwi kuliko kuwa watazamaji 100%?
 
Wote nao wanakuwa kama wanasiasa na ndio shida moja kubwa sana katika Taifa letu
 

Kweli kabisa Kishoka wala hatuhitaji hao wa ma pi hechi dii, kujua kwamba commercial farming na kilimo kwanza ni ndoto za alinacha kama hakuna barabara za kwenda huko kwenye mahekari na mahekari ya ardhi na kama hakuna viwanda vya kusindika vyakula au kuprocess mazao ya biashara yatakayovunwa kuko mashambani

vitu vingine hata mwenye dumbness ya uchumi kama mimi anaweza kufikiria tu...
 

Hii kauli haikupaswa kutolewa na wachumi kwa kweli. Yaani Tanzania haina vichwa vya kufanya hili la uchumi? Ndiyo maana tunao wachina hata wauza mkaa na nyanya sasa. Inaudhi na kushangaza hili taifa linakoelekea.

Kwa jinsi baadhi yetu walivyokithiri kwa uvivu, kuna wakati watasema tupate rais Mchina na Mhindi pale Ikulu ili watukuzie uchumi wetu. Hivi sisi tutaweza kufanya kitu gani hasa duniani?
 
Ushaanza tena kuuongopea umma wa 'economics dummy', hivo hizo zinazoongelia 'new agenda' na 'new direction' unataka kusema hazina proposed theoretical models for economic development?

Soma titles za huyo jamaa. Hajaandika kitu chochote ambacho kinaweza kuwa na manufaa China, India, USA au Brazil. Titles zote ni narratives ya vile vilivyotokea.
 
Labda wame macoservative sana katika masuala nyeti ya taifa letu
 
Researches zote alizoandika huyo jamaa yako zinahusu Africa au Tanzania. Na zote ziko kwenye applications na hakuna hata moja theoretical.

Integrity 0, imagination 0.

Huyu si ndiye aliyekuwa chini ya Balali wakati watu wana EPA BOT? Sasa m-resume mkubwa wote huo alishindwa nini kuokoa mabilioni?
 
Integrity 0, imagination 0.

Huyu si ndiye aliyekuwa chini ya Balali wakati watu wana EPA BOT? Sasa m-resume mkubwa wote huo alishindwa nini kuokoa mabilioni?

Kwani li resume likubwa ndio nini? I guess labda linawa impress watu kama Companero
 
I blame the fact that,as a country,we do not have economic policies.In the traditional sense of the word i.e.

It is not any one economist's fault that none of our ''economic dreams'' are put into practice nor that those in charge keep playing hide and seek whenever issues on policy implementation are brought on the table.

Chinese and Indian economic advisers can only do so much as far as helping our economy is concerned.We still got to get our hands dirty...one thing we absolutely hate.
 
Last edited:
Integrity 0, imagination 0.

Huyu si ndiye aliyekuwa chini ya Balali wakati watu wana EPA BOT? Sasa m-resume mkubwa wote huo alishindwa nini kuokoa mabilioni?

Hahusiki kabisa na ufisadi. Huyo aliletwa kusafisha uozo uliokuwepo. Hiyo ndiyo kazi aliyoanza kuitekeleza siku za mwisho za Balali BOT. Hilo ndilo bado analitekeleza. Hana hatia huyu ndio maana jina lake bado ni safi.

Huyu kosa lake kubwa ni moja tu: Kutuletea taasisi na sera mufilisi za Uliberali Mamboleo!
 
Tatizo la Tanzania sio PhD older wa Economics, tatizo la Tanzania ni kwamba majority ya wachumi wetu wana abudu theory za kishenzi za wachumi kutoka World Banka and IMF. Wao wenyewe hawana imani na vitu wanavyo vielewa.

Nilisha andika mara mmoja kwamba kama ningekuwa nauwezo wa kuvett wachumi wa nchi, basi nisinge thubutu hata siku mmoja kuweka mtu yoyote aliyewai kufanya kazi Bank ya Dunia (WB). This includes Ben Ndulu.

