Nyanya Za Mshumaa/Chungu/Ngogwe Za Kukaanga

Nyanya Za Mshumaa/Chungu/Ngogwe Za Kukaanga

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
nyanya%20mshumaa-chungu.JPG

Vipimo

Nyanya za mshumaa/chungu 20 kiasi


Kitunguu 1


Nyanya/tungule 2


Mafuta ya zaytuni (olive oil) 3 vijiko vya supu


Pilipili mbichi 1


Kitunguu saumu(thomu/galic) 3 chembe

Chumvi kiasi



Namna Ya Kutayarisha Na Kupika




  1. Osha nyanya za mshumaa/chungu kisha zichemshe kidogo.



bittereggplant.jpg




  1. Mwaga maji, menya maganda na ukatekate vipande vipande.


  1. Katakata kitunguu, nyanya vipande vidogovidogo (chopped)


  1. Saga au katakata pilipili mbichi na thomu.



  1. Weka mafuta katika sufuria, tia vitu vyote pamoja. Kaanga kwa muda huku unakoroga hadi iwive.


  1. Pakuwa katika chombo, nyunyizia mafuta ya zaytuni.
 
Mie napenda za nazi au katika soup ya samaki iwe na vegetables na hii naweka mwisho karibu ya kuepua inakua nzuriii
 
mie napenda manake zinajenga heshima kwa afya ya ndoa lol!!
 
Back
Top Bottom