Nyaya za TTCL Dar es Salaam ni uchafuzi wa mazingira. Mamlaka zifanye jambo

Nyaya za TTCL Dar es Salaam ni uchafuzi wa mazingira. Mamlaka zifanye jambo

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,311
Reaction score
15,640
Kweli sijui kama TTCL wanajielewa aisee. Unapopita maeneo mengi yenye mazingira mazuri na yaliyopendeza, unakutana na nyaya za TTCL zilizopita hovyohovyo, nyingine zikiwa zinaning'inia chini, huku nguzo zimepinda ovyo bila anayejali. NEMC wanapaswa kuwadhibiti hawa jamaa, maana inaonekana hawajui au hawajali kabisa.

Kiufupi, taswira ya jiji la Dar es Salaam inachafuliwa na hizi nyaya za TTCL. Zimekuwa kama uchafu; hazina mpangilio, utadhani zimefungwa na mateja. Sio Oysterbay, Masaki, Posta, Mikocheni wala Mbezi – kote ni uchafu wao unaoharibu sura ya mji.

TTCL, hebu kuweni serious basi. Zifungeni kwa mpangilio, zipitisheni chini, au mkate na kuziondoa kabisa kama hazitumiki.
 
Unakuta wire mmoja umedondoka chini nyingine zipo vipande zinaning'inia kwenye nguzo vinguzo vyao wanavishikamanisha vingi vingi sometimes vinakuwa katikati ya nguzo za Tanesco.

Bado kuchanganya nyaya zinazotumika na zisizotumika,sijui kwanini jamaa ni wavivu hawatoi kabisa wire zilizokatika,unakuta line moja ina wire zaidi ya sita ukiangalia kwa umakini unagundua nne zimeishia katikati means hazina kazi kwa sababu zilikatika.
 
Unakuta wire mmoja umedondoka chini nyingine zipo vipande zinaning'inia kwenye nguzo vinguzo vyao wanavishikamanisha vingi vingi sometimes vinakuwa katikati ya nguzo za Tanesco.

Bado kuchanganya nyaya zinazotumika na zisizotumika,sijui kwanini jamaa ni wavivu hawatoi kabisa wire zilizokatika,unakuta line moja ina wire zaidi ya sita ukiangalia kwa umakini unagundua nne zimeishia katikati means hazina kazi kwa sababu zilikatika.
Yaani inaonesha wazi wanavyolipua kazi zao kisa ni taasisi ya serikali. Ufungaji wao wa hizi nyaya hata teja hawezi funga vile,unakuta bunda la wire linaning'inia miaka yote utasema ni mtu aliliacha jana ili aje aendelee na kazi ya ufungaji nyaya. Yaani hopeless kabisa
 
Kweli sijui kama TTCL wanajielewa aisee. Unapopita maeneo mengi yenye mazingira mazuri na yaliyopendeza, unakutana na nyaya za TTCL zilizopita hovyohovyo, nyingine zikiwa zinaning'inia chini, huku nguzo zimepinda ovyo bila anayejali. NEMC wanapaswa kuwadhibiti hawa jamaa, maana inaonekana hawajui au hawajali kabisa.

Kiufupi, taswira ya jiji la Dar es Salaam inachafuliwa na hizi nyaya za TTCL. Zimekuwa kama uchafu; hazina mpangilio, utadhani zimefungwa na mateja. Sio Oysterbay, Masaki, Posta, Mikocheni wala Mbezi – kote ni uchafu wao unaoharibu sura ya mji.

TTCL, hebu kuweni serious basi. Zifungeni kwa mpangilio, zipitisheni chini, au mkate na kuziondoa kabisa kama hazitumiki.
Picha
 
HIvi zile simu zao zilizokua zinatumia antena zilikua na shida gani mpaka wakarudi tena na haya manyaya
 
HIvi zile simu zao zilizokua zinatumia antena zilikua na shida gani mpaka wakarudi tena na haya manyaya
Nyaya ni kwa ajili ya internet ila wamekua wapuuzi wanaziacha hovyohovyo tu kama uchafu. I don't know how much does it cost kuzifunga vizuri
 
Back
Top Bottom