Nssf westadi, swift freight na ubabaishaji nje ya nchi!

Nssf westadi, swift freight na ubabaishaji nje ya nchi!

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Siku ya jumamosi tarehe 7/12/13 kuliandaliwa mkutano au tafrija au hafla maalum ya kuwakutanisha watanzania waishio sehemu mbalimbali nchini Uingereza. Mkutano huo ulidaiwa kuyatarishwa na kampuni ya usafirishaji mizigo iendayo nchini Tanzaia iitwayo Swift Freights UK Ltd ambayo inadhaniwa inamilikwa na mtanzania aitwae Abdul Faraj.

Mkutano huo ulikuwa unatarajiwa kuwakutanisha wawakilishi wa shirika la hifadhi ya jamii la NSSF ambao walikuwa wanakuja kuuza ushauri kuhusu mpango maalum uitwao WESTADI ambao unawahusu watanzania waishio nje ya nchi.

Mpango huo unatoa fursa kwa kila mtanzania kuweza kuchangia kwenye mfuko huo dola za marekani karibu 300 kila mwaka fedha ambazo zingesaidia katika nyakati za maafa kama kifo ambapo mwili wa marehemu unaweza kusafirishwa hadi nyumbani kwa gharama za kutoka katika mfuko huo pamoja na msindikizaji.

Pia kila mwanachama wa kutoka nje akiwa nyumbani Tanzania anaweza kupata huduma ya matibabu bure pamoja na watu wa karibu wanne ambao wapo nyumbani nchini Tanzania ambao wangeweza kusaidiwa kupata huduma za matibabu ya bure endapo wangehitaji huduma hiyo.

Pia shughuli hiyo ingeambatana na sherehe za kuadhimisha miaka 52 ya uhuru, ambayo kilele chake ni Jumatatu, tarehe 9 December mwaka huu.

Kwa mujibu wa matangazo yaliyobandikwa katika tovuti za Ankal Issa Michuzi na ile ya dada yetu Jestina George, shughuli hiyo ingefanyiwa katika ukumbi maafuru wa shughuli wa La Royale Banquenting Suites uliopo White Hart Lane, Tottenham kuanzia saa 1 jioni hadi saa tisa asubuhi.

Ilidaiwa katika tangazo hilo kwamba kiingilio kingekuwa ni bure na kungekuwepo muziki ambao ungepigwa na mmoja wa ma DJ maarufu nchini UK bwana Chambi na pia kungekuwepo bendi ya wanamuziki ambao ni raia wa Congo ambao wana makazi yao sehemu hiyo ya kaskazini mwa jiji la London.

Jambo la kushangaza na la kutia aibu ni jinsi ubabaishaji uliojionyesha waziwazi kuhusu jambo zima na utaratibu mzima na namna jinsi sisi watanzania hasa tuishio nje tunavyoshindwa kuelimika katika masuala kama haya ya kufanya iwe hafla, sherehe au shughuli maalum.

Jambo la kwanza ni kutoonekana wa wawakilishi wa NFFS ambao ndio wageni maalum wa shughuli nzima kwamba ndio wangekuwa wasemaji wakuu na watoaji ushauri na ufafanuzi wa mpango mzima wa NSSF kwa sisi watanzania tuliotaka kupata maelezo.

Je kama wawakilishi wa NSSF walikuwepo London kwa shughuli hii, je waliishia wapi na waisonekane ukumbini na kama walikuwepo lakini wakaamua kuondoka je ni kwa sababu gani?

Je ni nani alipewa jukumu la kuandaa shughuli hii maalum na ni nani amelipia gharama zote za matayarisho ya shughuli hii? Pia je mheshimiwa balozi wetu bwana Kalaghe alifahamu juu ya ujio wa NSSF nchini UK na kwa kiwango gani ameshiriki kuhamasisha watanzania kuhudhuria shughuli hii kupitia tovuti ya ubalozi?

Nimemwingiza mheshimiwa balozi kwa kuzingatia kwamba shughuli hii iliambatana na kumbukumbu ya miaka 52 ya uhuru wa Tanzania hivyo kuipa uzito wa hali ya juu shughuli hii hivyo kungekuwepo na ugeni rasmi , ugeni wa NSSF WESTADI na wageni maalum kutoka, je kama anafahamu hii ni kwa kiwango (capacity) gani?

