Noah Saputu asisitiza usawa ajira za TAMISEMI

Noah Saputu asisitiza usawa ajira za TAMISEMI

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

NOAH SAPUTU MOLLEL - ASISITIZA USAWA KATIKA AJIRA ZINAZOTANGAZWA TAMISEMI

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Mhe. Noah Lemburis Saputu Mollel wakati akichangia bungeni katika vikao vinavyoendelea amesisitiza pawepo na usawa katika kugawa ajira pia ameiomba Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuwa barabara za Arumeru zitengenezwe.

"Barabara ya Loning'o kwenda Mringa imekatika daraja, Barabara kutoka mnadani kwenda hospitali ya Oturumenti imekatika, naiomba sana wizara kupitia waziri wetu aone namna gani tunapata fedha za dharura, kwa ajili ya kuhakikisha maeneo haya yaliyokatika yanaweza kutengenezwa mara moja"Noah Lemburis Saputu Mollel -Mbunge wa Arumeru Magharibi.

"Nina meseji zaidi ya 200 mpaka 300 vijana wanasema tutafutieni ajira, kwa hiyo niombe basi ajira hzi zigawanywe kwa mikoa, na baadae kwenye mikoa igawanywe kwenye Wilaya ili tuweze kupata usawa katika kupata ajira hizi"Noah Lemburis Saputu Mollel -Mbunge wa Arumeru Magharibi.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-04-20 at 16.49.13.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-20 at 16.49.13.jpeg
    36.3 KB · Views: 11
  • WhatsApp Image 2023-04-20 at 16.49.14(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-20 at 16.49.14(1).jpeg
    32 KB · Views: 12
Back
Top Bottom