Hatimae mechi za Kimataifa zimekamilika, na yafuatayo ni maelezo juu ya performance za wachezaji wa Simba SC waliokua wakitumikia mataifa yao;
1. Emanuel Anord Okwi
Huyu jamaa kacheza mechi zote 2.. Kafunga goli 2, assist 2, kasababisha penalty pia alikua man of the match katika mechi 1.
2. Juuko Murshid
Beki huyu kisiki kacheza mechi 2.. Na kaisaidia timu yake ya Taifa ya Uganda kushinda mechi zote, huku akihakikisha timu haifungwi goli lolote.
3. Clatous Chota Chama
Kiungo bora kabisa kuwahi kushuhudiwa nchini Zambia, alicheza nae mechi zote 2. Aliasist goli 1 huku akiibuka man of the match katika mechi 1.
4. Haruna Niyonzima
Kiungo huyu machachari toka nchini Rwanda, aliitumikia nchi yake katika mechi 2.. Huku akiasist goli 1.
5. Meddie Kagere
Goal Machine, MK14 pamoja na mabeki kumkamia sana.. Aliasist goli 1 katika mechi 2 alizocheza.
CONCLUSION:
Kwa viwango walivyoonesha hawa wachezaji katika kipindi hiki, ama kweli bara la Africa lilitikisika.
Tukutane next time. Ahsanteni.