Nikija kwenye shughuli yenyewe haikuwa ya kufana sana kutokana na wageni hafifu ambao pia walichelewa sana kuingia kwenye shughuli yenyewe mpaka kuanzia mida ya saa tano usiku badala ya saa moja kamili ya usiku kama ilivyopangwa.

Jambo la muda linatusumbua sana watanzania wa UK ambao kulingana na maisha tunayoishi na wenyeji tumeona jinsi muda unavyopewa kipaumbele katika kila mazingira lakini kwa hili tumeshindwa sana. Ni shughuli, sherehe na tafrija nyingi sana watanzania wa UK wanachelewa tena hadi masaa manne kiasi cha kuwaambukiza hata wasanii wetu akina Diamond ambae alichelewa sana alipofanya onyesho lake la mwisho pale Kenning Town ambapo aliingia saa saba unusu za usiku.

Nikirudi kwa mtayarishaji bwana Faraji na wageni wake wa NSSF inasemwa kwamba wageni hawa hawakuwepo ukumbini na pengine hawakuhudhuria kabisa sherehe yenyewe. Sasa je ni sababu zipi zilizopelekea hali hii ukizingatia kwamba hakuna taarifa yoyote ya kuomba radhi na kufafanua kidogo hali yoyote iliyotkea hadi kusiwepo shughuli ya WESTADI na badala yake wananchi waendelee kununua vinywaji na nyama choma na kusakata rumba?

Nikiwa mmoja wa watanzania ambao tumeishi Ulaya kwa muda mrefu najisikia aibu sana pale sisi watanzania tunaposhindwa kuandaa hata kasherehe ka watu hamsini tu achilia mbali 100 kwani tunaonyesha waziwazi jinsi tulivyozoea maisha ya ujanjaujanja na ubabaishaji na kibaya zaidi pale tunapokuwa ni wasomi.

Kama mtanzania yoyote ambae yumo humu JF na alihudhuria shughuli hii maoni yenu yanakaribishwa kwa lengo la kujitambua tupo wapi na tunakwenda wapi.

Watanzania wenzetu wa USA je mpango wa WESTADI umewanufaisha vipi na vipi maandalizi yake yalifanywa na nani?, tafadhali tujadiliane bila jazba.
 
Nikiwa mmoja wa watanzania ambao tumeishi Ulaya kwa muda mrefu najisikia aibu sana pale sisi watanzania tunaposhindwa kuandaa hata kasherehe ka watu hamsini tu achilia mbali 100 kwani tunaonyesha waziwazi jinsi tulivyozoea maisha ya ujanjaujanja na ubabaishaji na kibaya zaidi pale tunapokuwa ni wasomi.

Watanzania wenzetu wa USA je mpango wa WESTADI umewanufaisha vipi na vipi maandalizi yake yalifanywa na nani?, tafadhali tujadiliane bila jazba.

Mkuu, hiyo huduma ndo juzijuzi nimeisikia kwa rafiki yangu mmoja ambaye yuko Washington DC.
Sidhani kama ni huduma ya walanguzi, maana pia nilisoma habari zake katika tovuti ya NSSF. Cha msingi hapo ni kwamba, wa kushikwa shati ni yule aliyewaita, yule aliyewatangazia kuwa kuna shughuli, na wala si NSSF. Yawezekana kuna mtu alitaka tu kujinifaisha hapo.

Lazima ujue kuwa mtoto wa mamba ni mamba. Wengi wa Wabongo walioko nchi za nje ni wale ambao wazee wao wana uwezo kifedha, yaani ni wale ambao ndo mafisadi na wafanya biashara haramu huko nyumbani kwetu. Sasa wao kama wametoka kwenye hizo familia za walanguzi na mafisadi, na wao wanatafuta ujanja huo huo kwa ajili ya kujinufaisha. Kampuni ya usafirishaji si ndiyo ya akina Chris Lukosi kweli?
 
