Nyerere hakukosea

Nyerere hakukosea

Ustaadh

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2009
Posts
413
Reaction score
19
"Inawezekana tatizo la paka kwa panya lingekwisha kama paka angefungiwa kengele shingoni: taabu ni kumpata panya wa kuifanya kazi hiyo. Na panya watakuwa wajinga sana wakidhani kuwa paka watajifunga au watafungana kengele shingoni" - Mwl. J. K. Nyerere

MWALIMU NYERERE ALIKUWA SAHIHI, TUSITARAJIE KUWA CCM WATAONDOKA MADARAKANI KWA KWA HIARI YAO WENYEWE. NI LAZIMA TUKUBALI GHARAMA YA "PANYA KUMFUNGA PAKA KENGELE". MABADILIKO LAZIMA YATOKEE KWA GHARAMA YOYOTE ILE ILI KUINUSURU NCHI YETU VINGINEVYO TUTAENDELEA KULIA NA KUSAGA MENO!
 
Nyerere ndiye aliyesababisha hii CCM itawale milele. Ni makosa kumtumia Nyerere as an example leader.
 
Shamu,
Lakini CCM ya leo si ile aliyoiasis JKN. Hawana uadilifu, hawana upendo wa watu, hawana mwelekeo.
 
Nyerere ndiye aliyesababisha hii CCM itawale milele. Ni makosa kumtumia Nyerere as an example leader.

Wewew ni Fisadi wa Mawazo , na una chuki binafsi na wivu!

Mtu yeyote mwenye akili za kawaida anaona wazi utofauti wa uongozi kati ya enzi hizo mbili...wewe unaishi wapi?

Nyerere alisababisha vp CCm itawale milele?

Au huwa anakuja siku ya kura kama jinamizi na
kukulazimisha uipigie kura sisiemu?...Tueleze mwenzetu inakuwakuwaje!
 
si "mapaka" tena bali ni "mambwa".......kaaazi kweli kweli
 
Wewew ni Fisadi wa Mawazo , na una chuki binafsi na wivu!

Mtu yeyote mwenye akili za kawaida anaona wazi utofauti wa uongozi kati ya enzi hizo mbili...wewe unaishi wapi?

Nyerere alisababisha vp CCm itawale milele?

Au huwa anakuja siku ya kura kama jinamizi na
kukulazimisha uipigie kura sisiemu?...Tueleze mwenzetu inakuwakuwaje!

Why he chose to change the constitution in order to benefit one party? Tofauti kubwa ya Nyerere na viongozi wa sasa hivi ni kwamba, now we live on open society, democracy, freedom, and freedom of press. There were a lot of bad things that happened when Nyerere was a leader. Hakuna mtu au kiongozi aliyethubutu kuripoti, au kuzungumza jambo lolote baya linalohusu CCM.
 
Why he chose to change the constitution in order to benefit one party? Tofauti kubwa ya Nyerere na viongozi wa sasa hivi ni kwamba, now we live on open society, democracy, freedom, and freedom of press. There were a lot of bad things that happened when Nyerere was a leader. Hakuna mtu au kiongozi aliyethubutu kuripoti, au kuzungumza jambo lolote baya linalohusu CCM.
Shamu,
Nani alikushika mdomo wakati huo? Mbona wengine tulikuwa tunazungumza na bado tunadunda?
 
Shamu,
Lakini CCM ya leo si ile aliyoiasis JKN. Hawana uadilifu, hawana upendo wa watu, hawana mwelekeo.


Jasusi,

Nyerere alichangia kwa kiasi kidogo yote yaliyopo sasa hivi. Aliwaamini mbwa mwitu.. angewachnguza kidogo angebaini.... uwezo alikuwa nao.
 
