Noti ya shilingi mia tano kubadilishwa kuwa sarafu

naona tumeamua kuwaiga wenzetu jirani wa mu7 kuwa na 500 ya coin soon kadiri uchumi unavyo drop tutawaiga kuwa na noti ya 50,000/=

Sioni km sarafu au noti ni kipimo halisi cha uchumi kwan uchumi wa tz na wa Uganda upi uko juu?
 
tushare kwa pamoja!
KWA TREND HII YA BOT; UCHUMI WA TANZANIA ULALE MAHALI PEMA PEPONI.!

Siungi mkono hoja ya Benki kuu (BOT) kufuta noti ya Sh.500/= na kuifanya sarafu. Huu ni wendawazimu mkubwa katika sekta ya uchumi "the most unpleasant economic decision" kwa sababu zifuatazo;

MOSI; fedha yoyote inapobadilishwa kuwa sarafu kutoka shillingi ni kuishusha thamani. Hii ni kwa sababu kiuchumi inabadilika matumizi na kuanza kutumika zaidi ktk sekta ya uchumi mdogo km wa wauza njugu mtaani, mama lishe, na maeneo mengine yasiyozalisha sana kiuchumi (less productive sector).

Maeneo yenye uzalishaji mkubwa (lead productive sector) yatashindwa kuitumia fedha hii kwa kuwa tu ni ya sarafu. Kw mfano kuanzia sasa haitakua rahisi kukuta sarafu hizi za 500/= maeneo kama Airport, Migodini au Supermarket.

Hiki ni kiashiria cha kushuka kwa thamani kwa fedha hiyo. (Indicator for currency devaluation).

Hivi hatujiulizi kwanini Marekani hadi dollar moja ni ya noti sisi 500/= tunaweka sarafu?? Dollar moja ina single digit lakini ipo kwenye noti, sisi tunalazimisha kuweka 500 kwny sarafu wakati ina tripple digit. Tunaforce Galloping inflation.

PILI; unapotengeneza sarafu ya pesa kubwa ina maana sarafu zinapotea na kujiondoa ktk mzunguko wa fedha. So tutegemee siku si nyingi sarafu za sh.100/= na sh 200/= hazitakuwepo tena mtaani.

Ikifikia hatua hii ujue nchi imeanza kuyumba kiuchumi na mfumko wa bei umevuka kiwango cha kawaida (extention from Moderate inflation to Galloping inflation).

Wenzetu Kenya hadi sarafu ya sh.10 inatumika. Ukienda Nairobi, Mombasa au maeneo mengine ya Kenya utata watoto wakinunua madafu, ice cream au matunda kwa sh.10.

Hapa kwetu sarafu ya sh.10 ilikufa na Nyerere. Ya sh.5 ikaenda na Sokoine. Ya sh.20 na 50 zimemfuata Kawawa. Sasa benki kuu wanalazimisha sarafu ya sh.100 na ya sh.200 zikamfuate Karume mahali pema peponi. Noti ya sh.1,000/= nayo inakaribia kwenda ahera maana BOT wameleta sarafu ya sh.1,500/=.

TATU; BOT kuwa wametoa hoja mufilisi kuwa wamefuta noti ya Sh.500/= na kuireplace kwa sarafu baada ya kugundua noti hiyo inachakaa haraka sn na inadumu kwa muda mfupi mno kwenye mzunguko.

Hoja hii ni mufilisi kwa sababu solution ya noti kuchakaa mapema si kureplace sarafu bali ni kuimarisha noti hiyo kwa kuitengeneza kwa material imara zaidi.

Hivi noti ya 10,000/= nayo ikichakaa mapema BOT wataleta sarafu instead?? Huu ni wendawazimu.

Mojawapo ya sifa za fedha imara ni uwezo wa kukaa kwny mzunguko muda mrefu (durability). Sasa fedha inapopoteza durability dawa sio kubadili muundo wake (changing of currency format is not a solution for impermanency)

Lakini hata hivyo BOT wameonesha hawakufanya utafiti wa kina kabla ya kuleta sarafu ya 500/=. Wanasema zinachakaa haraka ukilinganisha na noti nyingine. Hii ni hoja dhaifu sana kutolewa na mtu anayejiita Profesa wa uchumi Benno Ndullu.

Yani Profesa Ndulu anataka noti ya 500/= na ya 10,000/= zidumu kwenye mzunguko kwa muda sawa?? Yani 10,000/= ikidumu miaka miwili, 500/= nayo idumu miaka miwili. Bila shaka hapo ndo ataona noti ya 500/= haichakai haraka.

Hii ni "akili ndogo kujaribu kutawala akili kubwa". Noti ya 500 haiwezi kulinganishwa na noti nyingine kwenye mzunguko kwa sababu ina frequent circulation. Yani ktk uchumi noti yenye thamani ndogo huwa inazunguka zaidi kuliko ya thamani kubwa.