Mkuu, hiyo huduma ndo juzijuzi nimeisikia kwa rafiki yangu mmoja ambaye yuko Washington DC.
Sidhani kama ni huduma ya walanguzi, maana pia nilisoma habari zake katika tovuti ya NSSF. Cha msingi hapo ni kwamba, wa kushikwa shati ni yule aliyewaita, yule aliyewatangazia kuwa kuna shughuli, na wala si NSSF. Yawezekana kuna mtu alitaka tu kujinifaisha hapo.

Lazima ujue kuwa mtoto wa mamba ni mamba. Wengi wa Wabongo walioko nchi za nje ni wale ambao wazee wao wana uwezo kifedha, yaani ni wale ambao ndo mafisadi na wafanya biashara haramu huko nyumbani kwetu. Sasa wao kama wametoka kwenye hizo familia za walanguzi na mafisadi, na wao wanatafuta ujanja huo huo kwa ajili ya kujinufaisha. Kampuni ya usafirishaji si ndiyo ya akina Chris Lukosi kweli?

Inawezekanaje NSSF wakakubali huu ujanja maana lazima wawe na mtu anaeangalia mitandaoni kuona kama kuna ujanja unafanyika kutumia jina lao.

Naungana nawe kabisa kuhusu familia za mafisaji lakini kwanini?

Mwisho nafikiri hii Swift Freight UK Ltd ipo chini ya Faraji na Chris Lukosi ni bosi wa Serengeti Greight Forwarders.
 
Inawezekanaje NSSF wakakubali huu ujanja maana lazima wawe na mtu anaeangalia mitandaoni kuona kama kuna ujanja unafanyika kutumia jina lao.

Naungana nawe kabisa kuhusu familia za mafisaji lakini kwanini?

Mwisho nafikiri hii Swift Freight UK Ltd ipo chini ya Faraji na Chris Lukosi ni bosi wa Serengeti Greight Forwarders.

Asante kwa kunisahihisha, mkurugenzi. Nilidhani huyu Lukosi anahusika maana naona vipachiko vyake vingi ni vya kusifia ufisadi na mafisadi.
 
magoma motomoto.jpgNdugu zangu watanzania wakati umefika kuanza kuthamini vitu vizuri vinavyofanyika katika jamii yetu ughaibuni.


Huyu bwana Faraji amekuwa akiandaa hizi shughuli kwa muda mrefu hapa Uingereza anachokipata kwa kuandaa hizi shughuli anakijua yeye.


Safari hii kwa upande wa burudani vyote vilikuwepo kama tulivyoambiwa yaani ukumbi La Royale, kiingilio BURE, bendi ya Kahwele, ma-dj seti mbili ya Andrew/Chambi na Double T toka Luton. Chezea Swift Freights wewe?

watu kibao.jpg
Jamani mie binafsi na wenzangu tuliokuwa nao tuliburudika mno tukiamini hatimaye Independence Party London imefufuka. Tena nikakutana na vijeba vyenzangu vya UK ambao hatujakutana mamiaka.

wageni.jpg
Hayo mambo ya Westadi tukaambiwa yameahirishwa hadi mwakani. Faraji andaa tena na safari hii itabidi ukumbi utanuliwe manake mambo yale si ya kitoto.


Lakini kawaida tu sie Waswahili hata tuwe Oxford Circus ni hatuna jema. Kwa mliokosa poleni ila picha za kumwaga kwenye mablog ya Flora Bahati Lyimo ‘Mbuta Nanga@ na Jestina George.

umati uhuru Uk.jpg
 
View attachment 125873Ndugu zangu watanzania wakati umefika kuanza kuthamini vitu vizuri vinavyofanyika katika jamii yetu ughaibuni.


Huyu bwana Faraji amekuwa akiandaa hizi shughuli kwa muda mrefu hapa Uingereza anachokipata kwa kuandaa hizi shughuli anakijua yeye.


Safari hii kwa upande wa burudani vyote vilikuwepo kama tulivyoambiwa yaani ukumbi La Royale, kiingilio BURE, bendi ya Kahwele, ma-dj seti mbili ya Andrew/Chambi na Double T toka Luton. Chezea Swift Freights wewe?