Naongea haya sababu nina taaluma katika sector hii, soma vitabu vyote vilivyo andikwa na wachumi wa World Bank utakubali kwamba wao wanaimani na kitu kimoja "One Fits all Mentallity".

Kingine ni uvivu wa kufanya research ambao wanao MaPhD older wa Tanzania, wao wanacho jali ni pesa kutoka kwenye IFI wazitumie kisha wacopy na kupaste data za mwaka 50. That is the reason why IMF wataendelea kuleta wachumi wao ambao wameshaambiwa kabisa kwamba there is no medicine for Africa problem.

Soma vitabu vifuatavyo . The Confession of Economic Hit". The bottom billion, The white Man Burden, kisha som a wapuuzi kama hawa " The end of Poverty (architector wa MGD's), Macroeconomics in the Global Economy. Utakubaliana na mimi kwamba Umasikini wa Africa ni big business in the west. Na hakuna atakae kubali hizi nchi ziwe tajiri..... kwani ni political and economic threat on the west.
 


thanks you Mtanganyika for this useful post
 
I am sorry to say this is one of the most self demeaning statements of these modern times.
How can one think of HIS developments in terms of the Chinese and Indians?
The Proffessor is deranged and should have his head checked.
What will the Chinese or Indians tell youu that is not common knowledge?
Mkapa said wengi tuna uvivu wa kufikiri, mimi naongeza uvivu wa kiutendaji na kutegemea rushwa kama njia ya kipato.
 
We need to turn those Phd holders's mindset. They should lead the way like what Prof Mohamad Yunus of Baghladesh did. He initiated something unique without being told by politicians or bankers.
Phd za kusoma tu ili kupuata Kazi TRA na world bank wakati mfumo wa uchumi wetu wala haueleweki hakutusaiidi. Na hili sio suala la wana siasa. Ni la wachumi kutoa proposal zao na kuwashauri wana siasa. The problem I see is that almost all professions in Tanzania have delegated or surrendered professionalism to politics. Politics comes first then the other follows.
 

Mtanganyika:

Mfano wako ni sawa na kukataa mechanics wa Tanzania kwa sababu wanachojua ni ku-repair gari za kigeni. Na kuelekeza juhudi katika kutafuta engineers ambao watatengeneza magari kwa kutumia principles za kitanzania. Chances are you would find none.

Kama hutaki wachumi waliofanya kazi WB and IMF kwa sababu wana-influence kutoka katika benki hizo, basi hata hao ambao hawajawahi kufanya kazi kwenye taasisi hizo wanatumia principal zilezile.

Na kwa mtaji huu itabidi uchague wataalamu ambao wanakataa modern principles of economy. Na kwa bahati mbaya watu hao hawapo. Hivyo utaishia kuchagua asiyejua kitu chochote.

Kuna posti kibao humu ndani zinazomsifia Paul Kagame. The truth is the bulk of expertise ambayo Kagame anaitumia ni hile hile ambayo ilikuwa imelala katika nchi zingine za kiAfrika.

PUT YOUR MONEY WHERE YOUR MOUTH IS.
 

Originality katika levels nyingi za wasomi wetu ni kitu ambacho kipo short in supply.

Sasa hivi nchi nyingi za Latin America zina bankers na wachumi wazuri. Wengi wao walisoma katika vyuo vya Marekani na kufanya kazi katika World bank na IMF kupata exposure na baadaye wamerudi makwao.

Tatizo la waAfrika wakipata kazi kwenye mashirika makubwa, wanachukua kama permanent positions.

Balali, Ndullu, Idrisa walikwenda World bank kufanya kazi hili wapate kipato kikubwa na sio exposure ambayo ingewafanya warudi nyumbani na kuleta mabadiliko.

Kwanini mtanzania afanye kazi world bank miaka 20? Miaka mitano nadhani inatosha na kuwapisha wengine. Na ndio maana kila mtu akipata posti ya kwenye mashirika ya kimataifa, wenzake wanampongeza kuwa ameula.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…