Jasusi,

Nyerere alichangia kwa kiasi kidogo yote yaliyopo sasa hivi. Aliwaamini mbwa mwitu.. angewachnguza kidogo angebaini.... uwezo alikuwa nao.
FairPlayer,
Ningekubaliana na wewe kama sote tungejua mapema kuwa Mkapa angebadilika na kuwa fisadi. Watu wengi waliokuwa karibu na Mwalimu, including Salim, ni wanafiki. Walijua Mwalimu hapendi hiki hapendi kile kwa hiyo nao wakapretendkuwa hawako hivi hawako vile. Lowassa alikuwa fisadi tangu utotoni. Lakini alijua kuficha makucha yake. Hawa mbwa mwitu wa CCM wote walijua kuficha makucha yao. Ndo maana niliondoka CCM baada ya Mwalimu kufariki.
 
CCM ya Nyerere (CCM-NY) sio ya Mwinyi (CCM-MW), Mkapa (CCM-MK) wala Kikwete (CCM-KI)! Ile ya Nyerere iliongozwa na Azimio la Arusha lililokuwa na Miiko ya Uongozi! Kwenye CCM-NY hakuna aliyethubutu kujilimbikizia mali isivyo halali! Mwenye mali hakuruhusiwa kugombea uongozi wa CCM-NY! CCM-MW ilifuta Azimio la Arusha, madirisha yasiyo na nyavu ya kiuchumi yalifunguliwa! Kwa hiyo upepo "mzuri" wa kiuchumi uliruhusiwa lakini kwa kuwa hakukuwa na nyavu pia mbu, vumbi, wadudu wa bidhaa feki na bei rahisi walimaliza kabisa viwanda vyetu ambavyo havijanyanyuka hadi leo! Mpaka sasa we are consuming what we don't produce and we are producing what we don't consume! CCM-MW ilimzaa CCM-MK ambaye iliendekeza mno wezi ambao walipewa jina "zuri" la wawekezaji! Ukiongea jambo baya juu ya mwekezaji unaonekana wewe sio mzalendo! Wizi huu ulizaa ufisadi! CCM-MK iliwalea mno mafisadi na ukiongea vibaya juu ya mafisadi unaambiwa wewe ni "mvivu wa kufikiri" au "una wivu wa kike!" CCM-KI inaendeshwa kisanii: hakuna mipango yoyote zaidi ya ile iliyokuwapo ya kuingia Ikulu! Baada ya kuingia hawajajua wafanye nini! Usanii unaendelea kila nyanja: kwenye mapambano dhidi ya ufisadi wengine wanatakiwa wapumzike, wakati baadhi wanashtakiwa! Wengine wanapewa muda wa kurudisha hela walizoiba, wengine wanafunguliwa mashtaka bila kupewa huo muda! CCM-KI ni nyepesi mno kuona matatizo lakini ni nzito mno kuchukua hatua, imejaa woga na kuoneana haya! CCM hii inaonekana haina central command, kila mtu ni msemaji! Migawanyiko, vijembe, matusi, kukashfiana ili kutafuta cheap popularity kila kona! Usipokuwa na vijisenti kwenye CCM-KI sahau kabisa kuchukua fomu ya kugombea uongozi, utaaibika! CCM-KI si Chama cha Wakulima na Wafanyakazi: Ni Chama Cha Wafanyabiashara! Ukiambiwa CCM ina wenyewe, they always mean what they say, and say what they mean!
 
Nyerere alionyesha sana wasiwasi kwa Lowasa na akawaaminisha Watanzania wakatambua hilo. Lakini tokea Lowasa aanze kujijenga kuingia kwenye Uwaziri mpaka alikofikia angalia sasa yanayotokea mpaka inafikia ni sisi wenyewe wa kujilaumu.
 
Jamani kila karne na zama zake. sasa hatuwezi kulinganisha chumvi na sukari. Enzi za JKN kulikuwa chama kimoja na sasa vyama vingi. Hivyo ni bora tubadilike kulingana na mazingira.
 
Wote mafisadi wa Mawazo. wizi mtupu. hamna hoja. labdamnieleze namna ya kwenda mbele na nione daliliza kwenda mbele. Maneno tupu na mnajifanya mnajua sana. kwendeni zenu.Kazi kupanga mipango ya kwendA NYUMA.
 
Back
Top Bottom