View attachment 125875
Jamani mie binafsi na wenzangu tuliokuwa nao tuliburudika mno tukiamini hatimaye Independence Party London imefufuka. Tena nikakutana na vijeba vyenzangu vya UK ambao hatujakutana mamiaka.

View attachment 125874
Hayo mambo ya Westadi tukaambiwa yameahirishwa hadi mwakani. Faraji andaa tena na safari hii itabidi ukumbi utanuliwe manake mambo yale si ya kitoto.


Lakini kawaida tu sie Waswahili hata tuwe Oxford Circus ni hatuna jema. Kwa mliokosa poleni ila picha za kumwaga kwenye mablog ya Flora Bahati Lyimo ‘Mbuta Nanga@ na Jestina George.

View attachment 125872

Mkuu Mzenji nimekwishafahamu lakini bado hujajibu hoja yangu ya msingi, soma tena hoja yangu.
 
Kiongozi Richard, nadhani hoja zako za msingi ni mbili ubabaishaji watu kutumia jina na NSSF kwa faida zao lakini hapo juu nimesema kuwa tulitaarifiwa kuwa shughuli hiyo imeahirishwa na wengi wale ambao walikuwa wamejiandikisha kuhushuria walifahamisha kubadilika kwa sherehe toka uzinduzi wa westadi na kuwa sasa itakuwa sherehe ya muungano. Hivyo hapa hakuna suala la ubabaishaji tulipokea hii flyer iliyoambatanishwa hapa chini pamoja na maelezo.

Pili kama shighuli ya uzinduzi wa Westadi imeahirishwa hadi mwakani basi kulikuwa hakuna sababu ya msingi ya wahusika wa WESTADI kuhudhuria shughuli hii.

Ukitizama picha juu utaona shughuli ilifana vilivyo, kama taarifa wewe hazikufikia katika muda muafaka basi nadhani tuwashauri hawa waandaji siku za usoni waweze kuwekeza nguvu zaidi katika mawasiliano kwa sababu jambo lililofanywa lilikuwa ni la kuongeza tija katika jamii. Sasa NSSF watazindua hiyo WESTADI mwakani na kudhihirisha hamna ubabaishaji katika hili suala.
Swift Freights Uk - TZ Independece day.jpg
Hili hapa juu ndio tangazo tililotumia katika inbox baada ya kujiandikisha kuhudhuria, utaona kuwa halisemi chochote juu ya WESTADI au NSSF.
 
Kiongozi Richard, nadhani hoja zako za msingi ni mbili ubabaishaji watu kutumia jina na NSSF kwa faida zao lakini hapo juu nimesema kuwa tulitaarifiwa kuwa shughuli hiyo imeahirishwa na wengi wale ambao walikuwa wamejiandikisha kuhushuria walifahamisha kubadilika kwa sherehe toka uzinduzi wa westadi na kuwa sasa itakuwa sherehe ya muungano. Hivyo hapa hakuna suala la ubabaishaji tulipokea hii flyer iliyoambatanishwa hapa chini pamoja na maelezo.

Pili kama shighuli ya uzinduzi wa Westadi imeahirishwa hadi mwakani basi kulikuwa hakuna sababu ya msingi ya wahusika wa WESTADI kuhudhuria shughuli hii.

Ukitizama picha juu utaona shughuli ilifana vilivyo, kama taarifa wewe hazikufikia katika muda muafaka basi nadhani tuwashauri hawa waandaji siku za usoni waweze kuwekeza nguvu zaidi katika mawasiliano kwa sababu jambo lililofanywa lilikuwa ni la kuongeza tija katika jamii. Sasa NSSF watazindua hiyo WESTADI mwakani na kudhihirisha hamna ubabaishaji katika hili suala.
View attachment 125986
Hili hapa juu ndio tangazo tililotumia katika inbox baada ya kujiandikisha kuhudhuria, utaona kuwa halisemi chochote juu ya WESTADI au NSSF.

Sawa mkuu lakini hio picha uliyoweka hapa mbona umeichakachua na inaonyesha tarehe 11/12/13?

Haya ni mambo yaleyale ninayoyazungumzia.

Picha ya kwanza iliyowekwa kwenye blogs zote mbili nilizojitaja zilikuwa na kataswira ka NSSF WESTADI kikionyesha udhamini wao wa shughuli hii,na ilikaa chini kulia kwenye kona.

