Elections 2010 Nyie viongozi hebu onyesheni kujali basi mnaowaongoza

Elections 2010 Nyie viongozi hebu onyesheni kujali basi mnaowaongoza

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Hebu angalia hiyo picha hapo chini. Ona hao watoto walivyorundikana humo darasani. Ona walivyobanana kwenye hayo madawati. Angalia hao walio sakafuni.
Wengine wameinama sijui hata kwa nini. Labda migongo inawauma.

Jamani hivi sisi ni majuha kiasi cha kushindwa hata kutengeneza mazingira yenye ahueni ambayo wanetu watasoma bila kuteseka? Sitaki kuamini tu majuha kiasi hicho lakini sina jinsi. Watu gani wenye akili wataruhusu watoto wao wasomee kwenye mazingira kama hayo? Nyambaaaf kabisa.

Hivi kujenga madarasa mazuri yenye kupendeza na yenye viti au madawati ya kutosha ni sawa kweli na kutengeneza maroketi ya kwenda angani na huko kwenye sayari zingine? Ni wazi jibu hapo si sawa. Sasa unahitaji uwe na akili kiasi gani ili uweze kuboresha mazingira ya kusomea wanao? Hakika huhitaji akili kama za kutengeneza maroketi.

Sayansi ya maroketi ni fani iliyo changamani (complicated) zaidi na yenye kuhitaji umakini wa hali ya juu. Ugumu wa kujenga shule nzuri zenye vifaa vya kutosha uko wapi? Nielezeni mwenzenu maana nimefikiria weee hadi nimeanza kuona kizunguzungu. Sioni ugumu uko wapi lakini naona ni wazi kuwa hatuwezi. Nazidi kuchanganyikiwa kabisa.

Sisi ni watu wa ajabu sana. Viongozi wetu wanaishi maisha ya hali ya juu sana. Wanajifanya wanajali watu wawaongozao. Waongo wakubwa hao. Hawajali chochote. Wangekuwa wanajali walahi tena hali kama za hili darasa hapo chini zisingekuwepo.

Kazi kusafiri na kununua magari ya bei mbaya kila kukicha. Hawaishi kutumia mihela kibao (mibilioni) kufanyia 'ukarabati' makazi yao yenye mabwawa ya kuogelea huku kuna watoto wa shule wanakalia sakafuni wakivuta na kupumua hewa yenye mavumbi. Ni utu kweli huu?

Badilikeni nyie watawala. Kuweni na mioyo ya kibinadamu. Sio vizuri kuishi maisha ya anasa kwa kutumia hela za walipa kodi walio masikini huku mkiwaacha hao walipa kodi waishi kama si binadamu. Wajalini watu mnaowaongoza.


attachment.php
 
Nyani.. nasikitika kukutaarifu kuwa hali hiyo haitokani kabisa na uongozi uliopo madarakani; hii inatokana na mapenzi ya mungu kwetu. Wazazi wa watoto hao na jamii inayowazunguka haihusishi hicho kilichopo mbele yetu na utawala ulioko madarakani. Ukiwauliza CCM hiki ni nini watatuambia kuwa ni "changamoto bado zipo". Hapa ndipo Ilani ya Chadema iko very specific:

a. Inalitambua tatizo hili:

.. Shule za umma zimetelekezwa (bado kuna maelfu ya watoto wetu wanaokaa kwenye matofali na kwenye mavumbi), walimu wanadhalilishwa kiasi hata cha kuchapwa viboko, na hakuna wa kuwatetea. ..

Na tena,

Watoto wanaosoma katika shule za serikali wanasoma katika mazingira magumu sana. Kwenye shule kadha wa kadha za bweni na za kutwa lishe bado ni tatizo na ni duni. Matokeo yake wazazi wenye uwezo wanalazimika kuwapeleka watoto wao katika shule za binafsi, ambazo ni chache na ghali. Matokeo yake tumetengeneza ubaguzi katika mfumo wa elimu kati ya shule binafsi na za serikali. Hali hii ni hatari kwa mustakabali wa taifa kwa muda mrefu ujao.

na wanasema hivi katika kushughulikia hili:

· Kuimarisha shule za umma ili zitoe elimu bora. Hili litafanywa kwa kuanzisha kampeni ya kujenga upya, kukarabati na kuzipatia shule zote nchini huduma muhimu za jamii hasa maji safi na umeme
.



