Nusura niwe muuaji!

Nusura niwe muuaji!

shibela

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
1,068
Reaction score
3,507
Ukimfanyia mtu ubaya, jitenge naye, hata kama anaonekana mpole na mnyonge. Moyo wa mtu ni kama kichaka; huwezi kujua anachoficha.

Hii ni moja ya kumbukumbu mbaya sana maishani mwangu – moja kati ya mbili zilizonikumba.

Kuna mradi niliopanga na Frank, tulipanga vizuri na mipango ikaonekana imekaa sawa. Kosa langu lilikuwa kumuamini Frank na kumwachia yeye awe kiongozi wa mradi huo! Nikatoa akiba yangu yote na kuiweka pale, nikiwa na matumaini makubwa sana.

Miezi miwili tu ikapita, mambo yakaanza kutokuwa sawa na kila siku kulikuwa na kisingizio kipya; mara limeingilia hili, mara limezuka lile! Miezi ilizidi kusonga na taa nyekundu ikawa imewaka kichwani, lakini nikaendelea kujidanganya, sitaki kukubali kama Frank ananidhurumu!

Lakini ukweli ukabainika – Frank kanidhurumu! Nilijaribu kumwambia anirudishie hata nusu ya gharama zangu, lakini akaanza kunizungusha tu, mara anatabasamu kana kwamba hakufanya kosa lolote. Moyo ulikuwa unaniuma sana, nikiwa na stress balaa, hakuna kitu kilichokuwa kinaniendea sawa. Nakiri wazi kuwa hata mapenzi hayajawahi kuniumiza kama dhuruma aliyonifanyia Frank!

Wakati huo, Frank kwake ni kama hakuna kilichotokea; maisha yake yanaendelea vizuri tu.

Nilijikuta nawaza namna gani nitaweza kumkomesha Frank, nikafikiria mpaka kumpa kilema cha maisha ili kila atakapojiona anikumbuke. Lakini hilo wazo lilikataliwa na akili yangu. Sikupenda kushirikisha mtu kwenye hili maana najua hakuna siri ya watu wawili.

Mwisho wa yote, nikajikuta nafikiria kumuua Frank kwa mikono yangu. Hasira ilikuwa imenikamata kiasi kwamba natetemeka, na karibu naanza kuchanganyikiwa. Kila mtu aliyeniuliza kuna nini, nilijikuta nakosa maneno na naishia kulia kwa uchungu. Moyo na akili vilikuwa vimevurugika kabisa, huku mvurugaji anatamba tu mjini kana kwamba hakutenda dhambi.

Nilipanga mpango wangu – nitaondoka nchi bila kuacha alama yoyote, na sitorudi tena mpaka kifo.

Siku hiyo nikampigia simu Frank, nikamwomba tukutane naye akakubali.

Mimi: Una watoto wangapi?

Frank: Hujui nina watoto wangapi? Mbona umeuliza hivyo?

Mimi: Napenda sana watoto. Mimi na Ngosha tunataka kuoana, na ninataka uwe kwenye kamati!

Frank: Sawa, hakuna shida, tutawasiliana!

Hii ilikuwa njia rahisi ya kuhakikisha atakuwa kwenye ratiba yangu.

Nikaomba ruhusa ya muda mfupi kazini na kurudi nyumbani, nikiwa na mpango wa kumuaga mama yangu kabla sijajiharibia maisha yangu.

Nilipofika, mama alinipokea vizuri, akiwa mwenye furaha na kujivunia sana mimi. Tulikuwa tunatembea pamoja kila wakati, na kila tukikutana na mtu lazima ananitambulisha kwa furaha – hata kama hajamuuliza. "Huyu ndiye mwanangu wa mkoa fulani, anafanya kazi fulani!" huku mimi nikiwa sitaki kujulikana kazi yangu hasa ni ipi!

Upendo wa mama yangu ulinifanya nipate utulivu wa fikra, nikawa na amani tena. Nikajiuliza: kwa nini nimuumize mama kwa kwenda jela au kuikimbia nchi kwa jambo kama hili? Pesa zimepotea, lakini nitapata nyingine. Mradi sijapoteza kazi, mikono, au miguu, bado nina nafasi ya kusonga mbele.