Sasa wewe mkuu unaleta picha uliyoifanyia editing tena tarehe 11/12/13

What is this my friend, what type of merchant are you?
 
Sawa kabisa Richard hilo unalozungumzia ni la kabla ya shughuli ya Westadi kuahirishwa , lakini baada ya kuahirishwa hilo tangazo hapo juu ndio lililowekwa. ukifuata string yetu hapo juu nadhani tupo pamoja kiongozi hamna uchakachuaji hayo mabadiliko yalifanywa baada ya WESTADI kuamua kuahirisha uzinduzi hadi mwakani. Hapo ndipo promota mwingine aliingilia kati na kuhakiki kuwa siku ya uhuru haipiti hivihivi.

Kwa mantiki hii nadhani ilibidi hawa waandaji wapongezwe na kushauriwa jinsi ya kuboresha ufanisi wa shughuli kama pana mapungufu uliyoyaona kwani hamna kati yetu aliyekamilika.

Tukiwa na mtizamo huu tutajenga lakini vinginevyo itakula kwa Tanzania, tujifunze kushirikiana na kupeana ushauri badala ya kutupiana lawama wakati lengo letu wote ni moja kuijenga nchi yetu na watu wake. Mataifa mengine huungana mkono katika nyakati za kitaifa kama hizi, kwa nini na sisi tusiwe hivyo.

Mungu ibariki Tanzania!!!
 
Nimekufahamu mkuu, tena sana tu.

Mimi ni muumini mkubwa sana wa masuala ya kuheshumu muda na mipangilio, kwahio inapoonekana kwamba kuna walakini takita shughuli mbalimbali za maana kama hizi tunazohudhuria na ambazo ni adimu ni lazima kutolewe kasoro.

Nafikiri pia wewe uliwahi kuhudhuria sherehe za Uhuru ambazo mheshimiwa balozi wa wakati ule bwana Charles Kibelo alihudhuruia pale Broad Water Farm na tukatumbuziwa na marehemu mzee Ndala Kasheba na King Kiki.

Nafikiri ile ilikuwa ni moja ya shughuli zilizowahi kufana sana hapa UK na ambazo kijana mwenzetu Abdul anaweza kujifunza na akaangalia masuala yote ya "events management".

Mimi Nampa support ya nguvu na hata wewe wote sisi ni dugu moja , tupo Ulaya lakini tujifunze kuheshimu shughuli , muda na mipangilio huo ndio unakuwa mtindo wa watu walioelimika, mambo ki-Ulaya Ulaya tu.

Au sio mkuu!

Lol
 
Nimekufahamu mkuu, tena sana tu.

Mimi ni muumini mkubwa sana wa masuala ya kuheshumu muda na mipangilio, kwahio inapoonekana kwamba kuna walakini takita shughuli mbalimbali za maana kama hizi tunazohudhuria na ambazo ni adimu ni lazima kutolewe kasoro.

Nafikiri pia wewe uliwahi kuhudhuria sherehe za Uhuru ambazo mheshimiwa balozi wa wakati ule bwana Charles Kibelo alihudhuruia pale Broad Water Farm na tukatumbuziwa na marehemu mzee Ndala Kasheba na King Kiki.

Nafikiri ile ilikuwa ni moja ya shughuli zilizowahi kufana sana hapa UK na ambazo kijana mwenzetu Abdul anaweza kujifunza na akaangalia masuala yote ya "events management".

Mimi Nampa support ya nguvu na hata wewe wote sisi ni dugu moja , tupo Ulaya lakini tujifunze kuheshimu shughuli , muda na mipangilio huo ndio unakuwa mtindo wa watu walioelimika, mambo ki-Ulaya Ulaya tu.

Au sio mkuu!

Lol

Nimekusoma Kiongozi, bahati mbaya kipindi hicho mimi bado nilikuwa sijatinga Uingerezani kipindi cha balozi Kibelloh, lakini nakubaliana na wewe mpangilio ni kitu muhimu sana katika shughuli na ndio maana nadhani ni muhimu hizi shughuli zinatakiwa ziongozwe na umoja wa Watanzania pamoja na ubalozi ili kuweka ufanisi zaidi na wewe pia naona ni mtu mahiri unayelewa mambo kwa nini usijribu kumpa huyu Abdul au Jumuiya ya Watanzania ushirikiano wako ili kuboresha mambo.