CCM nayo ina mipango yake kuhusu masuala haya haya. Kubwa ni nani anaweza kuaminiwa?



lLakini CC
 
Dah! Hivi niko peke yangu tu ninayeumia nikiona mateso wanayopata watoto wa shule (hasa zile za umma)?
 
Mimi wanaonishangaza ni wananchi. Wanawajali viongozi lakini viongozi hawawajali wao.
Kulikuwa hakuna umuhimu wowote wa kujenga Twin Towers,dola milioni 320(kama sijakosea) zingeweza kukarabati shule zote za serikali na kuweka madawati .Sisi wapiga kura tunachangia kwa kiasi kikubwa kwa watoto wetu kukaa chini.
 
Nilipochoka zaidi ni pale aliposomea computer kwa kila mwanafunzi.
Naona jk kila wakati anapoongea kama vile yupo ndotoni vile. Kashindwa kubandika maji ya uji jikoni huku akiwatangazia walaji kua soon ugali utakua mezani. He he he he...jamaa mweupe akilini kinoma
 
Mkuu Ngabu, kwa miaka zaidi ya 45 CCM imewafanya Watanzania kuwa Wajinga, Imewafanya Watanzania kuwa Duni mbele ya Viongozi wao, wasioweza kuhoji mabaya wanayotendewa au kudai haki wanzonyimwa na sasa CCM inawekeza katika huo Ujinga, Hakuna Mrombo asiyejua Wizi wa Mramba, Hakuna Mmasai asiyejua Wizi wa Lowasa, Hakuna Mnyamwezi asiyejua Uporaji wa Rostam, Hakuna Msukuma asiyejua source ya Vijisent vya Chenge , kibaya Zaidi hawa waheshimiwa wanaweza kurudi Bungeni kwa Kishindo, katika Ule Umati wa Jangwani wapo Wazazi ambao Watoto wao wanakaa chini shule na wapo watu ambao hawana hata uhakika wa mlo mmoja lakini Wajinga ndio Wavunwao na waliwao
 
Nilipochoka zaidi ni pale aliposomea computer kwa kila mwanafunzi.

Mpaka ifike oct 30 utakuwa umezimia si kuchoka ndugu yangu. Kwani hukumbuki juzi kaahidi uwanja wa ndege kama ''Heathrow'' kule kigoma wakati huo huo anaazima vichwa vya treni kutoka punjab, na ameshindwa kuweka kokoto reli aliyoacha mjerumani.!!!
Miaka 50 bado watu wanavaa njano na kijani na vipeperushi. Kama kuna uchawi basi CCM wanakiboko!
 
Mpaka ifike oct 30 utakuwa umezimia si kuchoka ndugu yangu. Kwani hukumbuki juzi kaahidi uwanja wa ndege kama ''Heathrow'' kule kigoma wakati huo huo anaazima vichwa vya treni kutoka punjab, na ameshindwa kuweka kokoto reli aliyoacha mjerumani.!!!
Miaka 50 bado watu wanavaa njano na kijani na vipeperushi. Kama kuna uchawi basi CCM wanakiboko!

Hivi ni kwa Msaada wa Nchi gani vile maana Ahadi Nyingi ni kwa Msaada wa Wajomba zetu
 
Hivi ni kwa Msaada wa Nchi gani vile maana Ahadi Nyingi ni kwa Msaada wa Wajomba zetu

Sina uhakika lakini nadhani ni Jamica, alikuwa huko hivi karibuni. Kama si hao basi yaweza kuwa Bhutan,Haiti au Fiji na Tonga.
 
Wadau.... mitanzania ndivyo tulivyo!!!

Tutaamka, tutavaa khanga na tisheti, tutabandika mapicha kila sehemu (hata makaburini utadhani waliolala kwa amani na wataamaka kupiga kura), tutaimba, tutasubiri VX V8 zije, tumshangilie mgombea na kisha turudi nyumbani kuhangaikia ugali na 1/8 kilo ya maharage kwa familia zetu za watu saba

tuna laana ya kutohoji, ukihoji wewe hufai, ukihoji wewe ni mdhambi!!!

