Nyaraka mpya za Kagoda zawalipua Rostam, Manji

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,380

Attachments

Kesho nakutana na DPP kuweza kuongea naye juu ya ushahidi niliowasilisha juu ya walioiba fedha za umma kupitia Kagoda

Nina picha, video zinazoonyesha wizi wa Kagoda wazi.

Kinara wa wizi huu ni Rostam Aziz aliyekuwa mbunge wa Igunga.

Wa pili ni Yusufu Manji

Wanaohusika serikali inadai haiwafahamu. Nawafahamu na wanakaa Kinondoni na walifanya hivyo kwa maelekezo ya Rostam Aziz.

Walioenda Brela kusajili kampuni tuna picha zao na majina yaliyoandikwa ni ya uwongo.

Jina Kagoda linatokana na KATO na GODA.

Angalia nyaraka zilizoambatanishwa.

Baada ya Kagoda kufunguliwa, ilitakiwa itengenezwe account ambayo ilitengenezwa CRDB na mdhamini alikuwa Yusufu Manji (angalia attachment chini ya 1st post ikionyesha na account number).

BoT wanawajua wahusika wote kwani pesa zilihamishwa kwa ushirikiano na CRDB.

Bharat Goda kwa maelekezo ya Rostam Aziz alipeleka barua inayoonyesha kuwa Bil 8 ziende kwenye account tofauti. Viambatanisho vipo, hivyo zikaongezwa kwenye Bil 25 nyingine iliyokuwa kwenye account tofauti.

Bil 33 baadae zilihamishwa kwenda kwenye account nyingine ambayo Yusufu Manji aliidhamini huko Holland Branch

Pesa hizi baadae zilitoroshwa kwenda Dubai kwa ushirikiano wa Yusufu Manji kwenye mafungu ya $ milioni moja moja. Kwa kutumia kampuni ya Quality Finance Corp
 
Dah,ngoja niicheki kwa makini kwanza
 
Hizi nyuzi za hatari!
Hebu endelea kutujuza mkuu
 
Magamba watamtumia tena RA kwenye kampeni Igunga? Msema kweli ni nani tena jamani?
 
Bil 33 baadae zilihamishwa kwenda kwenye account nyingine ambayo Yusufu Manji aliidhamini huko Holland Branch

Hivi hawa jamaaa hwakuzirudisha hizo pesa? Nasikia kuna wengine walirudisha zikapelekwa TIB kwa Peter Noni na hiyo wakapewa msamaha wa kuburuzwa mahakamani!!
 
Msemakweli ni nani huyoo jamani?
 
Kamati ya Mwanyika ilikataa habari za Manji za kujitetea kuwa hakuhusika na Kagoda kwa kudai kuwa babake ndo alihusika. Mwanyika na wenzake walichofanya ni kufunga account zote za Quality Finance Corp. Wakazuia passport yake asitoke nje ya nchi. Walidhamiria kumfirisi, na akadai kuwa alikopeshwa na Kagoda na Rostam akamshauri kuwa bora warudishe hela hizo
 
Weka mambo kaka, sisi tusasoma tuma tu
 
Kampuni ya Afritainer ilirejesha kiasi cha kama Bil 3 hivi (na ushahidi upo). Wakurugenzi wa kampuni hii ni wajomba zake Rostam, wamefanya uhuni mwingine wa kuwaondoa hawa wajomba zake kama wakurugenzi na kuwaweka wakurugenzi feki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…