Uncle Araali
JF-Expert Member
- Jul 31, 2014
- 950
- 1,262
WASEMAVYO WANAFASIHI:
"...Kusema haya na haya, duniani kuna vilima na mabonde; kuna kupanda na kushuka; kuna mashaka na raha. Yote hayo hayaendelei, likawa moja tu hilohilo kila siku.
Unapanda kilima kwa mashaka,taabu,kuchoka na jasho kukutoka. Lakini kilima kina mwisho wake; haiwi kuwa utakipanda tu moja kwa moja; mwisho wa kilima utateremka bonde kwa raha na wepesi, na hata ukimaliza bonde hilo, kaa ukijua kuwa mbele yako kuna kilima kingine kinakungoja. Hivi ndivyo dunia inavyokwenda; baada ya dhiki, faraji, na baada ya faraji, dhiki.
..." ( Mohamed S. Abdulla: DUNIANI KUNA WATU)
"...Kusema haya na haya, duniani kuna vilima na mabonde; kuna kupanda na kushuka; kuna mashaka na raha. Yote hayo hayaendelei, likawa moja tu hilohilo kila siku.
Unapanda kilima kwa mashaka,taabu,kuchoka na jasho kukutoka. Lakini kilima kina mwisho wake; haiwi kuwa utakipanda tu moja kwa moja; mwisho wa kilima utateremka bonde kwa raha na wepesi, na hata ukimaliza bonde hilo, kaa ukijua kuwa mbele yako kuna kilima kingine kinakungoja. Hivi ndivyo dunia inavyokwenda; baada ya dhiki, faraji, na baada ya faraji, dhiki.
..." ( Mohamed S. Abdulla: DUNIANI KUNA WATU)