Tuna matatizo genetically i guess

Mitanzania ndivyo ilivyo NN na wewe na mimi ni watanzania
 
Wadau.... mitanzania ndivyo tulivyo!!!

Tutaamka, tutavaa khanga na tisheti, tutabandika mapicha kila sehemu (hata makaburini utadhani waliolala kwa amani na wataamaka kupiga kura), tutaimba, tutasubiri VX V8 zije, tumshangilie mgombea na kisha turudi nyumbani kuhangaikia ugali na 1/8 kilo ya maharage kwa familia zetu za watu saba

tuna laana ya kutohoji, ukihoji wewe hufai, ukihoji wewe ni mdhambi!!!

Tuna matatizo genetically i guess

Mitanzania ndivyo ilivyo NN na wewe na mimi ni watanzania

Mimi hapo ndo huwa nashangaa... mtu akishapewa Kofia na T-shirt na Khanga yuko radhi kutembea some kilometers akipigwa jua na vumbi kushangilia ujinga... then anarudi nyumbani hana hata mlo wa usiku. Sijui hii laana ilitoka wapi...
 
kwakweli inasikitisha sana na Taifa linazidi kupotea na kudevelop matabaka baina ya wananchi wake, Hivi Serikali iliopo madarakani kwa muda mrefu, imewahi kukaa na kujiuliza kwa umakini na kuona huruma katika hili? tunategemea viongozi gani wajao? ni hatari.
 
Mimi hapo ndo huwa nashangaa... mtu akishapewa Kofia na T-shirt na Khanga yuko radhi kutembea some kilometers akipigwa jua na vumbi kushangilia ujinga... then anarudi nyumbani hana hata mlo wa usiku. Sijui hii laana ilitoka wapi...
we si umesikia ahadi kemkem anazotoa jamaa kila akiamka... utafikiri kapagawa na ahadi!!!

but do you know why he does that??? i know... ITS BECAUSE HE WILL NOT COME BACK TO DEFEND WHAT HE PROMISED, HE IS IN HIS LAST TERM, AND THAT IS WHERE WE NEED TO CHALLENGE HII YA TWO TERM KWANI SASA IMEKUA ROUTINE NA USELESS FOR OUR BELOVED COUNTRY
 
Mimi hapo ndo huwa nashangaa... mtu akishapewa Kofia na T-shirt na Khanga yuko radhi kutembea some kilometers akipigwa jua na vumbi kushangilia ujinga... then anarudi nyumbani hana hata mlo wa usiku. Sijui hii laana ilitoka wapi...

Inawezekana kabisa kuwa hata mahitaji yetu wenyewe hatuyajui/tumeyasahau!
 
Wana JF,

Mimi Husema hizi zote ni njaaaa zetu sie watanzania kweli T-shirt, Kofia, Kanga na 2000/=Tsh ndio zinatukaanga kila baada ya miaka 5 na wanowaharibu kabisa wadanganyika ni wale viongozi wa shina,matawi,kata mabalozi wao ndio huwa wana mislead wadanganyika na wanadanganyika haswaa ati esp huko vijijini makwetu huko tutokeako na kunadaiwa kura hupigwa nyingi kuliko lakini wao ndo wanakuwa wamwisho kujali sijui na wao watazinduka lini ukienda unakuta kaya kadhaa zimeisha kuwa na msimamo mmoja kama eg ni Getruda Mongella basi hata utoke mkasika(Murutunguru) kwenda Ukara huwezi wabadilisha hawa watu na hii ni sumu iliyo sambazwa na waha waha makada wa CCM eg katibu wa kata siju mweka haziana na mabalozi wa CCM. Tunako kwenda ni kubaya sana tunajipotosha vibaya na hizi siasa


KAMA SIASA NI MCHEZO MCHAFU KWANINI WANATAKA KURA ZETU ???? NA KAMA SIASA SIO MCHEZO MCHAFU KWANINI HAWA VIONGOZI SI WAKWELI????
 
Back
Top Bottom