Nyankurungu: Hayati Rais Magufuli hakuwa na tozo ni kweli. Yeye alikuwa na "Presumtive Tax assessment" tulilipa kodi hadi za enzi ya Mkapa na Kikwete

Utalii uko rebound na ule mgodi wa dhahabu nyanzaga kuanza na viwanda vya kusafisha dhahabu vikifika ata peak sidhan kama mama atakamatika.

Maumivu ya Sasa ni ya miaka 2 kwa sababu uchumi ukiharibika Sana kwa hiyo recovering yake kwa mda mfupi itaumiza.

Nachomkubali Maza hana mda wa kuropoka na kufoka foka wanaelekezana kimya kimya na wasimamizi/ washauri wake kama mawaziri nk tone yao sasa wameanza kumuelewa na kumpigania.
 
Mimi mkoa niliko Maza katangaza km 75 za barabara za lami 3,km 25 kila barabara lakini Magu alizikuta na hakufanya lolote.

Maza mimi namuelewa kinyama.
 
Sawa ila isipande kwa kukomoana, mfano kwenye miamala, nnapotuma pesa ikatwe na anaeto hyo hyo pesa akatwe. Kwa 5000 ukakate 1500 yote mbona n kama unyonyaji.
 
Katika Marais wote naona alikuwa anaenda vizuri kujenga ni uchumi ni Magufuli! Alienda kujenga vyonzo vya mda mrefu vya mapato matharani kubana zaidi kwenye madini, mashirika kutoa gawio, ujenzi wa miundombinu kama barabara, airport ujenzi wa rada, ujenzi wa vyombo vya usafiri na ukarabati wa meli katika maziwa yetu pamoja na ujenzi wa reli ya sgr pamoja ujenzi wa bwawa la umeme huko Rufiji.
 
Kwanza ni kweli pasi na shakha kipindi cha nyuma kabla ya Magufuli ilikuwa kawaida tu kutolipa kodi ata kwa wafanya biashara wakubwa na wengi walikwepa na hapo magufuli ndo alipo wabambia.
 

Kupora hela halali za wafanyabiashara hata siku moja sio kujenga uchumi bali ni kubomoa ,take my words itatuchukukua miaka mingine ishirini kuweza kufikia level ya shuguli za kiuchumi zilizokuwepo kwa mwaka 2015
 
Unafahamu presumptive tax ni kitu gani?

Kila mfanyabiashara yupo elligible kwa ajili ya presumptive tax?

Unajua sababu za kufanya makusanyo yapae kutoka bil 700 mpaka tril 1.5 wakati wa hayati JPM?
 
Kwanza ni kweli pasi na shakha kipindi cha nyuma kabla ya Magufuli ilikuwa kawaida tu kutolipa kodi ata kwa wafanya biashara wakubwa na wengi walikwepa na hapo magufuli ndo alipo wabambia.
Acha usanii
 
Kupora hela halali za wafanyabiashara hata siku moja sio kujenga uchumi bali ni kubomoa ,take my words itatuchukukua miaka mingine ishirini kuweza kufikia level ya shuguli za kiuchumi zilizokuwepo kwa mwaka 2015
Tatizo lenu mnapenda ushabiki. Mnaona bora mfanyabiashara mkubwa akwepe kodi lakini awapatie pesa ya soda na jojo wanamichezo.
 
Acha blah blah bandika ushahidi wa mfumo halisi wa ukokotoaji sio kuweka maneno yako mwenyewe.

Kwa sasa wafanyabiashara wakubwa hawalipi kodi kabisa
1. Ushahidi Nenda Kariakoo au Samora kisha nunua kitu chochote halafu dai risiti uone kitakachotokea
2. Nenda Uhuru na mtaa wa Kongo ingia duka lolote la bidhaa unayohitaji nunua kisha dai risiti usikie utakachoambiwa
3. Nenda Ilala au Temeke kwa wauza vipuri vya magari nunua kisha dai risiti uone kama ujasiri wako utakushauri ubaki eneo hilo
4. Mashine za EFD karibu kila siku unapodai risiti huonekana havifanyi kazi
5. Maghorofa yaliyosimama ujenzi miaka mitano iliyopita kwa sasa karibia yote yanakabia kumalizika, yanajengwa kwa kasi ya ajabu
6. Wamachinga biashara imedoda wengine mpaka wameacha wanatafuta kazi ya shamba boy
 
Ungejibu kuhusu shutuma hizo za UONGO wa chama chenu ili kututoa shaka sisi wananchi tusio na vyama.Hao nao wana lao la kujibu.
 
Vizuri.Mawazo na hoja zako hazina budi kuheshimiwa lakini ungebalance kwa kudadavua shutuma ambazo hayati anashutumiwa ili kuwasaidia wasio na upande(team) kama mimi kuweza kuchuja mbivu na mbichi.
 
Kwenye namba 6 ndio umejichanganya maana hao wakubwa ndio walikuwa wanawapa machinga mizigo na wanauza bila kutoa risiti, Sasa Bora wauze wenyewe
 
Washabiki wa Mama wengi waimba taarab,naamini 2025 Maji yakimfikia shingoni Mama yenu,basi atamuita Mama Janet aje amsaidie,
 
Ungejibu kuhusu shutuma hizo za UONGO wa chama chenu ili kututoa shaka sisi wananchi tusio na vyama.Hao nao wana lao la kujibu.
Kama ww hauna chama ni kwann unalazimisha mimi niwe na chama? Wote hatuna chama, lkn ukweli lazima uzingatiwe na viongozi wote bila kujali vyama vyao. Hatuwezi kuongelea uongo wa upande mmoja tukaacha wa upande wa pili afu tukija kuwachagua waje na uongo zaidi ya huu tunaoongelea hapa. Itakuwa haina maana ya mabadiliko.
 
Nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa maji na mafuta yanaweza kuchanganyika.

Muda ni muamuzi mzuri, tuendelee kusubiri.
 
Magufuli alirithi Hitachi ya ambition ya $, katika Benki kuu, lakini yeye hakuacha hata senti na made ni juu.

Pili Mama hana tabia ya kupora watu
 


Umetisha sana 🤛🏿
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…