NSSF & PPF Tujengeeni nyumba sisi wanachama wenu

ELNIN0

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2009
Posts
4,161
Reaction score
1,476
Wakuu,

Nimetoka NSSF kuchukua kadi mpya sasa hivi pia nikapata kucheki salio langu, yaani wakinipa hizo pesa leo nina uhakika wa kuwa na nyumba ya kisasa.

Ombi langu kwa mifuko hii wangebuni miradi ili watuwezeshe na sisi wanachama wao tunufaike kwa mfano ujenzi wa nyumba za kisasa na kutukopesha sisi wanachama wake kwa riba nafuu wakitumia masalio yetu kama dhamana ya mikopo.

Kama hawatoi mikopo hata mi naona hakuna haja ya mamilion yangu wakae nayo wakati mi nahangaika kukopa benki wa riba kubwa, na hii ndiyo inachangia watu wakibadili mwajiri wanazivuta pesa sababu hakuna faida unapata zikiwa huko.

Kama kuna mtu humu anafanya katika mifuko hii ya jamii atupe ufafanuzi zaidi hasa hili la kuwekeza kwenye nyumba na kuwakopesha wanachama wake.
 
Majimbo, kama mwanachama ana akiba yake tuseme inazidi 20m kwa nini asitumie dhamana hii kukopeshwa vitu vya msingi kama nyumba, elimu? kwa nini wao wanatumia pesa zetu kuwekeza kwenye majengo na kuyakodisha ki biashara ali hali wanachama wanabakia wamechokaa chakari.

Hizi benefits na riba wanazitoa ni ndogo sana ambazo haziwezi kumtoa mwanachama from point A to B.
 

watakujengea vipi hiyo nyumba wakati kulipa ela yenyewe kasheshe wakati hiyo ni ela yako sio yao uliwaazima mtaji wakazungushie .mimi nawadai ela nssf mpaka sasa urasimu mtupu sijalipwa ela yangu na muda wa miezi sita(toka nimeacha kazi) umeshapita wa kuchukua!! na sijui wanalipa ileile wanayokukata au wanalipa na riba, mwenye kujua anieleweshe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…