Mpaka leo naamini kuwa nilikosa tu ushauri mzuri wakati ule nilipodhurumiwa, na ndio sababu nilifikia mawazo ya mbali.
 
c8a965f4c21db39b150c53e2d3f21846.jpg
 
Ukimfanyia mtu ubaya, jitenge naye, hata kama anaonekana mpole na mnyonge. Moyo wa mtu ni kama kichaka; huwezi kujua anachoficha.

Hii ni moja ya kumbukumbu mbaya sana maishani mwangu – moja kati ya mbili zilizonikumba.

Kuna mradi niliopanga na Frank, tulipanga vizuri na mipango ikaonekana imekaa sawa. Kosa langu lilikuwa kumuamini Frank na kumwachia yeye awe kiongozi wa mradi huo! Nikatoa akiba yangu yote na kuiweka pale, nikiwa na matumaini makubwa sana.

Miezi miwili tu ikapita, mambo yakaanza kutokuwa sawa na kila siku kulikuwa na kisingizio kipya; mara limeingilia hili, mara limezuka lile! Miezi ilizidi kusonga na taa nyekundu ikawa imewaka kichwani, lakini nikaendelea kujidanganya, sitaki kukubali kama Frank ananidhurumu!

Lakini ukweli ukabainika – Frank kanidhurumu! Nilijaribu kumwambia anirudishie hata nusu ya gharama zangu, lakini akaanza kunizungusha tu, mara anatabasamu kana kwamba hakufanya kosa lolote. Moyo ulikuwa unaniuma sana, nikiwa na stress balaa, hakuna kitu kilichokuwa kinaniendea sawa. Nakiri wazi kuwa hata mapenzi hayajawahi kuniumiza kama dhuruma aliyonifanyia Frank!

Wakati huo, Frank kwake ni kama hakuna kilichotokea; maisha yake yanaendelea vizuri tu.

Nilijikuta nawaza namna gani nitaweza kumkomesha Frank, nikafikiria mpaka kumpa kilema cha maisha ili kila atakapojiona anikumbuke. Lakini hilo wazo lilikataliwa na akili yangu. Sikupenda kushirikisha mtu kwenye hili maana najua hakuna siri ya watu wawili.

Mwisho wa yote, nikajikuta nafikiria kumuua Frank kwa mikono yangu. Hasira ilikuwa imenikamata kiasi kwamba natetemeka, na karibu naanza kuchanganyikiwa. Kila mtu aliyeniuliza kuna nini, nilijikuta nakosa maneno na naishia kulia kwa uchungu. Moyo na akili vilikuwa vimevurugika kabisa, huku mvurugaji anatamba tu mjini kana kwamba hakutenda dhambi.

Nilipanga mpango wangu – nitaondoka nchi bila kuacha alama yoyote, na sitorudi tena mpaka kifo.

Siku hiyo nikampigia simu Frank, nikamwomba tukutane naye akakubali.

Mimi: Una watoto wangapi?

Frank: Hujui nina watoto wangapi? Mbona umeuliza hivyo?

Mimi: Napenda sana watoto. Mimi na Ngosha tunataka kuoana, na ninataka uwe kwenye kamati!

Frank: Sawa, hakuna shida, tutawasiliana!

Hii ilikuwa njia rahisi ya kuhakikisha atakuwa kwenye ratiba yangu.

Nikaomba ruhusa ya muda mfupi kazini na kurudi nyumbani, nikiwa na mpango wa kumuaga mama yangu kabla sijajiharibia maisha yangu.

Nilipofika, mama alinipokea vizuri, akiwa mwenye furaha na kujivunia sana mimi. Tulikuwa tunatembea pamoja kila wakati, na kila tukikutana na mtu lazima ananitambulisha kwa furaha – hata kama hajamuuliza. "Huyu ndiye mwanangu wa mkoa fulani, anafanya kazi fulani!" huku mimi nikiwa sitaki kujulikana kazi yangu hasa ni ipi!

Upendo wa mama yangu ulinifanya nipate utulivu wa fikra, nikawa naA amani tena. Nikajiuliza: kwa nini nimuumize mama kwa kwenda jela au kuikimbia nchi kwa jambo kama hili? Pesa zimepotea, lakini nitapata nyingine. Mradi sijapoteza kazi, mikono, au miguu, bado nina nafasi ya kusonga mbele.

Mpaka leo naamini kuwa nilikosa tu ushauri mzuri wakati ule nilipodhurumiwa, na ndio sababu nilifikia mawazo ya mbali.
nakupenda sana mrembo
 
Pole sana na kingine tukiaminiwa tuaminike wakuu, dhuluma sio nzuri.

Usimuoneshe mtu 100% yakuwa unamwamini, hili huwa ni kosa kubwa sana maana binadamu huwa tuna tabia ya kubadilika.

Kwenye uwekezaji hasa biashara haipaswi kuwekeza fungu lote ulilonalo, kuna risks na mabadiliko mengine ambapo kama umetia mzigo wote unakuwa huna msaada au pa kugeukia.
 
Ukimfanyia mtu ubaya, jitenge naye, hata kama anaonekana mpole na mnyonge. Moyo wa mtu ni kama kichaka; huwezi kujua anachoficha.

Hii ni moja ya kumbukumbu mbaya sana maishani mwangu – moja kati ya mbili zilizonikumba.

Kuna mradi niliopanga na Frank, tulipanga vizuri na mipango ikaonekana imekaa sawa. Kosa langu lilikuwa kumuamini Frank na kumwachia yeye awe kiongozi wa mradi huo! Nikatoa akiba yangu yote na kuiweka pale, nikiwa na matumaini makubwa sana.

Miezi miwili tu ikapita, mambo yakaanza kutokuwa sawa na kila siku kulikuwa na kisingizio kipya; mara limeingilia hili, mara limezuka lile! Miezi ilizidi kusonga na taa nyekundu ikawa imewaka kichwani, lakini nikaendelea kujidanganya, sitaki kukubali kama Frank ananidhurumu!

Lakini ukweli ukabainika – Frank kanidhurumu! Nilijaribu kumwambia anirudishie hata nusu ya gharama zangu, lakini akaanza kunizungusha tu, mara anatabasamu kana kwamba hakufanya kosa lolote. Moyo ulikuwa unaniuma sana, nikiwa na stress balaa, hakuna kitu kilichokuwa kinaniendea sawa. Nakiri wazi kuwa hata mapenzi hayajawahi kuniumiza kama dhuruma aliyonifanyia Frank!

Wakati huo, Frank kwake ni kama hakuna kilichotokea; maisha yake yanaendelea vizuri tu.

Nilijikuta nawaza namna gani nitaweza kumkomesha Frank, nikafikiria mpaka kumpa kilema cha maisha ili kila atakapojiona anikumbuke. Lakini hilo wazo lilikataliwa na akili yangu. Sikupenda kushirikisha mtu kwenye hili maana najua hakuna siri ya watu wawili.

Mwisho wa yote, nikajikuta nafikiria kumuua Frank kwa mikono yangu. Hasira ilikuwa imenikamata kiasi kwamba natetemeka, na karibu naanza kuchanganyikiwa. Kila mtu aliyeniuliza kuna nini, nilijikuta nakosa maneno na naishia kulia kwa uchungu. Moyo na akili vilikuwa vimevurugika kabisa, huku mvurugaji anatamba tu mjini kana kwamba hakutenda dhambi.

Nilipanga mpango wangu – nitaondoka nchi bila kuacha alama yoyote, na sitorudi tena mpaka kifo.

Siku hiyo nikampigia simu Frank, nikamwomba tukutane naye akakubali.

Mimi: Una watoto wangapi?

Frank: Hujui nina watoto wangapi? Mbona umeuliza hivyo?

Mimi: Napenda sana watoto. Mimi na Ngosha tunataka kuoana, na ninataka uwe kwenye kamati!

Frank: Sawa, hakuna shida, tutawasiliana!

Hii ilikuwa njia rahisi ya kuhakikisha atakuwa kwenye ratiba yangu.

Nikaomba ruhusa ya muda mfupi kazini na kurudi nyumbani, nikiwa na mpango wa kumuaga mama yangu kabla sijajiharibia maisha yangu.

Nilipofika, mama alinipokea vizuri, akiwa mwenye furaha na kujivunia sana mimi. Tulikuwa tunatembea pamoja kila wakati, na kila tukikutana na mtu lazima ananitambulisha kwa furaha – hata kama hajamuuliza. "Huyu ndiye mwanangu wa mkoa fulani, anafanya kazi fulani!" huku mimi nikiwa sitaki kujulikana kazi yangu hasa ni ipi!

Upendo wa mama yangu ulinifanya nipate utulivu wa fikra, nikawa na amani tena. Nikajiuliza: kwa nini nimuumize mama kwa kwenda jela au kuikimbia nchi kwa jambo kama hili? Pesa zimepotea, lakini nitapata nyingine. Mradi sijapoteza kazi, mikono, au miguu, bado nina nafasi ya kusonga mbele.

Mpaka leo naamini kuwa nilikosa tu ushauri mzuri wakati ule nilipodhurumiwa, na ndio sababu nilifikia mawazo ya mbali.
Pole sana aisee, hela inavyo patikana kwa usumbufu mkubwa kiasi hiki halafu atokee mtu aipoteze kwa wepesi kisha aonyeshe kutokujali huwa ina uma kusiko weza kuelezeka.

Vyovyote ungefanya lakini thamani ya uhai haijawahi kulingana na chochote, uhai au maisha ya mtu au chochote hayakutokea kwa bahati mbaya hivyo hio hela inakosa thamani mara nyingi sana mbele ya uhai .

Pia ni heri kushirikisha pito lolote unalopitia, hata mtoto unaweza kuongea nae kumuelezea maumivu ulio nayo hata kama hatakuambia pole ila kule kusema kuna saidia mno.

Shukurani kwa upendo wa mama ulikunusuru na mengi ndugu yangu .
 
Ukimfanyia mtu ubaya, jitenge naye, hata kama anaonekana mpole na mnyonge. Moyo wa mtu ni kama kichaka; huwezi kujua anachoficha.

Hii ni moja ya kumbukumbu mbaya sana maishani mwangu – moja kati ya mbili zilizonikumba.

Kuna mradi niliopanga na Frank, tulipanga vizuri na mipango ikaonekana imekaa sawa. Kosa langu lilikuwa kumuamini Frank na kumwachia yeye awe kiongozi wa mradi huo! Nikatoa akiba yangu yote na kuiweka pale, nikiwa na matumaini makubwa sana.

Miezi miwili tu ikapita, mambo yakaanza kutokuwa sawa na kila siku kulikuwa na kisingizio kipya; mara limeingilia hili, mara limezuka lile! Miezi ilizidi kusonga na taa nyekundu ikawa imewaka kichwani, lakini nikaendelea kujidanganya, sitaki kukubali kama Frank ananidhurumu!

Lakini ukweli ukabainika – Frank kanidhurumu! Nilijaribu kumwambia anirudishie hata nusu ya gharama zangu, lakini akaanza kunizungusha tu, mara anatabasamu kana kwamba hakufanya kosa lolote. Moyo ulikuwa unaniuma sana, nikiwa na stress balaa, hakuna kitu kilichokuwa kinaniendea sawa. Nakiri wazi kuwa hata mapenzi hayajawahi kuniumiza kama dhuruma aliyonifanyia Frank!

Wakati huo, Frank kwake ni kama hakuna kilichotokea; maisha yake yanaendelea vizuri tu.

Nilijikuta nawaza namna gani nitaweza kumkomesha Frank, nikafikiria mpaka kumpa kilema cha maisha ili kila atakapojiona anikumbuke. Lakini hilo wazo lilikataliwa na akili yangu. Sikupenda kushirikisha mtu kwenye hili maana najua hakuna siri ya watu wawili.

Mwisho wa yote, nikajikuta nafikiria kumuua Frank kwa mikono yangu. Hasira ilikuwa imenikamata kiasi kwamba natetemeka, na karibu naanza kuchanganyikiwa. Kila mtu aliyeniuliza kuna nini, nilijikuta nakosa maneno na naishia kulia kwa uchungu. Moyo na akili vilikuwa vimevurugika kabisa, huku mvurugaji anatamba tu mjini kana kwamba hakutenda dhambi.

Nilipanga mpango wangu – nitaondoka nchi bila kuacha alama yoyote, na sitorudi tena mpaka kifo.

Siku hiyo nikampigia simu Frank, nikamwomba tukutane naye akakubali.

Mimi: Una watoto wangapi?

Frank: Hujui nina watoto wangapi? Mbona umeuliza hivyo?

Mimi: Napenda sana watoto. Mimi na Ngosha tunataka kuoana, na ninataka uwe kwenye kamati!

Frank: Sawa, hakuna shida, tutawasiliana!

Hii ilikuwa njia rahisi ya kuhakikisha atakuwa kwenye ratiba yangu.

Nikaomba ruhusa ya muda mfupi kazini na kurudi nyumbani, nikiwa na mpango wa kumuaga mama yangu kabla sijajiharibia maisha yangu.

Nilipofika, mama alinipokea vizuri, akiwa mwenye furaha na kujivunia sana mimi. Tulikuwa tunatembea pamoja kila wakati, na kila tukikutana na mtu lazima ananitambulisha kwa furaha – hata kama hajamuuliza. "Huyu ndiye mwanangu wa mkoa fulani, anafanya kazi fulani!" huku mimi nikiwa sitaki kujulikana kazi yangu hasa ni ipi!

Upendo wa mama yangu ulinifanya nipate utulivu wa fikra, nikawa na amani tena. Nikajiuliza: kwa nini nimuumize mama kwa kwenda jela au kuikimbia nchi kwa jambo kama hili? Pesa zimepotea, lakini nitapata nyingine. Mradi sijapoteza kazi, mikono, au miguu, bado nina nafasi ya kusonga mbele.

Mpaka leo naamini kuwa nilikosa tu ushauri mzuri wakati ule nilipodhurumiwa, na ndio sababu nilifikia mawazo ya mbali.
Hii kitu nimejifunza wiki 1 iliyopita kwamba ukipata shida kama unaona uwezo wako umefika mwisho kulifanyia utatuzi jaribu kumshirikisha mtu wako wa karibu naamini utapata mwangaza mpya kuliko unapobaki nalo moyoni unaweza kujisababishia afya ya mwili na akili, hata kama huyo mtu hana uwezo wa kulitatua suala lako ila unapomueleza unapunguza hasira na sumu iliyo katika moyo wako na ukipata nafasi ya kulia we lia tu haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke ila unapotoa chozi kuna ugumu uliokuwa nao katika moyo utaachia taratibu utaona unakaa sawa huenda ata akili itaanza kurecover na kulifikilia jambo lako kwa sura chanya.

N:B - Usipende kumweleza kila mtu matatizo yako tafuta mtu sahihi either wa karibu yako ambaye ana high thinking capacity kwa maana ata kama hatokusaidia huenda atakupa ushauri utakao kupatia utatuzi au tafuta mtaalamu wa saikolojia utapata mwangaza katika utatuzi wa jambo lako.

IT'S OK TO NOT BE OK.
AKILI YA MWENZAKO CHANGANYA NA YAKO.

✍🏾Nawasilisha.
 
Umenikumbusha miaka mingi nyuma nilivyokua natega pambizoni mwa barabara nikimvizia mtesi wangu alikua anapenda kukatisha barabara hiyo ya mtaa majira ya jioni.
Baasi nilikua namsubiria huku nimekunja ndita kwa hasira akitokeza tu nikamgongelee mbali kama mbwai iwe mbwai.
Ila naye alikua kama ana machale hivi siku zote hizo nilifeli. Mpaka nilipoamua kuachana naye.
 
Dhulumu☑️
Dhurumu❌,,,Hakikisha anarudisha pesa yako,,,Karibu Mkoa Fulani
Mwenyekiti wa baraza la kiswahili kuna vitu jifunze uviache vipite katika maisha yako kwa usalama wako na kizazi chako, makosa yapo ili kutujenga ukilipa wema kwa ubaya uliofanyiwa inaumiza zaidi.
 
Back
Top Bottom