Mimi nadhani WaTZ lazima tupeane mashavu ili tufanye mambo makubwa na ya maendeleo lakini tukiendelea kupigana vita huku kwenye mitandao hao wanaokosolewa ni rahisi wakawa defensive na kusababisha malumbano badala ya kujadiliana jinsi ya kuungana na kurekebisha mambo kwa manufaa ya sisi wadau ambao hupendelea hizi shughuli ili tukutane na jamaa ambao hatujaonana miaka tele.

Cha msingi tunahitaji chombo chetu cha watanzania chenye nguvu ya watu ambacho wote tutakiunga mkono katika kuendesha masuala ya kijamii hapa Uingereza.

Pamoja tutafika kaka...!!!
 
Nimekusoma Kiongozi, bahati mbaya kipindi hicho mimi bado nilikuwa sijatinga Uingerezani kipindi cha balozi Kibelloh, lakini nakubaliana na wewe mpangilio ni kitu muhimu sana katika shughuli na ndio maana nadhani ni muhimu hizi shughuli zinatakiwa ziongozwe na umoja wa Watanzania pamoja na ubalozi ili kuweka ufanisi zaidi na wewe pia naona ni mtu mahiri unayelewa mambo kwa nini usijribu kumpa huyu Abdul au Jumuiya ya Watanzania ushirikiano wako ili kuboresha mambo.

Mimi nadhani WaTZ lazima tupeane mashavu ili tufanye mambo makubwa na ya maendeleo lakini tukiendelea kupigana vita huku kwenye mitandao hao wanaokosolewa ni rahisi wakawa defensive na kusababisha malumbano badala ya kujadiliana jinsi ya kuungana na kurekebisha mambo kwa manufaa ya sisi wadau ambao hupendelea hizi shughuli ili tukutane na jamaa ambao hatujaonana miaka tele.

Cha msingi tunahitaji chombo chetu cha watanzania chenye nguvu ya watu ambacho wote tutakiunga mkono katika kuendesha masuala ya kijamii hapa Uingereza.

Pamoja tutafika kaka...!!!

Kabisa kabisa.

Tatizo la kutokuwa na umoja wa watanzania UK ni moja tu nalo ni kuchanganya siasa na umoja huo, ukishaanza mambo ya siasa ndani ya umoja matokeo yake ni kutokuwa na umoja thabiti.

Ukichukulia mfano wa kiongozi mmoja maarufu ambae kwa sasa hayupo UK yeye alikuwa katika chama cha CCM na baade akaingia chama cha CHADEMA, sasa hii ni dalili ya kutokuwa na msimamo.

Umoja wa watanzania UK inatakiwa iwe ni taasisi kamili na inayoheshimika na isiyofuata mlengo wowote ule iwe siasa au ushabiki.

Taasisi hii haitaangalia kwamba sherehe za uhuru ni kwa Tanzania bara au Zanzibar bali wataandaa iwe ni kitu kimoja na sherehe itawakutanisha watanzania wote.

Tatizo kubwa la watanzania wa UK kutokuwa na taasisi imara ni ubabaishaji wa wale naopewa dhamana na hili likirekebishwa basi kila kitu kitakwenda sasa.

Mimi hivi karibuni nilikuwa US na nikashangazwa na wenzetu wa US kwamba wana mwalimu wa Kiswahili ambae ana jukumu la kufunza watoto wa kitanzania lugha yetu hiyo mama.

Tukitaka kuwaadabisha watoto silaha kubwa ni lugha ya kwenu na ndio wenzetu wahindi, wasomali na wengine wanafanya, pamoja na kuhakikisha wana mawasiliano ya mara kwa mara na nyumbani Tanzania.

Lakini kwa kupitia taasisi ya watanzania UK kutakuwa na mambo mengi sana ya kutukutanisha, kuanzia biashara, mikutano, sherehe iwe harusi au hata wakati wa majonzi kama vifo.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom