Nusra akamatwe na bosi

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Jamaa wawili walikuwa wameajiriwa kwa Bosi mmoja, baada ya muda wakagundua kuwa Bosi wao alikuwa na tabia ya kuondoka saa 7 mchana na harudi tena mpaka kesho yake. Siku moja wakakubaliana nao wafunge kazi mapema waende zao nyumbani. Moja wao alifika kwake akapata muda mzuri wa kupumzika akaona raha akaazimia kuwa kesho yake lazima atoroke tena. Huyu mwingine kufika kwake kasikia sauti za ajabu toka chumbani kwake, alipochungulia ndani akamkuta bosi wake na mkewe, akafunga mlango haraka na kukimbilia kazini. Kesho yake mwenzie akamwambia tutoroke tena, jamaa akagoma akasema,' Weeee sitaki tena huu mchezo, jana kidogo nikamatwe na Bosi'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…