Nssf

victorjane

Member
Joined
Dec 2, 2010
Posts
23
Reaction score
2
Wadau kuna yeyote anayejua kama kuna kilichoendelea katika ajira za nssf mara baada ya kufanya written interview pale ifm?mimi nilifanya katika i.t position
 
Mkuu mi mwenyewe nilfanya i.t kabla ya sabasaba walikuwa bado awajashortlist kuanzia hapo sijui nini kinaendelea hadi nshasahau.
 
Thanks a lot for the info mkuu..hili ni tatizo la kitaifa watu wanatangaza kazi wakati hawajajipanga matokeo yake candidates watakuja kuitwa wakati watu washasahau na washajipanga na mambo mengine
 
Fuatilieni mnaweza mkakuta watu wameshaajiriwa kwenye hizo post mlizofanyia interview,hii ni bongo bana..
 
yaani ajira za bongo hazina maana kabisa tena serikali ndo upuuzi mtupu,unaweza kuitwa kwenye interview kumbe watu walishapatikana yaani wanafanya kama formality,utakuta wakubwa wameshapitisha vimemo na watu wameshapata kazi.Mfano hai kuna jamaa nafanya naye kazi hapa wizara ya afya,huwezi amini hata cheti cha kidato cha nne hakuwa nacho,kaingia kwenye interview hata kujaribu kuongea kimombo hamna kitu,cha ajabu baada ya hapo ilipigwa simu toka juu ikiagiza huyu mheshimiwa lazima apate kazi,na mwisho wa siku alipata na analipwa mshahara mkubwa tu ambao hata hauendani na elimu ambayo nathubutu kusema hana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Jamani kwa kweli hili nalo ni tatizo ambalo ni ugonjwa katika nchi yetu. Upendeleo na ubaguzi ni mkubwa sana nchi hii. Mimi nafanya kwenye shirika moja la umma. Mambo yanayofanyika kwenye idara ya IT na idara zingine kwa ujumla, inasikitisha sana. Mpaka wakati mwingine tunajiuliza hivi kweli MUNGU anaona yote haya?. Boss ameletwa na na mwenye company. Yaani watu wanaajiriwa kutoka nje na the way interview zinavyofanyika yaani MUNGU ndio anajua. Wengine wanaletwa kwa mtindo wa kuchukuwa mtu kutoka nje bila interview.

HR wanaagizwa kumwita mtu ambaye wanamtaka among watu kibao ambao waliomba nfasi zilizowahi kutangazwa kama formality. Na hawakuwahi kuitwa hata mmoja kwa kutangazwa kwenye magazeti. Na wenyewe wanaamua nani wanamtaka na wanampigia simu maana wanafahamiana.

Kisha anafanyiwa interview na mtu mmoja boss kiasi sio Director/ Team ya interview kama mnavyofahamu, laa. Baada ya mtu huyo mmoja akiishafanyiwa interview anapelekwa jina lake kwenye BOARD ili apitishwe. . Kumbuka hajafanya na wezake? Ni yeye tu pekee.
Lakini kumbuka watu wa ndani wapo na wana degree za siku nyingi tu!.

Hawa wanofanyiwa interview za namna hii ni marafiki wa Boss na wanapokuja hata namba ya kazi hajapata anapangwa kwenda kwenye kozi fupi nje ya nchi. Na watu wandani wapo ambao wanafahamu system ya mahali husika. Wafanyakazi wa ndani wanajiuliza sasa sisi tumeonekana hatuna labda CERTIFICATIONS, na hatujui mambo fulani wanaotaka wakubwa. Sasa tunajiuliza kama wanajua kila kitu kwa nini wapelekwe tena kwenye kozi fupi? Maana wasiojua ndio wangepelekwa kwenye mafunzo hayo ya vitendo lwapone magonjwa yao, lakini wapi!

Yaani ukichunguza ni mtu ameahidiwa ULAJI na akitoka ULAYA au jirani Africa wanarudisha FADHILA kwa safari za mara kwa mara kwa wakubwa wanao waajiri. Yaani kuna MAONEVU MAKUBWA NCHI HII ambapo unapotafakari unawaza mpaka unaingia kwenye dhambi na cheo hutapewa ukisema sema. WANAPEWA VYEO NA SAFARI NA UTAGUNDUA BAADAYE KWAMBA NI MARAFIKI ZAO AU NDUGU WA WAKUBWA. WAKIISHA AJIRIWA WANSEMA WENYEWE MIMI NIMEAHIDIWA SAFARI ZA MARA KWA MARA

Ninatafakari hivi DHAMBI hii yakubagua watu na kupendelea watu na kuajiri kinyemela itakwisha lini kwenye WIZARA, MASHIRIKA YA UMMA?
MUNGU ingilia kati DHAMBI HII INANUKA.......
 

JF we dare to talk free and openly, taja hiyo taasisi kuipa hoja yako uzito
 
kweli mkuu tutajie taasisi inawezekana wengine tushawahi kufanya interview huko au tujue hata wakitangaza tusijusumbue kuandika application mkuu
 
Wadau kuna yeyote anayejua kama kuna kilichoendelea katika ajira za nssf mara baada ya kufanya written interview pale ifm?mimi nilifanya katika i.t position
Kuna tatizo kubwa sana pale NSSF ukabila,undugu,udini hutumika sana katika ajira zao,vimemo toka kwa wakubwa ndio mtindo wao.Ukiona wametangaza nafasi 10 ujue 8 zimeshajazwa tayali zilizobaki ndio wanawaachia.
Kuna watu waliajiliwa mwaka jana vimemo vilitoka wizarani na vingine toka kwa DG.Nazungumza haya from my own experiance coz nimefanya nao kazi.
 


Mkuu wewe pia ulijoin kwa vimemo???
 
jana watu wa IT wamefanya Interview....kama hukuitwa jana ,nahisi ndio ntolee...
 
Ni kweli Udini unasumbua na tuwe wakweli waliowengi ni wapemba mfano hapa Dodoma yani kuna binti kaajiwa humu ndani lakn hajui hata kutumia Computer yeye anakazi ya kupiga simu makao makuu then wanamuelekeza na ikumbukwe muda huo anatumia resource za gvt aisee nikashangaa kweli
 
wadau naona hamuoni vizuri nchi hii.TRA mambo yakoje?BOT,FOREIGN AFFAIR.
HAMUONIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII?Mmekazana tu NSSF.BUNGENI.Kote huko udini,ukabila,ukanda umejaa.Fanyeni research hiyo ndio bongo bwana.
 
vimemo kila pahala mmeona NSSF tu.Wadau wizara ya elimu mambo yakoje kwenye scholarship?nilipeleka maombi wizara ya elimu na nina first class kama walivyokuwa wanataka ila wadau nimepigwa chini sababu ni zilezile udini,ukanda,ukabila,
HAMUONIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…