Hivyo noti ya 500/= inaweza kupita kwenye mikono ya watu 2000 ndani ya mwezi mmoja wakati ile ya 10,000/= imepita kwenye mikono 20 tu kwa mwezi.

Hii ni kwa sababu mzunguko wa noti hizi hutegemea matumizi. Ya 500/= itazunguka kwny daladala, wauza magazeti, vijiwe vya kahawa etc, wakati ile ya 10,000/= itazunguka Supermarket, Airport, hoteli kubwakubwa etc.

Hivyo ni dhahiri kuwa noti ya 500/= itaanza kuchakaa mapema kuliko noti ya 10,000/= au ya 5,000/= au noti nyingine kubwa. Sasa cha ajabu Profesa Beno Ndulu hajui hili na badala yake ameona solution ni kuleta sarafu. Aibu gani hii kwa mtu anayejiita Profesa wa uchumi kushindwa kujua vitu common km hivi ambavyo hata muuza machungwa wa Keko anavijua.

Kumbukeni noti za sh. 10 20 50 100 zilivyoondoka na Sarafu zake kushindwa kukaa kwenye kiwango cha matumizi.
 
Watanzania wa kipato cha chini si watunzaji wa noti, hivyo wacha waletewe sarafu.
 
Kuna mahali nilitoa comment kuwa Prof.Ndulu ameonyesha udhaifu na pia kutia aibu.

Hivi mtoto wa First Year pale UDSM anayesoma basic Theories za Economics akisoma Money Circulation angeshindwa kufanya maamuzi bora kuliko haya ya Prof?
 
"less productive sector"? - unamaanisha "ajira zisizo rasmi"?
 

Japokuwa nimezaliwa na kulelewa katika CCM,lakini mfumo wa siasa na uongozi unaendelea nchini mwangu haunipi imani na matumaini ya kuona kuna uthabiti katika kumsaidia Mtanzania masikini katika nyanja zote. Inasikitisha kuona katika nchi zilizoendelea wanatumia mpaka CENTS, lakini zaidi mafungu ya noti kuanzia 5-7 nahizi wametumia miaka nenda rudi mfano;

US$ noti $1,$2,$5,$10,$20,$50,$100 nkcoins mpaka cents
NZ$ no $5,$10,$20,$50,$100 lakini coins mpaka cents 10
 
Ukiona nchi inakushinda waaminishe watu kuna udini na ukabila nchini mwako.
 
Tulipo sarafu za sh. 5, 10, 20, 50 hazinunui kitu sasa ujio wa 500 ni kuimaliza 100
 
Watanzania wa kipato cha chini si watunzaji wa noti, hivyo wacha waletewe sarafu.

Mkuu tatizo sio utunzaji wa noti ;tatizo ni quality ya material waliyotengenezea hizi noti mpya wakati Ndullu ameukwaa ugavana, mbona zile noti kabla ya hizi zilikuwa na ubora wa hali ya juu!! Kumbuka kuwa wananchi walilalamikia ubora wa hizi noti mara tu zilipotoka lakini huyo professa akasema eti hizo ndio security features zitakazozuia watu kutengeneza noti[ counterfetting]!!! Pale hakuna gavana kuna boya tu.
 
Wadau mnieleweshe, kuna tofauti kati ya sarafu na shilingi?
 
Tulipo sarafu za sh. 5, 10, 20, 50 hazinunui kitu sasa ujio wa 500 ni kuimaliza 100
Kwa nini 100 imalizwe wakati ilipoanzishwa ya shilingi 200 mlisema kuwa 50 itapotea lakini bado inaendelea kutumika?
 
Hatuna gavana pale BOT.

Kuondoa noti ya sh 500 na kuweka sarafu ni kushusha thamani ya hela yetu. Mimi nilitegemea wataalamu wetu huko BOT wangetilia maanani maneno ya Mkapa kwamba anataka mpaka sarafu ya shilingi moja iwe na matumizi.

Nasikia sasa kuna mpango wa kutengeneza noti ya sh elfu 50; na laki moja. Mungu tuepushe na utawala wa hawa mashetani wa ccm. Hawaitakii mema nchi hii.
 
Sarafu ndiyo fedha. Noti siyo fedha ni legal tender. Ndiyo maana inaandikwa "fedha halali kwa malipo ya shillingi......"
Kwenye sarafu imeandikwa shillingi..... lakini noti inaandikwa " fedha halali kwa malipo ya shillingi....
In banking Law there is a difference between money and legal tender. Hope you get me!
 
Kwa nini 100 imalizwe wakati ilipoanzishwa ya shilingi 200 mlisema kuwa 50 itapotea lakini bado inaendelea kutumika?

Kijana
Hiyo sarafu ya sh 50 inapotea taratibu. Hata bei za vitu vidogovidogo sasa hivi ni mwendo wa mia na zaidi. Ni nadra kukuta kitu kinauzwa, kwa mfano sh 650; au 2450.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…